< Galates 3 >

1 Ô Galates insensés, qui vous a ensorcelés, vous devant les yeux de qui Jésus Christ a été dépeint, crucifié [au milieu de vous]?
Wagalatia wajinga, ni jicho gani ovu lililowaharibu? Je Yesu Kristo hakuoneshwa kama msulubiwa mbele ya macho yenu?
2 Je voudrais seulement apprendre ceci de vous: avez-vous reçu l’Esprit sur le principe des œuvres de loi, ou de l’ouïe de [la] foi?
Mimi nataka tu kufahamu hili kutoka kwenu. Je mlimpokea Roho kwa matendo ya sheria au kwa kuamini kile mlichosikia?
3 Êtes-vous si insensés? Ayant commencé par l’Esprit, achèveriez-vous maintenant par la chair?
Je, ninyi ni wajinga kiasi hiki? Je mlianza katika Roho ili mmalize katika mwili?
4 Avez-vous tant souffert en vain, si toutefois c’est en vain?
Je mliteseka kwa mambo mengi bure, kama kweli yalikuwa ya bure?
5 Celui donc qui vous fournit l’Esprit et qui opère des miracles au milieu de vous, [le fait-il] sur le principe des œuvres de loi, ou de l’ouïe de [la] foi?
Je yeye atoaye Roho kwenu na kutenda matendo ya nguvu kati yenu hufanya kwa matendo ya sheria au kwa kusikia pamoja na imani?
6 comme Abraham a cru Dieu, et cela lui fut compté à justice.
Abraham “Alimwamini Mungu akahesabiwa kuwa mwenye haki”.
7 Sachez donc que ceux qui sont sur le principe de [la] foi, ceux-là sont fils d’Abraham.
Kwa namna ile ile eleweni kwamba, wale ambao wanaamini ni watoto wa Abrahamu.
8 Or l’écriture, prévoyant que Dieu justifierait les nations sur le principe de [la] foi, a d’avance annoncé la bonne nouvelle à Abraham: « En toi toutes les nations seront bénies ».
Andiko lilitabiri kwamba Mungu angewahesabia haki watu wa mataifa kwa njia ya imani. Injili ilihubiriwa kwanza kwa Abrahamu: “katika wewe mataifa yote yatabarikiwa”.
9 De sorte que ceux qui sont sur le principe de [la] foi sont bénis avec le croyant Abraham.
Ili baadaye wale ambao wana imani wabarikiwe pamoja na Abrahamu, ambaye alikuwa na imani.
10 Car tous ceux qui sont sur le principe des œuvres de loi sont sous malédiction; car il est écrit: « Maudit est quiconque ne persévère pas dans toutes les choses qui sont écrites dans le livre de la loi pour les faire ».
Wale ambao wanategemea matendo ya sheria wako chini ya laana. Kwa kuwa imeandikwa, “Amelaaniwa kila mtu ambaye hashikamani na mambo yote yaliyoandikwa katika kitabu cha sheria, kuyatenda yote.”
11 Or que par [la] loi personne ne soit justifié devant Dieu, cela est évident, parce que: « Le juste vivra de foi ».
Sasa ni wazi kwamba Mungu hamhesabii haki hata mmoja kwa sheria, kwa kuwa “Mwenye haki ataishi kwa imani”.
12 Mais la loi n’est pas sur le principe de [la] foi, mais: « Celui qui aura fait ces choses vivra par elles ».
Sheria haitokani na imani, lakini badala yake “Ambaye hufanya mambo haya katika sheria, ataishi kwa sheria.”
13 Christ nous a rachetés de la malédiction de la loi, étant devenu malédiction pour nous (car il est écrit: « Maudit est quiconque est pendu au bois »),
Kristo alitukomboa sisi kutoka katika laana ya sheria wakati alipofanyika laana kwa ajili yetu. Kwa kuwa imeandikwa, “Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti.”
14 afin que la bénédiction d’Abraham parvienne aux nations dans le christ Jésus, afin que nous recevions par la foi l’Esprit promis.
Lengo lilikuwa kwamba, baraka ambazo zilikuwa kwa Ibrahimu zingekuja kwa watu wa mataifa katika Kristo Yesu, ili kwamba tuweze kupokea ahadi ya Roho kupitia imani.
15 Frères, je parle selon l’homme: personne n’annule une alliance qui est confirmée, même [celle] d’un homme, ni n’y ajoute.
Ndugu, ninazungumza kwa namna ya kibinadamu. Hata wakati ambapo agano la kibinadamu limekwisha kuwekwa imara, hakuna awezaye kupuuza au kuongezea.
16 Or c’est à Abraham que les promesses ont été faites, et à sa semence. Il ne dit pas: “et aux semences”, comme [parlant] de plusieurs; mais comme [parlant] d’un seul: – « et à ta semence », qui est Christ.
Sasa ahadi zilisemwa kwa Ibrahim na kwa kizazi chake. Haisemi, “kwa vizazi,” kumaanisha wengi, bali badala yake kwa mmoja pekee, “kwa kizazi chako,” ambaye ni Kristo.
17 Or je dis ceci: que la loi, qui est survenue 430 ans après, n’annule point une alliance antérieurement confirmée par Dieu, de manière à rendre la promesse sans effet.
Sasa nasema hivi, sheria ambayo ilikuja miaka 430 baadaye, haiondoi agano la nyuma lililowekwa na Mungu.
18 Car si l’héritage est sur le principe de loi, il n’est plus sur le principe de promesse; mais Dieu a fait le don à Abraham par promesse.
Kwa kuwa kama urithi ungelikuja kwa njia ya sheria, usingekuwa tena umekuja kwa njia ya ahadi. Lakini Mungu aliutoa bure kwa Ibrahimu kwa njia ya ahadi.
19 Pourquoi donc la loi? Elle a été ajoutée à cause des transgressions, jusqu’à ce que vienne la semence à laquelle la promesse est faite, ayant été ordonnée par des anges, par la main d’un médiateur.
Kwa nini sasa sheria ilitolewa? Iliongezwa kwa sababu ya makosa, mpaka mzao wa Ibrahimu aje kwa wale ambao kwao alikuwa ameahidiwa. Sheria iliwekwa katika shinikizo kupitia malaika kwa mkono wa mpatanishi.
20 Or un médiateur n’est pas [médiateur] d’un seul, mais Dieu est un seul.
Sasa mpatanishi humaanisha zaidi ya mtu mmoja, bali Mungu ni mmoja peke yake.
21 La loi est-elle donc contre les promesses de Dieu? Qu’ainsi n’advienne! Car s’il avait été donné une loi qui ait le pouvoir de faire vivre, la justice serait en réalité sur le principe de [la] loi.
Kwa hiyo je sheria iko kinyume na ahadi za Mungu? La hasha! Kwa kuwa kama sheria iliyokuwa imetolewa ilikuwa na uwezo wa kuleta uzima, haki ingepatikana kwa sheria.
22 Mais l’écriture a renfermé toutes choses sous le péché, afin que la promesse, sur le principe de [la] foi en Jésus Christ, soit donnée à ceux qui croient.
Lakini badala yake, andiko limefunga mambo yote chini ya dhambi. Mungu alifanya hivi ili kwamba ahadi yake ya kutuokoa sisi kwa imani katika Yesu Kristo iweze kupatikana kwa wale wanao amini.
23 Or avant que la foi vienne, nous étions gardés sous [la] loi, renfermés pour la foi qui devait être révélée;
Lakini kabla ya imani katika Kristo haijaja, tulikuwa tumefungwa na kuwa chini ya sheria hadi uje ufunuo wa imani.
24 de sorte que la loi a été notre conducteur jusqu’à Christ, afin que nous soyons justifiés sur le principe de [la] foi;
Kwa hiyo sheria ilifanyika kiongozi wetu hadi Kristo alipokuja, ili kwamba tuhesabiwe haki kwa imani.
25 mais, la foi étant venue, nous ne sommes plus sous un conducteur,
Sasa kwa kuwa imani imekuja, hatuko tena chini ya mwangalizi.
26 car vous êtes tous fils de Dieu par la foi dans le christ Jésus.
Kwa kuwa ninyi nyote ni watoto wa Mungu kupitia imani katika Kristo Yesu.
27 Car vous tous qui avez été baptisés pour Christ, vous avez revêtu Christ:
Wote ambao mlibatizwa katika Kristo mmejivika Kristo.
28 il n’y a ni Juif, ni Grec; il n’y a ni esclave, ni homme libre; il n’y a ni mâle, ni femelle; car vous tous, vous êtes un dans le christ Jésus.
Hakuna Myahudi wala Myunani, mtumwa wala huru, mwanaume wala mwanamke, kwa kuwa ninyi nyote ni mmoja katika Kristo Yesu.
29 Or si vous êtes de Christ, vous êtes donc [la] semence d’Abraham, héritiers selon [la] promesse.
Kama ninyi ni wa Kristo, basi ni uzao wa Ibrahimu, warithi kwa mujibu wa ahadi.

< Galates 3 >