< 2 Samuel 22 >

1 Et David chanta ce cantique au Seigneur, le jour où le Seigneur l'eut délivré de Saül et de tous ses ennemis.
Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
2 Et il dit, en ce cantique: Seigneur, mon rocher, ma forteresse, mon sauveur!
Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
3 Mon Dieu sera mon gardien, je me confierai à lui; mon protecteur, mon salut, mon refuge, vous me sauverez de l'homme inique.
Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
4 J'invoquerai le Seigneur, à qui appartient la louange, et il me délivrera de mes ennemis.
Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
5 Car les brisements de la mort m'ont investi, les torrents de l'iniquité m'ont frappé d'épouvante.
“Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
6 Les angoisses de la mort m'ont entouré, l'agonie de la mort a pris l'avance sur moi. (Sheol h7585)
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
7 Dans mes afflictions j'invoquerai le Seigneur, je crierai à mon Dieu; de son temple, il entendra ma voix, mes cris arriveront à ses oreilles.
Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
8 La terre a été troublée, et elle a tremblé; les fondements du ciel ont été bouleversés, et ils se sont déchirés, parce que la colère du Seigneur a éclaté contre la terre et le ciel.
“Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
9 Dans sa fureur une fumée s'exhale, le feu de sa bouche est dévorant; des charbons en ont été embrasés.
Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
10 Il a abaissé les cieux et il est descendu, et les ténèbres s'étendaient sous ses pieds.
Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
11 Et il s'est assis sur les chérubins, et il a pris son essor, et il s'est montré sur les ailes des vents,
Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
12 Et il s'est voilé de ténèbres. Et autour de lui, comme un tabernacle, il a étendu l'obscurité des eaux, condensées dans les nuées de l'air.
Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
13 Et les lueurs qui le précédaient ont mis des charbons en feu.
Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
14 Le Seigneur a tonné du haut du ciel, le très Haut a fait retentir sa voix.
Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
15 Il a lancé des traits et il a dispersé mes ennemis; il a fait tomber la foudre et il les a mis hors d'eux-mêmes.
Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
16 Aux reproches du Seigneur, sous le souffle de sa colère, on a vu les gouffres de la mer, et les bases de la terre ont apparu.
Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
17 Et il a envoyé d'en haut son ange, et il m'a pris, et il m'a tiré du tumulte des eaux.
“Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
18 Il m'a délivré de la force de mes ennemis, de ceux qui me haïssaient et qui l'emportaient sur moi.
Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
19 Les jours de mon affliction s'étaient précipités sur moi; mais le Seigneur a été mon appui;
Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
20 Il m'a conduit dans de libres espaces, et il m'a affranchi, parce qu'il se complaisait en moi.
Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
21 Le Seigneur m'a rétribué selon ma justice; il m'a rétribué selon la pureté de mes mains.
“Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
22 Parce que j'ai suivi les voies du Seigneur, et que je n'ai point outragé mon Dieu.
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
23 Parce que ses jugements et ses justices ont toujours été devant moi, et que je ne m'en suis jamais écarté.
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
24 Je serai sans tache à ses yeux, et je me tiendrai en garde contre mes dérèglements.
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
25 Le Seigneur me rétribuera selon ma justice, et selon la pureté de mes mains devant ses yeux.
Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
26 Avec le saint vous serez saint, avec l'homme accompli vous serez accompli.
“Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
27 Avec l'excellent vous serez excellent, avec le méchant vous serez méchant.
kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
28 Vous sauverez le peuple pauvre, et vous ferez baisser les yeux des superbes.
Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
29 Car, ô Seigneur, vous êtes ma lumière, et le Seigneur brillera devant moi dans mes ténèbres.
Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
30 Avec votre aide je courrai comme un homme fort; avec l'aide de mon Dieu je franchirai des remparts.
Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
31 Le Tout-Puissant, ses voies sont irréprochables; la parole du Seigneur est forte, éprouvée par le feu. Le Seigneur abrite tous ceux qui ont foi en lui.
“Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
32 Qui donc est fort, hormis le Seigneur? Qui donc sera créateur, hormis notre Dieu?
Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
33 Le Tout-Puissant, c'est lui qui me fortifie par sa puissance, et qui m'a préparé une voie irréprochable.
Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
34 Il rendu mes pieds légers comme ceux des cerfs; il m'a placé sur les hauts lieux.
Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
35 Vous avez exercé mes mains aux combats; vous avez brisé par mon bras un arc d'airain.
Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
36 Vous m'avez donné, Seigneur, le bouclier qui me sauve; mon obéissance à vos ordres m'a grandi.
Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
37 L'espace sous mes pas s'est étendu, et mes jambes ont conservé leur fermeté.
Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
38 Je poursuivrai mes ennemis, et je les effacerai, et je ne reviendrai point qu'ils ne soient anéantis.
“Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
39 Je les briserai, et ils ne se relèveront point; ils tomberont sous mes pieds.
Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
40 Et vous, par votre puissance, vous me fortifierez, Seigneur, pendant la bataille, et vous courberez sous moi ceux qui contre moi se sont levés.
Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
41 Vous m'avez fait voir le dos de mes ennemis, vous avez mis à mort ceux qui me haïssaient.
Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
42 Ils n'ont plus de secours; ils crieront au Seigneur, mais le Seigneur ne les exaucera plus.
Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
43 Je les ai broyés comme de la poussière; je les ai aplatis comme la boue du chemin.
Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
44 Vous me préserverez, ô Seigneur, des contradictions des peuples; et vous me maintiendrez à la tête des nations; un peuple que je ne connaissais pas m'a été asservi;
“Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
45 Les fils des étrangers m'avaient trompé; ils ont ouï votre parole, et ils m'ont été dociles.
nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
46 Les fils des étrangers seront rejetés avec mépris, et ils trébucheront dans leurs places de retraite.
Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
47 Vive le Seigneur! béni soit mon gardien, et Dieu, le gardien de mon salut, sera glorifié.
“Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
48 Le Seigneur qui m'a vengé, en châtiant par mon bras les nations, est tout-puissant.
Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
49 Il m'a tiré de leurs mains; vous m'élèverez encore, ô Seigneur, au- dessus de ceux qui se lèveront contre moi, vous me défendrez contre les hommes violents.
aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
50 A cause de cela, Seigneur, je vous rendrai gloire parmi toutes les nations, et je chanterai votre nom,
Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
51 O vous, qui rendez grand le salut de votre roi, qui êtes miséricordieux envers David, votre christ, et envers sa postérité à jamais!
Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”

< 2 Samuel 22 >