< 1 Rois 17 >

1 Or, Elie le prophète thesbite, de Thesba en Galaad, dit à Achab: Vive le Seigneur, Dieu des armées, Dieu d'Israël, devant qui je suis, il n'y aura en ces années ni rosée ni pluie, sinon à ma voix.
Basi Eliya, Mtishbi kutoka Tishbi katika Gileadi, akamwambia Ahabu, “Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninamtumikia, hapatakuwa na umande wala mvua katika miaka hii, isipokuwa kwa neno langu.”
2 Et la parole du Seigneur vint à Élie, disant:
Kisha neno la Bwana likamjia Eliya, kusema,
3 Va-t'en d'ici du côté de l'orient, et cache-toi dans le torrent de Chorrath, en face du Jourdain.
“Ondoka hapa, elekea upande wa mashariki ukajifiche katika Kijito cha Kerithi, mashariki mwa Yordani.
4 Tu boiras de l'eau du torrent, et j'ordonnerai aux corbeaux de te nourrir en ce lieu.
Utakunywa maji kutoka kile kijito, nami nimeagiza kunguru wakulishe huko.”
5 Et Elie fit selon la parole du Seigneur; il s'établit dans le torrent de Chorrath, en face du Jourdain.
Hivyo akafanya kile alichoambiwa na Bwana. Akaenda katika Kijito cha Kerithi, mashariki ya Yordani na akakaa huko.
6 Et les corbeaux lui apportèrent des pains à l'aurore, et des chairs le soir; et il but de l'eau du torrent.
Kunguru wakamletea mkate na nyama asubuhi na mkate na nyama jioni, naye akanywa maji kutoka kile kijito.
7 Quelque temps après le torrent se tarit, car il n'y eut point de pluie sur la terre.
Baada ya muda, kile kijito kikakauka kwa sababu mvua haikuwa imenyesha katika nchi.
8 Et la parole du Seigneur vint à Elie, disant:
Kisha neno la Bwana likamjia, kusema,
9 Lève-toi et va-t'en à Sarepta chez les Sidoniens; là, j'ai prescrit à une femme veuve de te nourrir.
“Ondoka, uende Sarepta ya Sidoni na ukae huko. Nimemwagiza mjane katika sehemu ile akupatie chakula.”
10 Et il se leva, et il partit pour Sarepta; arrivé devant les portes de la ville, il y vit une femme veuve qui ramassait du bois. Et Elie cria après elle, et il lui dit: Prends un peu d'eau dans une cruche, et je boirai.
Hivyo akaenda Sarepta. Alipofika kwenye lango la mji, mjane alikuwa huko akiokota kuni. Akamwita na kumwambia, “Naomba uniletee maji kidogo kwenye gudulia ili niweze kunywa.”
11 Elle en alla prendre; puis, le prophète cria après elle, et il lui dit: Apporte-moi un morceau du pain que tu as en ta maison.
Alipokuwa anakwenda kumletea, akamwita akasema, “Tafadhali niletee pia kipande cha mkate.”
12 Mais la femme répondit: Vive le Seigneur ton Dieu! je n'ai pas un seul pain cuit, je n'ai qu'un peu de farine dans la maie et quelques gouttes d'huile dans la fiole; je vais ramasser deux petits morceaux de bois; puis, je rentrerai, et je pétrirai pour moi et mes enfants; nous mangerons, et après nous mourrons.
Akamjibu, “Hakika kama Bwana Mungu wako aishivyo, sina mkate wowote, isipokuwa konzi ya unga kwenye gudulia na mafuta kidogo kwenye chupa. Ninakusanya kuni chache nipeleke nyumbani na nikapike chakula kwa ajili yangu na mwanangu, ili kwamba tule, kiishe, tukafe.”
13 Elie répliqua: Rassure-toi; rentre et fais ce que tu viens de dire; fais de plus pour moi un petit pain; tu me l'apporteras d'abord, tu en feras ensuite pour toi et pour tes enfants.
Eliya akamwambia, “Usiogope. Nenda nyumbani ukafanye kama ulivyosema. Lakini kwanza unitengenezee mimi mkate mdogo kutoka vile ulivyo navyo kisha uniletee na ndipo utayarishe chochote kwa ajili yako na mwanao.
14 Car voici ce que dit le Seigneur: La maie ne manquera plus de farine, et l'huile ne baissera plus dans la fiole, jusqu'au jour où le Seigneur donnera de la pluie à la terre.
Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Lile gudulia la unga halitakwisha wala ile chupa ya mafuta haitakauka hadi siku ile Bwana atakapoleta mvua juu ya nchi.’”
15 Et la femme s'en alla; elle pétrit, elle mangea; et le prophète et ses enfants mangèrent.
Akaondoka na kufanya kama Eliya alivyomwambia. Kwa hiyo kukawa na chakula kila siku kwa ajili ya Eliya, yule mwanamke na jamaa yake.
16 Et la maie ne manqua plus de farine, et l'huile ne baissa pas dans la fiole, selon la parole que le Seigneur avait dite par la voix d'Elie.
Kwa kuwa lile gudulia la unga halikwisha na ile chupa ya mafuta haikukauka, sawasawa na lile neno la Bwana alilosema Eliya.
17 Après cela, le fils de la femme maîtresse de la maison tomba malade, et sa maladie fut très violente; enfin le souffle de la vie se retira de lui.
Baada ya muda, mwana wa yule mwanamke mwenye nyumba akaugua. Hali yake ikaendelea kuwa mbaya sana, na hatimaye akaacha kupumua.
18 Et la femme dit à Elie: Qu'y a-t-il entre moi et toi, homme de Dieu? Es-tu venu chez moi pour rappeler le souvenir de mes péchés, et pour faire mourir mon fils?
Akamwambia Eliya, “Una nini dhidi yangu, ewe mtu wa Mungu? Umekuja ili kukumbushia dhambi yangu na kusababisha kifo cha mwanangu?”
19 Et le prophète répondit à la femme: Donne-moi ton fils. Et il le prit de son sein; et il le porta dans la chambre où il demeurait, et il l'étendit sur sa couche.
Eliya akamjibu, “Nipe mwanao.” Eliya akampokea kutoka kifuani mwake, akambeba mpaka chumba cha juu alipokuwa anaishi, akamlaza kitandani mwake.
20 Là, il cria et il dit: Malheur à moi, Seigneur! je vous prends à témoin en faveur de cette veuve chez qui j'habite; vous l'avez affligée en faisant mourir son fils.
Kisha akamlilia Bwana, akasema “Ee Bwana Mungu wangu, je, pia umeleta msiba juu ya mjane huyu ninayeishi pamoja naye, kwa kusababisha mwanawe kufa?”
21 Ensuite, il souffla trois fois sur l'enfant, il invoqua le Seigneur, et il dit: Seigneur mon Dieu, que l'âme de cet enfant revienne en lui.
Kisha akajinyoosha juu ya kijana mara tatu na kumlilia Bwana, akisema, “Ee Bwana Mungu wangu, nakuomba roho ya huyu kijana imrudie!”
22 Et il en fut ainsi. L'enfant jeta un grand cri;
Bwana akasikia kilio cha Eliya, na roho ya kijana ikamrudia, naye akafufuka.
23 Et Elie descendit de sa chambre dans la maison, et il le rendit à sa mère; et il lui dit: Regarde, ton enfant est en vie.
Eliya akamtwaa kijana na kumbeba kutoka chumbani mwake akamshusha kumpeleka kwenye nyumba. Akampa mama yake na kusema, “Tazama, mwanao yu hai!”
24 Et la femme dit à Elie: Je reconnais que tu es un homme de Dieu; la parole de Dieu dans ta bouche est véritable.
Ndipo yule mwanamke akamwambia Eliya, “Sasa ninajua kwamba wewe ni mtu wa Mungu, na kwamba neno la Bwana kutoka kinywani mwako ni kweli.”

< 1 Rois 17 >