< Galates 3 >

1 Ô Galates insensés, qui vous a ensorcelés, vous devant les yeux de qui Jésus Christ a été dépeint, crucifié [au milieu de vous]?
Ninyi Wagalatia wajinga! Ni nani aliyewaroga? Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele yenu kwamba amesulubiwa.
2 Je voudrais seulement apprendre ceci de vous: avez-vous reçu l’Esprit sur le principe des œuvres de loi, ou de l’ouïe de [la] foi?
Nataka nijifunze neno moja kutoka kwenu: Je, mlipokea Roho wa Mungu kwa kushika sheria, au kwa kuyaamini yale mliyosikia?
3 Êtes-vous si insensés? Ayant commencé par l’Esprit, achèveriez-vous maintenant par la chair?
Je, ninyi ni wajinga kiasi hicho? Baada ya kuanza kwa Roho, je, sasa mwataka kumalizia katika mwili?
4 Avez-vous tant souffert en vain, si toutefois c’est en vain?
Je, mlipata mateso kiasi hicho bure? Ni kama kweli yalikuwa bure!
5 Celui donc qui vous fournit l’Esprit et qui opère des miracles au milieu de vous, [le fait-il] sur le principe des œuvres de loi, ou de l’ouïe de [la] foi?
Je, Mungu huwapa Roho wake na kufanya miujiza katikati yenu kwa sababu mnatii sheria, au kwa sababu mnaamini kile mlichosikia?
6 comme Abraham a cru Dieu, et cela lui fut compté à justice.
Kama vile “Abrahamu alimwamini Mungu na ikahesabiwa kwake kuwa haki.”
7 Sachez donc que ceux qui sont sur le principe de [la] foi, ceux-là sont fils d’Abraham.
Fahamuni basi kwamba wale walio na imani, hao ndio watoto wa Abrahamu.
8 Or l’écriture, prévoyant que Dieu justifierait les nations sur le principe de [la] foi, a d’avance annoncé la bonne nouvelle à Abraham: « En toi toutes les nations seront bénies ».
Maandiko yakitabiri kwamba Mungu angewahesabia haki watu wa Mataifa kwa imani, alitangulia kumtangazia Abrahamu Injili akisema kwamba, “Kwa kupitia kwako mataifa yote yatabarikiwa.”
9 De sorte que ceux qui sont sur le principe de [la] foi sont bénis avec le croyant Abraham.
Kwa sababu hii, wale wote wanaoamini wanabarikiwa pamoja na Abrahamu, mtu wa imani.
10 Car tous ceux qui sont sur le principe des œuvres de loi sont sous malédiction; car il est écrit: « Maudit est quiconque ne persévère pas dans toutes les choses qui sont écrites dans le livre de la loi pour les faire ».
Kwa maana wote wanaotumainia matendo ya sheria wako chini ya laana, kwa kuwa imeandikwa, “Alaaniwe kila mtu asiyeshikilia kutii mambo yote yaliyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.”
11 Or que par [la] loi personne ne soit justifié devant Dieu, cela est évident, parce que: « Le juste vivra de foi ».
Basi ni dhahiri kwamba hakuna mtu anayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa kushikilia sheria, kwa maana, “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
12 Mais la loi n’est pas sur le principe de [la] foi, mais: « Celui qui aura fait ces choses vivra par elles ».
Lakini sheria haitegemei imani. Kinyume chake, “Mtu atendaye matendo hayo ataishi kwa hayo.”
13 Christ nous a rachetés de la malédiction de la loi, étant devenu malédiction pour nous (car il est écrit: « Maudit est quiconque est pendu au bois »),
Kristo alitukomboa kutoka laana ya sheria kwa kufanyika laana kwa ajili yetu, kwa maana imeandikwa, “Amelaaniwa yeye aangikwaye juu ya mti.”
14 afin que la bénédiction d’Abraham parvienne aux nations dans le christ Jésus, afin que nous recevions par la foi l’Esprit promis.
Alitukomboa ili kwamba baraka aliyopewa Abrahamu ipate kuwafikia watu wa Mataifa kwa njia ya Kristo Yesu, ili kwa imani tupate kupokea ile ahadi ya Roho.
15 Frères, je parle selon l’homme: personne n’annule une alliance qui est confirmée, même [celle] d’un homme, ni n’y ajoute.
Ndugu zangu, nataka nitoe mfano kutoka maisha ya kila siku. Kama vile hakuna mtu awezaye kutangua au kuongeza kitu katika agano la mtu ambalo limekwisha kuthibitishwa, vivyo hivyo kwa hali kama hii.
16 Or c’est à Abraham que les promesses ont été faites, et à sa semence. Il ne dit pas: “et aux semences”, comme [parlant] de plusieurs; mais comme [parlant] d’un seul: – « et à ta semence », qui est Christ.
Ahadi zilinenwa kwa Abrahamu na kwa mzao wake. Maandiko hayasemi “kwa wazao,” likimaanisha watu wengi, bali “kwa mzao wako,” yaani mtu mmoja, ndiye Kristo.
17 Or je dis ceci: que la loi, qui est survenue 430 ans après, n’annule point une alliance antérieurement confirmée par Dieu, de manière à rendre la promesse sans effet.
Ninachotaka kusema ni kwamba, sheria, ambayo ilitolewa miaka 430 baadaye, haitangui Agano lililothibitishwa na Mungu ili kuibatilisha ahadi ile.
18 Car si l’héritage est sur le principe de loi, il n’est plus sur le principe de promesse; mais Dieu a fait le don à Abraham par promesse.
Kwa maana kama urithi hupatikana kwa sheria, basi hautegemei tena ahadi, lakini Mungu kwa neema yake alimpa Abrahamu urithi kwa njia ya ahadi.
19 Pourquoi donc la loi? Elle a été ajoutée à cause des transgressions, jusqu’à ce que vienne la semence à laquelle la promesse est faite, ayant été ordonnée par des anges, par la main d’un médiateur.
Kwa nini basi iwepo sheria? Sheria iliwekwa kwa sababu ya makosa mpaka atakapokuja yule Mzao wa Abrahamu, ambaye alitajwa katika ile ahadi. Sheria iliamriwa na malaika kwa mkono wa mpatanishi.
20 Or un médiateur n’est pas [médiateur] d’un seul, mais Dieu est un seul.
Basi mpatanishi huhusisha zaidi ya upande mmoja, lakini Mungu ni mmoja.
21 La loi est-elle donc contre les promesses de Dieu? Qu’ainsi n’advienne! Car s’il avait été donné une loi qui ait le pouvoir de faire vivre, la justice serait en réalité sur le principe de [la] loi.
Je basi, sheria inapingana na ahadi za Mungu? La hasha! Kwa maana kama sheria iliyotolewa ingeweza kuwapa watu uzima, basi haki ingepatikana kwa njia ya sheria.
22 Mais l’écriture a renfermé toutes choses sous le péché, afin que la promesse, sur le principe de [la] foi en Jésus Christ, soit donnée à ceux qui croient.
Lakini Maandiko yamefanya vitu vyote vifungwe chini ya nguvu ya dhambi, ili yale yaliyoahidiwa kwa njia ya imani katika Yesu Kristo yapate kupewa wale wanaoamini.
23 Or avant que la foi vienne, nous étions gardés sous [la] loi, renfermés pour la foi qui devait être révélée;
Kabla imani hii haijaja tulikuwa tumewekwa chini ya sheria, tumefungwa mpaka ile imani ifunuliwe.
24 de sorte que la loi a été notre conducteur jusqu’à Christ, afin que nous soyons justifiés sur le principe de [la] foi;
Hivyo, sheria ilikuwa kiongozi kutufikisha kwa Kristo, ili tupate kuhesabiwa haki kwa imani.
25 mais, la foi étant venue, nous ne sommes plus sous un conducteur,
Lakini sasa kwa kuwa ile imani imekuja, hatusimamiwi tena na sheria.
26 car vous êtes tous fils de Dieu par la foi dans le christ Jésus.
Kwa maana ninyi nyote mmekuwa watoto wa Mungu katika Kristo Yesu kwa njia ya imani.
27 Car vous tous qui avez été baptisés pour Christ, vous avez revêtu Christ:
Kwa maana wote mliobatizwa ndani ya Kristo, mmemvaa Kristo.
28 il n’y a ni Juif, ni Grec; il n’y a ni esclave, ni homme libre; il n’y a ni mâle, ni femelle; car vous tous, vous êtes un dans le christ Jésus.
Wala hakuna tena Myahudi au Myunani, mtumwa au mtu huru, mwanaume wala mwanamke, maana nyote mmekuwa wamoja ndani ya Kristo Yesu.
29 Or si vous êtes de Christ, vous êtes donc [la] semence d’Abraham, héritiers selon [la] promesse.
Nanyi mkiwa ni mali ya Kristo, basi ninyi ni wa uzao wa Abrahamu na warithi sawasawa na ile ahadi.

< Galates 3 >