< Ézéchiel 26 >

1 II arriva dans la onzième année, le premier du mois, que la parole de l’Eternel me fut adressée en ces termes:
Mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
2 "Fils de l’homme, parce que Tyr s’est écriée au sujet de Jérusalem: Ah! Elle est brisée, celle qui était la porte des nations! Mon tour est venu: je vais être comblée, puisqu’elle est ruinée,
“Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema kuhusu Yerusalemu, ‘Aha! Lango la kwenda kwa mataifa limevunjika, nayo milango yake iko wazi mbele yangu, sasa kwa kuwa amekuwa magofu nitastawi.’
3 c’est pourquoi, ainsi parle le Seigneur Dieu: Voici que je m’en prends à toi, Tyr; je soulèverai contre toi des nations nombreuses comme la mer soulève ses vagues.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na wewe, ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi dhidi yako, kama bahari inayovurumisha mawimbi yake.
4 Elles détruiront les remparts de Tyr et démoliront ses tours; je la dénuderai de sa poussière et je ferai d’elle une roche aride.
Watavunja kuta za Tiro na kuibomoa minara yake, nitakwangua udongo wake na kuufanya mwamba mtupu.
5 Elle deviendra un étendoir à filets au milieu de la mer, car c’est moi qui parle, dit le Seigneur Dieu, et elle sera une proie pour les nations.
Itakuwa huko katikati ya bahari patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki, kwa maana nimenena, asema Bwana Mwenyezi. Atakuwa nyara kwa mataifa,
6 Et ses filles qui sont dans la campagne seront massacrées par le glaive; ainsi ils sauront que je suis l’Eternel.
nayo makao yake huko bara yataangamizwa kwa upanga. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.
7 Oui, ainsi parle le Seigneur Dieu, je vais, du Nord, amener contre Tyr Nabuchodonosor, roi de Babylone, le roi des rois, avec des chevaux, des chars, des cavaliers, une grande multitude et un peuple nombreux.
“Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kutoka kaskazini nitamleta dhidi ya Tiro Mfalme Nebukadneza wa Babeli, mfalme wa wafalme, akiwa na farasi na magari ya vita, wapanda farasi na jeshi kubwa.
8 Tes filles qui sont dans la campagne, il les fera périr par l’épée, et contre toi il élèvera des retranchements, jettera des redoutes et dressera des boucliers.
Atayaharibu makao yako huko bara kwa upanga, ataweka jeshi kukuzingira, atakuzingira mpaka kwenye kuta za ngome zako na kuinua ngao zake dhidi yako.
9 Les coups de son bélier, il les assénera sur tes remparts, et tes tours, il les brisera par ses armes.
Ataelekeza mapigo ya vyombo vyake vya kubomolea dhidi ya kuta zako na kubomoa minara yako kwa silaha zake.
10 Grâce à la multitude de ses chevaux, il te couvrira de leur poussière; du bruit des cavaliers, des roues et des chars tes murailles trembleront, quand il entrera par tes portes comme on entre dans une ville éventrée.
Farasi zake zitakuwa nyingi sana kiasi kwamba utafunikwa na mavumbi watakayotimua. Kuta zako zitatikisika kwa mshindo wa farasi wa vita, magari makubwa na magari ya vita wakati aingiapo malango yako kama watu waingiao mji ambao kuta zake zimebomolewa kote.
11 Sous les sabots de ses chevaux il foulera toutes tes rues, ta population, il la tuera par l’épée, et les monuments de ta puissance tomberont à terre.
“Kwato za farasi zake zitakanyaga barabara zako zote, atawaua watu wako kwa upanga na nguzo zako zilizo imara zitaanguka chini.
12 Ils pilleront tes richesses, feront main basse sur tes marchandises; ils démoliront tes murailles et abattront tes maisons de plaisance; tes pierres, tes bois et ta poussière, ils les jetteront dans l’eau.
Watateka utajiri wako na kuchukua nyara bidhaa zako, watazivunja kuta zako na kuzibomoa nyumba zako nzuri, watatupa baharini mawe yako, mbao zako na kifusi chako.
13 Je mettrai fin à la rumeur de tes chants, et le son de tes harpes ne se fera plus entendre.
Nitakomesha kelele za nyimbo zako, na uimbaji wako wa kinubi kamwe hautasikika tena.
14 Je ferai de toi une roche aride, tu deviendras un étendoir à filets. Tu ne seras plus rebâtie, car c’est moi, l’Eternel, qui parle, dit le Seigneur Dieu."
Nitakufanya mwamba mtupu, nawe utakuwa mahali pa kutandazia nyavu za kuvulia samaki. Kamwe hutajengwa tena, kwa maana Mimi Bwana nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
15 Ainsi parle le Seigneur Dieu à Tyr: "Certes, au bruit de ta chute, aux gémissements des mourants, quand s’accomplira la tuerie au milieu de toi, les îles trembleront.
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa Tiro: ‘Je, nchi za pwani hazitatetemeka kwa kishindo cha anguko lako, wakati majeruhi wanapolia kwa maumivu makali na wakati mauaji yanaendelea ndani yako?
16 Ils descendront de leurs trônes, tous les princes de la mer, ils ôteront leurs manteaux et dépouilleront leurs vêtements brodés; ils se vêtiront d’épouvante, s’asseoiront à terre, frissonneront à tout instant et seront atterrés à cause de toi.
Ndipo wakuu wote wa mataifa ya pwani watashuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuweka kando majoho yao na kuvua nguo zao zilizotariziwa. Wakiwa wamevikwa hofu kuu, wataketi chini ardhini, wakiwa wanatetemeka kila dakika na wakikustajabia.
17 Ils entonneront sur toi une complainte et te diront: "Comme tu as péri, toi si populeuse grâce aux mers, ville illustre, si puissante sur les flots, toi et tes habitants, qui inspiraient la terreur à tous les voisins!
Ndipo wao watakuombolezea na kukuambia: “‘Tazama jinsi ulivyoharibiwa, ee mji uliokuwa na sifa, wewe uliyekaliwa na mabaharia! Ulikuwa na nguvu kwenye bahari, wewe na watu wako; wote walioishi huko, uliwatia hofu kuu.
18 Maintenant les côtes tremblent au jour de ta chute, et les îles qui sont dans la mer sont épouvantées de ta fin.
Sasa nchi za pwani zinatetemeka katika siku ya anguko lako; visiwa vilivyomo baharini vinaogopa kwa kuporomoka kwako.’
19 Car, ainsi parle le Seigneur Dieu, lorsque je ferai de toi une ville ruinée, pareille aux villes qui ne sont plus habitées, lorsque je soulèverai contre toi les ondes de l’abîme et que te couvriront les eaux profondes,
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitakapokufanya uwe mji wa ukiwa, kama miji isiyokaliwa tena na watu, nitakapoleta vilindi vya bahari juu yako na maji yake makuu yatakapokufunika,
20 alors je te précipiterai avec ceux qui sont descendus dans la fosse, auprès des gens des temps antiques, et je te confinerai dans les régions souterraines, dans les ruines éternelles, auprès de ceux qui sont descendus dans la fosse, afin que tu cesses d’être habitée, tandis que je répandrai de la beauté au pays des vivants.
ndipo nitakapokushusha chini pamoja na wale washukao shimoni, kwa watu wa kale, nami nitakufanya uishi katika pande za chini za nchi kama katika magofu ya kale, pamoja na wale washukao shimoni, nawe hutarudi au kurejea kwenye makao yako katika nchi ya walio hai.
21 Je te réduirai à néant et c’en sera fini de toi: l’on te cherchera et plus jamais l’on ne te trouvera", dit le Seigneur Dieu."
Nitakufikisha mwisho wa kutisha wala hutakuwepo tena. Watu watakutafuta, lakini kamwe hutaonekana tena, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ézéchiel 26 >