< 1 Samuel 26 >

1 Après cela, des Ziphéens vinrent de la terre aride chez Saül à Gabaa, disant: Voilà que David est caché parmi nous sur la colline d'Echéla, en face de Jessème.
Hao Wazifu wakamwendea Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hakujificha katika kilima cha Hakila, kinachotazamana na Yeshimoni?”
2 Alors, Saül partit et descendit an désert de Ziph pour chercher David, avec trois mille hommes choisis en tout Israël.
Hivyo Sauli akashuka kwenda katika Jangwa la Zifu, akiwa na watu wake 3,000 wa Israeli waliochaguliwa, kumsaka Daudi huko.
3 Il campa sur la route en la colline d'Echéla, vis-à-vis Jessème, tandis que David demeurait dans le désert. Et David vit que Saül était venu pour le poursuivre dans le désert.
Sauli akapiga kambi yake kando ya barabara juu ya kilima cha Hakila kinachotazamana na Yeshimoni, lakini Daudi alikuwa anaishi huko jangwani. Alipoona kuwa Sauli amemfuata huko,
4 Et David envoya des éclaireurs, et il sut que Saül était arrivé en forces de Ceïla.
Daudi akatuma wapelelezi na akapata habari kwa hakika kwamba Sauli alikuwa amewasili.
5 Et David se leva sans bruit, et il se rendit au lieu où dormait Saül; il y avait là son général Abner, fils de Ner; Saül dormait sur un chariot couvert, ayant toute sa troupe campée autour de lui.
Ndipo Daudi akaondoka, akaenda hadi mahali Sauli alikuwa amepiga kambi. Akaona mahali Sauli na Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi, walipokuwa wamelala. Sauli alikuwa amelala ndani ya kambi, jeshi likiwa limemzunguka.
6 David s'adressant à Abimélech le Hettéen, et à Abessa, fils de Sarvia, frère de Joab, leur dit: Qui viendra avec moi dans le camp jusqu'à Saül? Et Abessa répondit: Moi, je t'accompagnerai.
Basi Daudi akamuuliza Ahimeleki Mhiti, na Abishai mwana wa Seruya, nduguye Yoabu, akisema, “Ni nani atakayeshuka pamoja nami kambini kwa Sauli?” Abishai akajibu, “Nitakwenda pamoja nawe.”
7 Et David avec Abessa se glissa parmi la troupe pendant la nuit. Saül dormait d'un profond sommeil sur un chariot couvert, sa javeline plantée en terre près de sa tête; Abner et ses gens dormaient autour de lui.
Hivyo Daudi na Abishai wakaenda kwenye jeshi wakati wa usiku, tazama Sauli, alikuwa amelala ndani ya kambi na mkuki wake umekitwa ardhini karibu na kichwa chake. Abneri na askari walikuwa wamelala kumzunguka Sauli.
8 Abessa dit à David: Le Seigneur aujourd'hui enferme ton ennemi dans tes mains; je vais à l'instant, d'un seul coup de javeline, le faire rouler à terre; je n'aurai pas besoin de le frapper deux fois.
Abishai akamwambia Daudi, “Leo Mungu amemtia adui yako mikononi mwako. Sasa niruhusu nimchome mpaka ardhini kwa pigo moja la mkuki wangu; sitamchoma mara mbili.”
9 Mais David dit à Abessa: Garde-toi de l'outrager; car qui peut sans crime porter la main sur l'oint du Seigneur?
Lakini Daudi akamwambia Abishai, “Usimwangamize! Ni nani awezaye kutia mkono juu ya mpakwa mafuta wa Bwana na asiwe na hatia?”
10 Et David ajouta: Vive le Seigneur! il ne mourra que quand le Seigneur le frappera, soit que son jour vienne et qu'il expire, soit qu'il succombe en combattant et aille rejoindre ses pères.
Daudi akasema, “Hakika kama vile Bwana aishivyo, Bwana mwenyewe atampiga; au wakati wake utafika, naye atakufa, au atakwenda vitani na kuangamia.
11 Que le Seigneur me préserve de porter la main sur l'oint du Seigneur; maintenant, prends à son chevet sa javeline et la fiole d'eau, puis allons- nous-en.
Lakini Mungu na apishie mbali nisije nikainua mkono juu ya mpakwa mafuta wa Bwana. Sasa chukua huo mkuki na hilo gudulia la maji vilivyo karibu na kichwa chake, tuondoke.”
12 Ainsi, David prit auprès du chevet la javeline et la fiole d'eau, et ils s'en allèrent. Nul ne les vit, nul ne sut qu'ils étaient là, nul ne s'éveilla; tous dormaient, car le Seigneur avait fait tomber sur eux une profonde torpeur.
Hivyo Daudi akachukua huo mkuki na hilo gudulia la maji vilivyokuwa karibu na kichwa cha Sauli, nao wakaondoka. Hakuna yeyote aliyeona au kufahamu habari hii, wala hakuna hata mmoja aliyeamka usingizini. Wote walikuwa wamelala, kwa sababu Bwana alikuwa amewatia kwenye usingizi mzito.
13 David traversa le camp, et il s'arrêta au loin, du côté opposé, sur la cime de la montagne; il y avait entre eux et lui un grand espace.
Kisha Daudi akavuka upande mwingine na kusimama juu ya kilima mahali palipokuwa na nafasi pana kati yao.
14 De là, David appela la troupe, et s'adressant à Abner, il dit: Ne répondras-tu point, Abner. Et Abner répondit, et il dit: Qui es-tu, toi qui appelles?
Daudi akalipigia kelele jeshi na Abneri mwana wa Neri, akisema, “Je, Abneri, hutanijibu?” Abneri akajibu, “Nani wewe umwitaye mfalme?”
15 Et David dit à Abner: N'es-tu pas un homme? Qui donc te vaut en Israël? Pourquoi ne gardes-tu pas le roi ton maître? Car quelqu'un du peuple est entré dans le camp pour le tuer.
Daudi akasema, “Wewe si ni mtu shujaa? Ni nani aliye kama wewe katika Israeli? Kwa nini basi hukumlinda mfalme bwana wako? Mtu mmoja alikuja kumwangamiza mfalme, bwana wako.
16 Ce n'est pas une bonne action que tu as faite là. Vive le Seigneur! vous êtes tous fils du meurtre, vous qui êtes commis à la garde du roi votre maître, l'oint du Seigneur. Maintenant, je te prie, la javeline du roi et la fiole d'eau qui étaient aussi auprès de son chevet, où sont-elles?
Ulichokifanya si kizuri. Kwa hakika kama aishivyo Bwana, wewe na watu wako mnastahili kufa, kwa sababu hamkumlinda bwana wenu, mpakwa mafuta wa Bwana. Tazameni hapo mlipo. Uko wapi mkuki wa mfalme na gudulia la maji ambavyo vilikuwa karibu na kichwa chake?”
17 Cependant, Saül reconnut la voix de David, et il dit: Est-ce ta voix, mon fils David? Et David répondit: C'est ton serviteur, Seigneur roi.
Sauli akatambua sauti ya Daudi, na kusema, “Je, hiyo ni sauti yako, Daudi mwanangu?” Daudi akajibu, “Naam, hiyo ndiyo, bwana wangu mfalme.”
18 Puis, il ajouta: Pourquoi le maître poursuit-il ainsi son serviteur? En quoi ai-je péché? Quelle iniquité a-t-on trouvée en moi?
Pia akaongeza, “Kwa nini bwana wangu anamfuatia mtumishi wake? Nimefanya nini, nalo kosa langu ni lipi nililolifanya niwe na hatia?
19 Maintenant donc que le roi mon maître écoute la parole de son serviteur. Si c'est Dieu qui t'excite contre moi, que ton sacrifice soit d'agréable odeur. Mais si ce sont des fils des hommes, maudits soient-ils devant le Seigneur, parce qu'ils m'ont chassé, de peur que je ne m'affermisse en l'héritage du Seigneur; et ils m'ont dit: Va-t'en, et sers d'autres dieux.
Sasa mfalme bwana wangu na asikilize maneno ya mtumishi wake. Kama Bwana amekuchochea dhidi yangu, basi yeye na aipokee sadaka yangu. Lakini hata hivyo, kama ni wanadamu waliofanya hivyo, walaaniwe mbele za Bwana! Wao sasa wamenifukuza kutoka sehemu yangu katika urithi wa Bwana wangu wakisema, ‘Nenda ukatumikie miungu mingine.’
20 Que mon sang ne soit point répandu sur la terre à la face du Seigneur, parce que le roi d'Israël est venu chercher ma vie, comme l'oiseau de nuit, quand il chasse dans les montagnes.
Basi usiache damu yangu imwagike kwenye ardhi mbali na uso wa Bwana. Mfalme wa Israeli ametoka kutafuta kiroboto, kama vile mtu awindavyo kware katika milima.”
21 Et Saül dit: J'ai péché, reviens, mon fils David, je ne te ferai point de mal, en récompense de ce qu'à tes yeux ma vie est précieuse. J'ai agi aujourd'hui comme un insensé, et j'ai ignoré beaucoup de choses.
Ndipo Sauli akasema, “Nimetenda dhambi. Rudi, Daudi mwanangu. Kwa kuwa uliyahesabu maisha yangu kuwa ya thamani leo, sitajaribu kukudhuru tena. Hakika nimetenda kama mpumbavu na nimekosa sana.”
22 Et David reprit la parole; et il dit: Voilà la javeline du roi; que l'un des serviteurs approche, et qu'il la prenne.
Daudi akajibu, “Mkuki wa mfalme uko hapa. Mmoja wa vijana wako na avuke kuuchukua.
23 Et le Seigneur accordera à chacun, selon sa foi et son équité. Cette nuit, quand le Seigneur t'a livré à mes mains, je n'ai pas voulu porter la main sur l'oint du Seigneur;
Bwana humlipa kila mtu kwa ajili ya haki yake na uaminifu wake. Bwana alikutia katika mikono yangu leo, lakini sikuinua mkono wangu juu ya mpakwa mafuta wa Bwana.
24 Et de même que ta vie a été précieuse à mes yeux, ma vie sera précieuse devant le Seigneur, et il m'abritera et il me délivrera de toutes mes afflictions.
Kwa hakika kama vile maisha yako yalivyokuwa ya thamani kwangu leo, vivyo hivyo maisha yangu na yawe na thamani kwa Bwana na kuniokoa kutoka taabu zote.”
25 Et Saül dit à David: Béni sois-tu, mon fils, tu prospèreras, et tu seras très puissant. Alors, David s'en alla à sa demeure, et Saül retourna à la ville où il résidait.
Ndipo Sauli akamwambia Daudi, “Mwanangu Daudi na ubarikiwe; utafanya mambo makubwa na hakika utashinda.” Basi Daudi akaenda zake, naye Sauli akarudi nyumbani.

< 1 Samuel 26 >