< 2 Chroniques 4 >

1 Et il fit un autel d'airain, long de vingt coudées, large de vingt, haut de dix.
Mfalme Solomoni akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini, upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi.
2 Et il fit une mer, jetée en fonte, ronde, haute de cinq coudées, ayant dix coudées de diamètre, et trente coudées de circonférence.
Akatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathini ingeweza kuizunguka.
3 Il y avait, au-dessous de ses bords tout alentour, des figures de bœufs, et la piscine avait dix coudées de tour; on avait jeté en fonte deux espèces de bœufs, en deux sortes de moules,
Chini ya huo ukingo, kulikuwa na mafahali kuizunguka, yaani mafahali kumi katika kila dhiraa moja. Hayo mafahali waliyasubu katika safu mbili yakiwa ya kitu kimoja na hiyo Bahari.
4 Où on avait fait douze bœufs: trois regardant le nord, trois l'occident, trois le midi, trois l'orient; la mer était posée sur eux, et le derrière de leur corps était caché par elle.
Bahari hiyo ilikaa juu ya mafahali kumi na wawili, mafahali watatu walielekeza nyuso zao kaskazini, watatu magharibi, watatu kusini na watatu mashariki. Bahari hiyo ilikaa juu ya hao mafahali, nazo sehemu zao za nyuma zilielekeana.
5 Elle avait un palme d'épaisseur, et ses bords étaient comme ceux d'une coupe, et ciselés de fleurs de lis; elle contenait trois mille mesures; il l'acheva,
Unene wake ulikuwa nyanda nne, na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 3,000.
6 Et il fit dix bassins: il en plaça cinq à droite et cinq à gauche, pour qu'on y lavât la matière des holocaustes; quant aux prêtres, ils se lavaient dans la mer.
Kisha akatengeneza masinia kumi kwa ajili ya kuoshea vifaa, naye akayaweka matano upande wa kusini na matano upande wa kaskazini. Ndani yake ndimo walioshea vifaa vya kutumika katika sadaka za kuteketezwa, lakini ile Bahari ilikuwa ni kwa ajili ya makuhani kunawia.
7 Et il fit dix chandeliers d'or, selon le modèle, et il les plaça dans la nef: cinq à droite, cinq à gauche.
Akatengeneza vinara vya taa kumi vya dhahabu kama ilivyoainishwa kwao na kuviweka hekaluni, vinara vitano upande wa kusini na vitano upande wa kaskazini.
8 Et il fit dix tables, et il les plaça dans la nef: cinq à droite, cinq à gauche; et il fit cent fioles d'or.
Akatengeneza meza kumi na kuziweka hekaluni, tano upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Pia akatengeneza mabakuli 100 ya dhahabu ya kunyunyizia.
9 Il fil aussi le parvis des prêtres, le grand parvis, les portes du parvis, et il revêtit d'airain leurs panneaux.
Akatengeneza ukumbi wa makuhani na ukumbi mwingine mkubwa na milango yake, naye akaifunika hiyo milango kwa shaba.
10 Il plaça la mer du côté droit du temple, vers l'angle regardant l'orient.
Akaweka ile Bahari upande wa kusini, kwenye pembe ya kusini mashariki ya nyumba.
11 Et Hiram fit les fourchettes, les poêles, la grille de l'autel et tous ses vases; et il acheva tous les travaux que lui avait commandés le roi Salomon pour le temple du Seigneur.
Pia akatengeneza masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi katika Hekalu la Mungu kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:
12 Il fit deux colonnes, et, sur leurs têtes, des cordons aux chapiteaux, et deux filets pour couvrir les deux chapiteaux des têtes de ces colonnes,
zile nguzo mbili; yale mataji mawili yaliyokuwa juu ya hizo nguzo, zile nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli yaliyowekwa juu ya zile nguzo;
13 Et quatre cents clochettes d'or dans les deux filets, et deux sortes de grenades dans chaque filet, pour couvrir les deux chapiteaux des têtes de colonnes.
yale makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);
14 Et il fit dix bassins, et il fit les cuvettes pour les bassins,
vishikio pamoja na masinia yake;
15 Et la mer, et les douze bœufs qui la supportent.
hiyo Bahari na hao mafahali kumi na wawili chini yake;
16 Et les vases pour les pieds, les seaux, les marmites, les crochets, et les autres vases qui lui étaient commandés; il les fit en airain pur, et il les apporta au roi dans le temple du Seigneur.
pia hayo masufuria, masepetu, uma za nyama na vyombo vingine vyote vilivyohusiana. Vitu vyote ambavyo Huramu-Abi alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyosuguliwa.
17 Le roi les avait jetés en fonte, dans la vallée du Jourdain, en une terre argileuse de la maison de Soccoth, entre cette ville et Saredatha.
Mfalme aliagiza wavisubu vitu hivi kwenye kalibu za udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani kati ya Sukothi na Sereda.
18 Et Salomon fit tous ces ustensiles à profusion, car l'airain ne put être épuisé.
Vitu hivi vyote Mfalme Solomoni alivyotengeneza vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.
19 Et il fit tous les vaisseaux du temple du Seigneur, l'autel d'or, les tables de proposition,
Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu: madhabahu ya dhahabu; meza za kuweka mikate ya Wonyesho;
20 Les chandeliers et les lampes en or pur, qui devaient éclairer la façade de l'oracle, selon son plan.
vinara vya taa vya dhahabu safi pamoja na taa zake ili ziwake mbele ya sehemu takatifu ya ndani kama ilivyoelekezwa;
21 Il fit leurs mouchettes, leurs récipients, les coupes, les réchauds et les encensoirs, d'or pur,
maua ya dhahabu yaliyofanyizwa, taa na makoleo (vilikuwa vya dhahabu bora kabisa);
22 Et la porte intérieure du temple qui mène au Saint des saints, et les portes d'or du temple.
mikasi ya dhahabu safi, mabakuli ya kunyunyizia, masinia na vyetezo; milango ya dhahabu ya Hekalu: yaani milango ya ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, na milango ya ukumbi mkuu.

< 2 Chroniques 4 >