< 1 Rois 19 >

1 Et Achab apprit à Jézabel sa femme tout ce qu'avait fait Elle, et comment il avait tué les prophètes par l'épée.
Ahabu akamwambia Yezebeli kila kitu Eliya alichokuwa amefanya na jinsi alivyowaua manabii wote kwa upanga.
2 Et Jézabel envoya chez Elie, et elle dit: Si tu es Elie, moi je suis Jézabel: que Dieu me punisse et me punisse encore, si demain, à pareille heure, je n'ai pas fait de ta vie ce que tu as fait de la vie de chacun d'eux.
Hivyo Yezebeli akamtuma mjumbe kwa Eliya, kusema, “Hao miungu initendee hivyo na kuzidi, kama kufikia kesho wakati kama huu sitaifanya roho yako kama mmojawapo wa hao manabii.”
3 Et Elie eut crainte; il se leva; il s'éloigna pour sauver sa vie, et se rendit à Bersabée en Juda, où il laissa son serviteur.
Eliya aliogopa, na akakimbia kuokoa maisha yake. Alipofika Beer-Sheba katika Yuda, akamwacha mtumishi wake huko,
4 Lui-même s'enfonça dans le désert à une journée de marche; il s'assit sous un genévrier, et il demanda la mort, disant: C'est assez, prenez maintenant mon âme, ô Seigneur, car je ne suis pas meilleur que mes pères.
lakini yeye mwenyewe akatembea mwendo wa kutwa nzima katika jangwa. Akafika kwenye mti wa mretemu, akakaa chini yake na kuomba ili afe. Akasema, “Yatosha sasa, Bwana, ondoa roho yangu, kwani mimi si bora kuliko baba zangu.”
5 Et il se coucha et il s'endormit sous le genévrier; or voilà qu'un ange le toucha, et lui dit: Lève-toi et mange.
Kisha akajinyoosha chini ya mti, akalala usingizi. Mara malaika akamgusa na akamwambia, “Inuka na ule.”
6 Il regarda, et il vit auprès de sa tête des gâteaux d'épeautre et une fiole d'eau; il se leva, il mangea, il but et il s'endormit.
Akatazama pande zote, napo hapo karibu na kichwa chake palikuwepo mkate uliookwa kwenye makaa ya moto na gudulia la maji. Akala na kunywa, kisha akajinyoosha tena.
7 L'ange du Seigneur revint une seconde fois, le toucha, et lui dit: Lève- toi et mange, car tu as à faire un long chemin.
Yule malaika wa Bwana akaja tena mara ya pili, akamgusa akamwambia, “Inuka na ule, kwa kuwa safari ni ndefu kwako.”
8 Et il se leva; il mangea et il but, et il partit fortifié par ces aliments, et il marcha quarante jours et quarante nuits jusqu'au mont Horeb.
Kwa hiyo akainuka, akala na kunywa. Akiwa ametiwa nguvu na kile chakula, akasafiri siku arobaini usiku na mchana mpaka akafika Horebu, mlima wa Mungu.
9 Là, il entra dans la caverne; il en fit sa demeure, et la parole du Seigneur vint à lui, disant: Que fais-tu là, Elie?
Huko akaingia katika pango, akalala humo usiku ule. Nalo neno la Bwana likamjia, kusema, “Unafanya nini hapa, Eliya?”
10 Le prophète répondit: J'ai eu le cœur rempli de zèle pour le Seigneur Tout-Puissant, parce que les fils d'Israël vous ont abandonné, qu'ils ont renversé vos autels, et tué par l'épée vos prophètes; seul j'ai survécu, et ils en veulent à ma vie.
Akajibu, “Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote. Waisraeli wamelikataa Agano lako, wamevunja madhabahu zako na kuwaua manabii wako kwa upanga. Ni mimi, mimi peke yangu, niliyebaki, nao sasa wananitafuta ili waniangamize.”
11 Or, la voix reprit: Tu partiras demain; mais tiens-toi devant le Seigneur sur la montagne, regarde: le Seigneur va passer. Aussitôt, voilà qu'un vent violent passa, déchirant la montagne, brisant les rochers, et le Seigneur n'était pas dans le vent; après le vent, il y eut un tremblement de terre, et le Seigneur n'était pas dans le tremblement de terre;
Bwana akasema, “Toka nje ukasimame juu ya mlima mbele za Bwana, kwa kuwa Bwana yu karibu kupita hapo.” Kisha upepo mwingi na wenye nguvu ukapasua milima ile na kuvunjavunja miamba mbele za Bwana, lakini Bwana hakuwamo katika ule upepo. Baada ya upepo palikuwa na tetemeko la nchi, lakini Bwana hakuwamo kwenye lile tetemeko.
12 Après le tremblement de terre, vint une flamme, et le Seigneur n'était pas dans la flamme; après la flamme, vint le murmure d'un souffle léger.
Baada ya tetemeko la nchi ukaja moto, lakini Bwana hakuwamo katika ule moto. Baada ya moto ikaja sauti ya utulivu ya kunongʼona.
13 Quand Elie entendit ce souffle, il se voila le visage de son manteau de peau de brebis; puis, il sortit et il se tint à l'entrée de la caverne; alors, une voix s'approcha de lui, disant: Que fais-tu là, Elie?
Eliya alipoisikia, akafunika uso kwa vazi lake, akatoka na kusimama kwenye mdomo wa pango. Kisha ile sauti ikamwambia, “Eliya, unafanya nini hapa?”
14 Et le prophète répondit: J'ai eu le cœur plein de zèle pour le Seigneur Tout-Puissant, parce que les fils d'Israël ont abandonné votre alliance, renversé vos autels, et tué par l'épée vos prophètes; seul j'ai survécu, et ils en veulent à ma vie.
Akajibu, “Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote. Waisraeli wamelikataa Agano lako, wamevunja madhabahu zako na kuwaua manabii wako kwa upanga. Ni mimi, mimi peke yangu, niliyebaki, nao sasa wananitafuta ili waniangamize.”
15 Et le Seigneur lui dit: Pars, remets-toi en marche, prends le chemin du désert de Damas, tu iras, et tu sacreras Azaël pour être roi de Syrie.
Bwana akamwambia, “Rudi kwa njia uliyoijia, uende kwenye Jangwa la Dameski. Wakati utakapofika huko, mtie Hazaeli mafuta awe mfalme wa Aramu
16 Et tu sacreras Jéhu, fils de Namsi, pour être roi d'Israël; et tu sacreras Elisée, fils de Saphat, pour être prophète après toi.
Pia mtie mafuta Yehu mwana wa Nimshi awe mfalme wa Israeli, na umtie Elisha mwana wa Shafati kutoka Abel-Mehola mafuta awe nabii badala yako.
17 Celui qu'épargnera l'épée d'Azaël, Jéhu le mettra à mort; celui qu'épargnera l'épée de Jéhu, Elisée le mettra à mort.
Yehu atamuua yeyote atakayeutoroka upanga wa Hazaeli, naye Elisha atamuua yeyote atakayeutoroka upanga wa Yehu.
18 Et je me réserve, en Israël, sept mille hommes, les seuls qui n'aient point fléchi le genou devant Baal, les seuls dont la bouche ne l'ait point adoré.
Hata sasa nimeweka akiba watu elfu saba katika Israeli, wote ambao hawajampigia Baali magoti, na wote ambao midomo yao haijambusu.”
19 Et Elie partit de ce lieu, et il trouva Elisée, fils de Saphat; celui-ci labourait avec des bœufs; il avait devant lui douze attelages, et seul il les conduisait. Le prophète alla droit à Elisée, et jeta sur lui son manteau de peau de brebis.
Hivyo Eliya akaondoka kutoka huko na kumkuta Elisha mwana wa Shafati. Alikuwa akilima kwa jozi kumi na mbili za maksai, na yeye mwenyewe aliongoza ile jozi ya kumi na mbili. Eliya akapita karibu naye, akamrushia vazi lake.
20 Et Elisée abandonna ses bœufs; il suivit à grands pas Elie, et il lui dit: Je vais embrasser mon père; puis, je t'accompagnerai. Elie reprit: Reviens, car j'ai travaillé pour toi.
Kisha Elisha akawaacha maksai wake, akamkimbilia Eliya, akamwambia, “Niruhusu nikawabusu baba yangu na mama yangu, halafu nitafuatana nawe.” Eliya akajibu, “Rudi zako, kwani nimekutendea nini?”
21 Et il s'éloigna d'Elie, il prit ses couples de bœufs, il les sacrifia, il les fit cuire avec l'attirail des attelages, il les donna au peuple, et il mangea; enfin il rejoignit Elie et il le servit.
Basi Elisha akamwacha Eliya, naye akarudi. Akachukua ile jozi yake ya maksai na kuwachinja. Akaipika ile nyama kwa kutumia miti ya nira kama kuni na kuwapa watu, nao wakala. Kisha akaondoka, akamfuata Eliya, akamtumikia.

< 1 Rois 19 >