< Daniel 4 >

1 Le roi Nabuchodonosor dit à tous les peuples, à toutes les tribus, à tous les hommes de langues diverses: Que la paix se multiplie parmi vous.
Mfalme Nebukadneza, Kwa kabila za watu, mataifa na watu wa kila lugha, wanaoishi katika ulimwengu wote: Mafanikio yawe kwenu sana!
2 Les signes et les prodiges que vient d'accomplir devant moi le Dieu très- haut, il me plaît de vous annoncer en personne
Ni furaha yangu kuwaambia kuhusu ishara za miujiza na maajabu ambayo Mungu Aliye Juu Sana amenifanyia.
3 Combien ils sont grands et irrésistibles; son royaume est le royaume éternel, et sa puissance s'étend de génération en génération.
Ishara zake ni kuu aje, na maajabu yake yana nguvu aje! Ufalme wake ni ufalme wa milele; enzi yake hudumu kutoka kizazi hadi kizazi.
4 Moi, Nabuchodonosor, comme j'étais en paix et florissant dans mon palais,
Mimi, Nebukadneza, nilikuwa nyumbani katika jumba langu la kifalme, nikiwa ninaishi kwa raha na hali ya kufanikiwa.
5 J'eus un songe, et il m'effraya, et je fus troublé sur ma couche, et les visions de ma tête me troublèrent.
Niliota ndoto iliyoniogopesha. Nilipokuwa nimelala kitandani mwangu, njozi na maono yaliyopita mawazoni mwangu vilinitisha.
6 Et, de moi-même, je donnai ordre d'amener en ma présence tous les sages de Babylone, et qu'ils me fissent connaître l'interprétation de mon songe.
Hivyo nikaagiza kwamba watu wote wenye hekima wa Babeli waletwe mbele yangu kunifasiria ndoto yangu.
7 Et les devins et les mages, les sorciers et les Chaldéens arrivèrent, et je dis mon songe devant eux, et ils ne m'en firent pas connaître l'interprétation;
Walipokuja waganga, wasihiri, wanajimu na waaguzi, niliwaambia ndoto yangu, lakini hawakuweza kunifasiria.
8 Jusqu'à ce que vint Daniel, que l'on nommait Baltasar, selon le nom de mon dieu, et qui avait en lui l'Esprit-Saint de Dieu, et je lui dis:
Mwishoni, Danieli alikuja mbele yangu nikamweleza hiyo ndoto. (Danieli anaitwa Belteshaza, kwa jina la mungu wangu, nayo roho ya miungu mitakatifu inakaa ndani yake.)
9 Baltasar, comme chef des devins, je sais que l'Esprit-Saint de Dieu est en toi, et que nul mystère pour toi n'est impénétrable; écoute donc la vision de mon songe, et dis-m'en l'interprétation.
Nilisema, “Belteshaza, mkuu wa waganga, ninajua kuwa roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, wala hakuna siri iliyo ngumu kwako. Hii ndiyo ndoto yangu, nifasirie.
10 Je regardais sur ma couche, et voilà qu'un arbre était au milieu de la terre, et sa hauteur était grande.
Haya ndiyo maono niliyoona nilipokuwa nimelala kitandani mwangu: Nilitazama, na mbele yangu ulisimama mti katikati ya nchi. Ulikuwa mrefu sana.
11 Il crût encore et se fortifia, et sa cime arrivait jusqu'au ciel, et son tronc jusqu'aux extrémités de la terre.
Mti ule ulikua, ukawa mkubwa na wenye nguvu, nayo ncha yake ikagusa anga; ulionekana mpaka miisho ya dunia.
12 Ses feuilles étaient belles, et ses fruits abondants; et l'aliment de tous les êtres se trouvait en lui; sous son ombre s'abritaient les bêtes sauvages, et sur ses rameaux les oiseaux du ciel faisaient leurs nids, et de lui toute chair se nourrissait.
Majani yake yalikuwa ya kupendeza, matunda yake yalikuwa mengi, na juu yake kulikuwa na chakula kwa ajili ya wote. Chini ya kivuli chake wanyama wa kondeni walipata hifadhi, na ndege wa angani waliishi katika matawi yake. Kila kiumbe kililishwa kutokana na mti huo.
13 J'étais attentif sur ma couche à cette vision de la nuit, et voilà qu'un veillant et un saint descendit des cieux.
“Katika maono niliyoyaona nikiwa nimelala kitandani mwangu, nilitazama, na mbele yangu alikuwepo mlinzi, aliye mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni.
14 Et, parlant à haute voix, il dit: Abattez l'arbre, arrachez ses rameaux, secouez ses feuilles, et dispersez ses fruits; que les bêtes soient chassées de dessous lui, et les oiseaux du ciel de ses branches.
Akaita kwa sauti kubwa: ‘Kateni mti huu, myafyeke matawi yake; yaondoeni majani yake na kuyatawanya matunda yake. Wanyama na wakimbie kutoka chini yake na ndege waondoke kutoka matawi yake.
15 Cependant laissez en terre la souche de ses racines; quant à lui, qu'il reste étendu en des chaînes de fer et d'airain, parmi l'herbe qui l'entoure, à la rosée du ciel; et qu'avec les bêtes il ait sa part de l'herbe de la terre.
Lakini acheni kisiki chake na mizizi, kikiwa kimefungwa kwa chuma na shaba, kibaki ardhini, kwenye majani ya kondeni. “‘Mwacheni aloweshwe na umande wa mbinguni, naye aachwe aishi pamoja na wanyama miongoni mwa mimea ya dunia.
16 Son cœur deviendra différent du cœur des hommes; et un cœur de bête lui sera donné; et sept fois les temps changeront sur lui.
Akili yake na ibadilishwe kutoka ile ya mwanadamu na apewe akili ya mnyama, mpaka nyakati saba zipite juu yake.
17 Telle est la sentence du veillant et la parole des saints, afin que les vivants sachent que le Seigneur est le dominateur du royaume des hommes, et qu'il le donne à qui bon lui semblera, et qu'il élèvera pour le gouverner celui qui est en mépris parmi les hommes.
“‘Uamuzi huu umetangazwa na walinzi, hukumu imetangazwa na watakatifu, ili walio hai wajue kuwa Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme zote za wanadamu, naye humpa yeyote amtakaye na kumtawaza juu yake hata yeye aliye mnyonge sana miongoni mwa wanadamu.’
18 Tel est le songe que j'ai eu, moi, le roi Nabuchodonosor, et toi, Baltasar, dis-m'en l'interprétation; car nul des sages de mon royaume ne peut me la donner; mais toi, Daniel, tu le peux, parce que l'Esprit-Saint de Dieu est en toi.
“Hii ndiyo ndoto niliyoipata mimi, Mfalme Nebukadneza. Sasa Belteshaza, niambie maana yake, kwa maana hakuna hata mmoja wa wenye hekima katika ufalme wangu anayeweza kunifasiria. Bali wewe waweza, kwa sababu roho ya miungu mitakatifu imo ndani yako.”
19 Alors Daniel, surnommé Baltasar, réfléchit environ une heure, et ses pensées le troublèrent. Enfin Baltasar répondit: Seigneur, dit-il, que ton songe soit pour ceux qui te haïssent, et son interprétation pour tes ennemis!
Ndipo Danieli (aliyeitwa pia Belteshaza) alipofadhaika sana kwa muda, nayo mawazo yake yakamtia hofu. Basi mfalme akasema, “Belteshaza, usiruhusu ndoto wala maana yake kukutia hofu.” Belteshaza akamjibu, “Bwana wangu, laiti ndoto hii ingehusu adui zako, na maana yake iwahusu watesi wako!
20 L'arbre que tu as vu grand et fort, dont la cime allait au ciel, et le tronc sur toute la terre;
Mti uliouona, uliokua ukawa mkubwa na wenye nguvu, nayo ncha yake ikagusa anga na kuonekana duniani kote,
21 Dont les feuilles étaient florissantes et les fruits abondants, en qui se trouvait l'aliment de tous, et sous lequel s'abritaient les bêtes sauvages, tandis que les oiseaux du ciel faisaient leur nid dans ses rameaux;
ukiwa na majani ya kupendeza na matunda mengi, ukitoa chakula kwa wote, na ukiwapa hifadhi wanyama wa kondeni na kuwa mahali pa viota katika matawi yake kwa ajili ya ndege wa angani.
22 Cet arbre, ô roi, c'est toi-même; car tu as grandi et tu t'es fortifié, et ta grandeur n'a cessé de croître, et elle est allée jusqu'au ciel, et ta domination jusqu'aux extrémités de la terre.
Ee mfalme, wewe ndiwe ule mti! Umekuwa mkubwa na mwenye nguvu, nao ukuu wako umekua mpaka kufika juu angani, nayo mamlaka yako yameenea mpaka miisho ya dunia.
23 Or quand le roi a vu le veillant et le saint descendre du ciel, et que le saint a dit: Arrachez l'arbre, détruisez-le, mais laissez en terre la souche de ses racines; quant à lui, qu'il reste étendu en des chaînes de fer et d'airain, parmi l'herbe qui l'entoure, exposé à la rosée du ciel, et qu'il partage avec les bêtes l'herbe des champs, jusqu'à ce que les temps aient changé sept fois sur lui:
“Ee mfalme, wewe ulimwona mlinzi, aliye mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni na kusema, ‘Ukateni mti na kuuangamiza, lakini kiacheni kisiki kikiwa kimefungwa kwa chuma na kwa shaba, kwenye majani ya kondeni, wakati mizizi yake inabaki ardhini. Mwacheni aloweshwe na umande wa mbinguni, mwacheni aishi kama wanyama pori mpaka nyakati saba zipite juu yake.’
24 Voici ce que cela signifie, ô roi, et c'est la sentence du Très-Haut, qui d'avance vient avertir le roi mon maître.
“Ee mfalme, hii ndiyo tafsiri, na hii ni amri ya Aliye Juu Sana aliyoitoa dhidi ya bwana wangu mfalme:
25 On t'exclura du commerce des hommes, et ta demeure sera parmi les bêtes sauvages, et l'on te donnera ta part de fourrage comme à un bœuf, et tu passeras les nuits à la rosée du ciel, et les temps changeront sept fois sur toi, jusqu'à ce que tu reconnaisses que le Très Haut est le maître du royaume des hommes, et qu'il le donne à qui bon lui semble.
Wewe utafukuzwa mbali na wanadamu, nawe utaishi pamoja na wanyama pori; utakula manyasi kama ngʼombe, na kuloana kwa umande wa mbinguni. Nyakati saba zitapita juu yako, mpaka utakapokubali kuwa Yeye Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye humtawaza yeyote amtakaye.
26 Et puisqu'il a été dit: Laissez en terre la souche des racines de l'arbre, ta royauté subsistera, après que tu auras reconnu la puissance du ciel.
Amri ya kuacha kisiki pamoja na mizizi yake inamaanisha kwamba ufalme wako utarejezwa kwako utakapokubali kwamba Mbingu ndizo zitawalazo.
27 C'est pourquoi, ô roi, que mon conseil te soit agréable; rachète tes péchés par des aumônes, et tes iniquités par la compassion pour les indigents, et Dieu peut-être sera longanime à tes offenses.
Kwa hiyo, ee mfalme, uwe radhi kupokea shauri langu: Acha dhambi zako kwa kutenda yaliyo haki, ukaache uovu wako, na uwe na huruma kwa walioonewa. Hivyo itawezekana baada ya hayo, mafanikio yako yakaendelea.”
28 Or les choses suivantes arrivèrent au roi Nabuchodonosor:
Haya yote yalimpata Mfalme Nebukadneza.
29 Après le douzième mois, comme il se promenait dans son palais royal, en Babylone,
Miezi kumi na miwili baadaye, mfalme alipokuwa akitembea juu ya paa la jumba la kifalme la Babeli,
30 Le roi prit la parole, et dit: N'est-ce point là Babylone la grande, que j'ai bâtie pour être ma résidence royale, dans ma force et ma puissance, en l'honneur de ma gloire?
alisema, “Je, huu si Babeli mji mkuu nilioujenga kama makao ya kifalme, kwa uwezo wangu mkubwa, na kwa ajili ya utukufu wa enzi yangu?”
31 Cette parole était encore dans la bouche du roi, quand une voix vint du ciel, disant: À toi, roi Nabuchodonosor, il est dit: Ton royaume t'échappe.
Maneno hayo yalikuwa bado katika midomo yake wakati sauti ilipokuja kutoka mbinguni, ikisema, “Mfalme Nebukadneza, hiki ndicho kilichoamriwa kwa ajili yako: Mamlaka yako ya ufalme yameondolewa kutoka kwako.
32 On va te chasser loin des hommes, et ta demeure sera parmi les bêtes sauvages; on te donnera du foin comme à un bœuf, et les temps changeront sept fois sur toi, jusqu'à ce que tu reconnaisses que le Très-Haut est le maître du royaume des hommes, et qu'il le donnera à qui bon lui semble.
Utafukuzwa mbali na wanadamu, ukaishi pamoja na wanyama pori, na utakula manyasi kama ngʼombe. Nyakati saba zitapita juu yako, mpaka utakapokubali kuwa Yeye Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye humtawaza yeyote amtakaye.”
33 À l'heure même, cette parole sur Nabuchodonosor s'accomplit: il fut chassé loin des hommes, il mangea de l'herbe comme un bœuf, et son corps fut baigné par la rosée du ciel, jusqu'à ce que ses cheveux eussent crû comme la crinière d'un lion, et ses ongles comme les griffes des oiseaux.
Papo hapo yale yaliyokuwa yamesemwa kuhusu Nebukadneza yakatimia. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akala majani kama ngʼombe. Mwili wake uliloweshwa kwa umande wa mbinguni mpaka nywele zake zikakua kama manyoya ya tai na kucha zake kama makucha ya ndege.
34 Et à la fin des jours moi, Nabuchodonosor, je levai les yeux au ciel, et les pensées me revinrent, et je bénis le Très-Haut, et je louai l'Éternel, et je lui rendis gloire, parce que sa puissance est inébranlable, et son royaume pour toutes les générations.
Mwisho wa huo wakati, mimi Nebukadneza, niliinua macho yangu kuelekea mbinguni, nazo fahamu zangu zikanirudia. Ndipo nikamsifu Yeye Aliye Juu Sana, nikamheshimu na kumhimidi yeye aishiye milele. Utawala wake ni utawala wa milele; ufalme wake hudumu kutoka kizazi na kizazi.
35 Et tous ceux qui habitent la terre sont comptés pour rien. En l'armée du ciel et parmi les habitants de la terre, il fait à sa volonté, et nul ne peut résister à sa puissance, ni lui dire: Qu'avez-vous fait?
Mataifa yote ya dunia yanahesabiwa kuwa si kitu. Hufanya kama atakavyo kwa majeshi ya mbinguni, na kwa mataifa ya dunia. Hakuna anayeweza kuuzuia mkono wake au kumwambia, “Umefanya nini wewe?”
36 Au même instant les pensées me revinrent, et je rentrai dans les honneurs de ma royauté, et ma forme me fut rendue, et mes princes et mes grands me recherchèrent, et une plus grande magnificence me fut rendue.
Wakati huo huo fahamu zangu ziliponirudia, nikarudishiwa heshima yangu na fahari yangu kwa ajili ya utukufu wa ufalme wangu. Washauri wangu na wakuu wangu walikuja kunitafuta, nami nikarudishwa kwenye kiti changu cha ufalme hata nikawa mkuu kuliko mwanzoni.
37 Maintenant donc, moi, Nabuchodonosor, je louerai et j'exalterai, et je glorifierai le Roi du ciel, parce que toutes ses œuvres sont vraies, que ses sentiers sont la justice, et qu'il est en son pouvoir d'humilier tous ceux qui marchent dans leur orgueil.
Basi mimi, Nebukadneza, humhimidi, na humtukuza na kumsifu Mfalme wa mbinguni, kwa sababu kila kitu afanyacho ni haki, na njia zake zote ni adili. Nao waendao kwa kiburi anaweza kuwashusha.

< Daniel 4 >