< Jérémie 42 >

1 Tous les chefs de troupes, ainsi que Johanan, fils de Karèah, et Yaazania, fils de Hochaïa, et tout le peuple, grands et petits, s’avancèrent,
Ndipo maafisa wote wa jeshi, pamoja na Yohanani mwana wa Karea, na Yezania mwana wa Hoshaya, na watu wote kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana wakamjia
2 et dirent au prophète Jérémie: "Agrée, de grâce, notre supplication et implore l’Eternel, ton Dieu, pour nous, pour cette poignée des nôtres qui existent encore; car de nombreux que nous étions, nous sommes réduits à peu de chose, comme tes yeux s’en rendent compte en nous voyant.
Yeremia nabii na kumwambia, “Tafadhali sikia maombi yetu na umwombe Bwana Mungu wako kwa ajili ya watu hawa wote waliosalia. Kwa kuwa kama unavyoona sasa, ingawa wakati fulani tulikuwa wengi, sasa tumesalia wachache tu.
3 Que l’Eternel, ton Dieu, nous indique le chemin que nous avons à suivre et la conduite que nous devons tenir!"
Omba ili Bwana Mungu wako atuambie twende wapi na tufanye nini.”
4 Le prophète Jérémie leur répondit: "Je vous entends; je vais implorer l’Eternel, votre Dieu, suivant votre demande, et toutes les réponses que l’Eternel m’adressera pour vous, je vous les communiquerai, sans rien vous cacher."
Nabii Yeremia akajibu, “Nimewasikia. Kwa hakika nitamwomba Bwana Mungu wenu kama mlivyoomba. Nitawaambia kila kitu asemacho Bwana, wala sitawaficha chochote.”
5 Et eux de répliquer à Jérémie: "Que l’Eternel se lève contre nous en témoin sincère et véridique, si nous manquons d’agir en tout conformément à ce que l’Eternel, ton Dieu, te donnera mission de nous dire!
Kisha wakamwambia Yeremia, “Bwana na awe shahidi wa kweli na mwaminifu kati yetu kama hatutafanya sawasawa na kila kitu Bwana Mungu wako atakachokutuma utuambie.
6 Que! a chose nous plaise ou nous déplaise, nous obéirons à la voix de l’Eternel, notre Dieu, auprès de qui nous te déléguons, avec la certitude d’être heureux par notre docilité aux ordres de l’Eternel, notre Dieu."
Likiwa jema au likiwa baya, tutamtii Bwana Mungu wetu, ambaye tunakutuma kwake, ili mambo yote yawe mema kwetu, kwa maana tutamtii Bwana Mungu wetu.”
7 Au bout de dix jours, la parole de l’Eternel fut adressée à Jérémie.
Baada ya siku kumi, neno la Bwana likamjia Yeremia.
8 Aussitôt il manda Johanan, fils de Karèah, et tous les chefs de troupes, ses compagnons, ainsi que le peuple tout entier, grands et petits,
Kwa hiyo akawaita pamoja Yohanani mwana wa Karea, na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye na watu wote kuanzia mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana.
9 et leur dit: "Voici ce qu’a déclaré l’Eternel, Dieu d’Israël, auprès de qui vous m’avez délégué pour lui exposer vos sollicitations.
Akawaambia, “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye mlinituma kuwasilisha maombi yenu:
10 Si vous continuez à demeurer dans ce pays, je vous y édifierai et ne vous détruirai pas, je vous y implanterai et ne vous en déracinerai plus; car j’ai regret au mal que je vous ai fait.
‘Kama mkikaa katika nchi hii, nitawajenga wala sitawabomoa, nitawapanda wala sitawangʼoa, kwani ninahuzunishwa na maafa niliyowapiga nayo.
11 Ne redoutez pas le roi de Babylone, devant qui vous tremblez; non, ne le redoutez pas, dit l’Eternel, car je serai avec vous pour vous secourir et vous sauver de ses mains.
Msimwogope mfalme wa Babeli, ambaye sasa mnamwogopa. Msimwogope, asema Bwana, kwa kuwa niko pamoja nanyi, nami nitawaokoa na kuwaponya kutoka mikononi mwake.
12 J’Attirerai sur vous sa compassion, il aura pitié de vous, et il vous rétablira sur votre territoire.
Nitawaonea huruma ili naye awe na huruma nanyi na kuwarudisha katika nchi yenu.’
13 Mais si vous dites: "Nous ne voulons pas rester dans ce pays-ci," en refusant d’écouter la voix de l’Eternel, votre Dieu,
“Hata hivyo, kama mkisema, ‘Hatutakaa katika nchi hii,’ hivyo mkaacha kumtii Bwana Mungu wenu,
14 si vous dites: "Non pas! mais nous allons nous rendre en Egypte, où nous ne verrons plus de combats ni n’entendrons plus le son de la trompette ni ne souffrirons du manque de pain, et là nous nous établirons."
nanyi kama mkisema, ‘Hapana, tutakwenda kuishi Misri, mahali ambapo hatutaona vita au kusikia sauti ya tarumbeta au kuwa na njaa ya chakula,’
15 Eh bien donc! Ecoutez la parole de l’Eternel, ô survivants de Juda! Ainsi parle l’Eternel-Cebaot, Dieu d’Israël: Si réellement vous vous obstinez à vous rendre en Egypte, si vous y entrez pour y séjourner,
basi sikieni neno la Bwana, enyi mabaki ya Yuda. Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Ikiwa mmekusudia kwenda Misri na kufanya makazi huko,
16 il arrivera que le glaive dont vous avez peur vous y atteindra, dans ce pays d’Egypte, et la famine, objet de vos inquiétudes, elle s’attachera à vous dans cette Egypte, et vous y périrez.
basi ule upanga mnaouogopa utawapata huko, na njaa mnayoihofia itawafuata huko Misri, nanyi mtafia huko.
17 Et tous les hommes qui se seront obstinés à pénétrer en Egypte pour y séjourner, ils deviendront la proie de l’épée, de la famine et de la peste, de sorte que personne parmi eux n’échappera et ne se soustraira au malheur que je ferai fondre sur eux.
Naam, wote waliokusudia kwenda kuishi Misri watakufa kwa upanga, njaa na tauni; hakuna hata mmoja wao atakayenusurika au kuokoka maafa nitakayoyaleta juu yao.’
18 Car ainsi parle l’Eternel-Cebaot, Dieu d’Israël: De même que ma colère et mon indignation se sont déversées sur les habitants de Jérusalem, de même mon courroux se déversera sur vous quand vous pénétrerez en Egypte. Vous deviendrez un objet d’imprécation, de stupeur, de malédiction et d’opprobre, et ne reverrez plus ce lieu-ci.
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Kama vile hasira yangu na ghadhabu yangu ilivyomwagwa juu ya wale walioishi Yerusalemu, ndivyo ghadhabu yangu itakavyomwagwa juu yenu mtakapokwenda Misri. Mtakuwa kitu cha kulaania na cha kutisha, cha kulaumia na cha kushutumia, nanyi kamwe hamtaona mahali hapa tena.’
19 L’Eternel vous le dit, ô survivants de Juda: N’Allez pas en Egypte. Sachez bien que je vous avertis solennellement en ce jour.
“Enyi mabaki ya Yuda, Bwana amewaambia, ‘Msiende Misri.’ Hakikisheni jambo hili: Ninawaonya leo
20 Car vous vous êtes menti à vous-mêmes, lorsque vous m’avez délégué auprès de l’Eternel, votre Dieu, en disant: "Implore en notre faveur l’Eternel, notre Dieu, et tout ce que l’Eternel, notre Dieu, dira, rapporte-le nous fidèlement et nous agirons en conséquence."
kwamba mmefanya kosa kubwa mioyoni mwenu mliponituma kwa Bwana Mungu wenu na kusema, ‘Mwombe Bwana Mungu wetu kwa ajili yetu, nawe utuambie kila kitu atakachosema, nasi tutafanya.’
21 Je vous ai tout rapporté en ce jour, mais vous n’écoutez pas la voix de l’Eternel, votre Dieu, et cela relativement à tout ce qu’il m’a donné mission de vous dire.
Nimewaambieni leo, lakini bado ninyi hamtaki kumtii Bwana Mungu wenu katika yote aliyonituma niwaambie.
22 Or donc, sachez-le bien, c’est par le glaive, par la famine et par la peste que vous périrez dans le pays où il vous plaît de vous rendre, pour y séjourner."
Basi sasa, hakikisheni jambo hili: Mtakufa kwa upanga, njaa na tauni mahali ambapo mnataka kwenda kuishi.”

< Jérémie 42 >