< Job 9 >

1 Job reprit la parole et dit:
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 Oui, je sais qu’il en est ainsi: comment l’homme aurait-il gain de cause avec Dieu?
“kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
3 Si nous désirions discuter avec lui, pas une fois sur mille il ne daignerait nous répondre.
Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
4 Eminemment sage, triomphant de force, qui jamais lui tint tête et s’en trouva bien?
Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
5 Il déplace les montagnes à l’improviste et les bouleverse dans sa colère.
ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
6 Il fait trembler la terre sur ses bases et ébranle les colonnes qui la supportent.
ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
7 II donne un ordre au soleil, et le soleil ne paraît point; il met un sceau sur les étoiles.
Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
8 A lui seul, il déploie les cieux; il chemine sur la crête des vagues.
ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
9 Ila fait la Grande Ourse, l’Orion, les Pléiades et les demeures sidérales du Midi.
ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
10 Il accomplit des merveilles sans fin, des prodiges qui ne se peuvent compter.
Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
11 Ah! S’Il passait auprès de moi, je ne le verrais point; s’il se glissait sous mes yeux, je ne le remarquerais pas.
Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
12 Quand il empoigne quelqu’un, qui lui fera lâcher prise? Qui lui dira: "Que fais-tu?"
Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
13 Dieu ne refoule pas sa colère; sous ses coups plient les satellites de l’orgueil.
Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
14 Et moi j’oserais lui répliquer, je ferais assaut de paroles avec lui,
Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
15 moi, qui tout innocent que je fusse, ne trouverais rien à lui répondre, et demanderais simplement grâce à mon juge!
Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
16 Dût-il même se rendre à mon appel, je ne croirais pas qu’il écoute ma voix;
Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
17 car il m’accable sous un vent de tempête et multiplie gratuitement mes blessures.
kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
18 Il ne me permet pas de reprendre haleine, tant il m’abreuve d’amertumes.
Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
19 S’Agit-il de faire preuve de force, il est là! S’Agit-il de jugement, il dira: "Qui pourrait m’assigner?"
Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
20 Fussé-je innocent, ma bouche me déclarerait coupable! Fussé-je sans reproche, elle me convaincrait de perversité!
Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
21 Oui, je suis sans reproche! Je ne me soucie pas de la vie, je suis las de l’existence.
Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
22 Tout revient au même: aussi dis-je que juste et méchant, il les fait également périr.
Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
23 Si un cataclysme entraîne des morts soudaines, il se rit de l’épreuve des innocents.
Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
24 Par lui, la terre a été livrée aux impies: il voile les yeux de ceux qui y rendent la justice. Si ce n’est lui, qui serait-ce?
Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
25 Mes jours sont plus rapides qu’un courrier; ils s’enfuient sans avoir vu le bonheur.
Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
26 Ils passent comme des barques de jonc, comme l’aigle qui se précipite sur la proie.
Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
27 Quand je dis: "Je veux oublier ma souffrance, laisser là ma mine attristée et reprendre mes esprits",
Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
28 je suis envahi par la crainte de mes tourments, sachant bien que tu ne m’absoudras pas.
Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
29 Je serai déclaré coupable: pourquoi donc prendre une peine inutile?
Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
30 Dussé-je me laver dans de la neige fondue et purifier mes mains avec de la potasse,
Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
31 aussitôt tu me plongerais dans une fosse fangeuse, et mes vêtements mêmes auraient horreur de moi.
Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
32 Car il n’est pas un homme comme moi pour que je lui réponde et que nous paraissions ensemble en justice.
Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
33 Il n’existe pas d’arbitre entre nous, qui puisse poser sa main sur tous deux.
Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
34 Qu’il écarte de moi sa verge, et que ses terreurs cessent de peser sur moi.
Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
35 Alors je parlerai sans le redouter, car je n’en suis pas là dans le secret de ma conscience.
Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.

< Job 9 >