< Zacharie 10 >

1 Demandez de la pluie à l’Eternel dans la saison des dernières pluies: c’est l’Eternel qui produit les éclairs. Il vous donnera des ondées abondantes, à chacun l’herbe des champs.
Mwombeni Bwana mvua wakati wa vuli; ndiye Bwana atengenezaye mawingu ya tufani. Huwapa watu manyunyu ya mvua, pia mimea ya shambani kwa ajili ya kila mtu.
2 C’Est que les Terafim débitent de vains discours, les augures des visions mensongères, les songes disent des faussetés, apportent des consolations illusoires; c’est pourquoi ils vaguent comme des brebis, ils sont dans la misère, faute de pasteurs.
Sanamu huzungumza udanganyifu, waaguzi huona maono ya uongo; husimulia ndoto ambazo si za kweli, wanatoa faraja batili. Kwa hiyo watu wanatangatanga kama kondoo walioonewa kwa kukosa mchungaji.
3 Contre les pasteurs ma colère s’est allumée, je sévirai contre les boucs conducteurs du troupeau, car l’Eternel-Cebaot a passé en revue son troupeau, la maison de Juda, et la considère comme son coursier d’honneur dans la bataille.
“Hasira yangu inawaka dhidi ya wachungaji, nami nitawaadhibu viongozi; kwa kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote atalichunga kundi lake, nyumba ya Yuda, naye atawafanya kuwa kama farasi mwenye kiburi akiwa vitani.
4 C’Est de là que provient la pierre d’angle, de là la cheville ouvrière, de là l’arc de combat; de là sortent les vainqueurs tous ensemble.
Kutoka Yuda litatokea Jiwe la pembeni, kutoka kwake vitatoka vigingi vya hema, kutoka kwake utatoka upinde wa vita, kutoka kwake atatoka kila mtawala.
5 Ils seront comme des héros piétinant, dans la mêlée, la boue des chemins; ils soutiendront la lutte, car l’Eternel est avec eux: ceux qui montent des chevaux seront couverts de confusion.
Kwa pamoja watakuwa kama mashujaa wanaokanyaga barabara za matope wakati wa vita. Kwa sababu Bwana yu pamoja nao, watapigana na kuwashinda wapanda farasi.
6 Je donnerai la victoire à la maison de Juda, je prêterai main-forte à la maison de Joseph; je les rétablirai après les avoir pris en pitié: ils seront comme si jamais je ne les avais délaissés, car je suis l’Eternel, leur Dieu, et je les exaucerai.
“Nitaiimarisha nyumba ya Yuda na kuiokoa nyumba ya Yosefu. Nitawarejesha kwa sababu nina huruma juu yao. Watakuwa kama watu ambao sijawahi kuwakataa kwa sababu mimi ndimi Bwana Mungu wao, nami nitawajibu.
7 Ephraïm sera tel qu’un vaillant guerrier, son cœur sera joyeux comme sous l’action du vin. Ses fils le verront et se réjouiront, leur cœur exultera en l’Eternel.
Waefraimu watakuwa kama mashujaa, mioyo yao itafurahi kana kwamba ni kwa divai. Watoto wao wataona na kufurahi, mioyo yao itashangilia katika Bwana.
8 Je leur ferai entendre le signal et les rassemblerai, parce que je les aurai rachetés. Ils seront nombreux comme jadis ils furent nombreux.
Nitawaashiria na kuwakusanya ndani. Hakika nitawakomboa, nao watakuwa wengi kama walivyokuwa mwanzoni.
9 Quand je les aurai semés parmi les nations, dans les pays lointains, ils se souviendront de moi; ils y vivront avec leurs enfants, puis ils reviendront.
Ijapokuwa niliwatawanya miongoni mwa mataifa, hata hivyo wakiwa katika nchi za mbali watanikumbuka mimi. Wao na watoto wao watanusurika katika hatari nao watarudi.
10 Je les ramènerai du pays d’Egypte, je les rassemblerai du pays d’Achour; je les ferai rentrer au pays de Galaad et au Liban, et ils s’y trouveront à l’étroit.
Nitawarudisha kutoka Misri na kuwakusanya toka Ashuru. Nitawaleta katika nchi ya Gileadi na Lebanoni, na hapo hapatakuwa na nafasi ya kuwatosha.
11 Alors la détresse franchira la mer et frappera les flots au sein de l’Océan, toutes les sources profondes du Nil tariront. Ainsi sera abaissé l’orgueil d’Achour, et le sceptre disparaîtra de l’Egypte.
Watapita katika bahari ya mateso; bahari iliyochafuka itatulizwa na vilindi vyote vya Mto Naili vitakauka. Kiburi cha Ashuru kitashushwa, nayo fimbo ya utawala ya Misri itatoweka.
12 Quant à eux je les rendrai puissants par l’Eternel, et ils marcheront fièrement en son nom, dit l’Eternel.
Nitawaimarisha katika Bwana, na katika jina lake watatembea,” asema Bwana.

< Zacharie 10 >