< Ruth 4 >

1 Booz monta à la porte de la ville et s'y assit. Or voici que celui qui avait droit de rachat et dont Booz avait parlé, vint à passer. Il lui dit: " Arrête-toi, assieds-toi ici, toi un tel. " Cet homme s'arrêta et s'assit.
Boazi akakwea mpaka kwenye lango la mji, akaketi pale. Yule mtu wa jamaa aliyekuwa wa karibu wa kukomboa, ambaye Boazi alimtaja, akaja. Boazi akasema, “Njoo hapa, rafiki yangu. Karibu uketi.” Naye akakaribia, akaketi.
2 Alors Booz prit dix hommes parmi les anciens de la ville, et il dit: " Asseyez-vous ici. " Et ils s'assirent.
Boazi akatwaa watu kumi miongoni mwa wazee wa mji, akawaambia, “Ketini hapa.” Nao wakaketi.
3 Il dit à celui qui avait le droit de rachat: " La portion de champ qui appartenait à notre frère Elimélech, a été vendue par Noémi, qui est revenue des champs de Moab.
Kisha akamwambia yule jamaa wa karibu wa kukomboa, “Naomi, aliyerudi hapa kutoka nchi ya Moabu, anauza sehemu ya ardhi iliyokuwa mali ya ndugu yetu Elimeleki.
4 Et j'ai dit: je veux t'en informer et te dire: Achète-la en présence de ceux qui siègent ici, et en présence des anciens de mon peuple. Si tu veux racheter, rachète; si tu ne veux pas, déclare-le-moi, afin que je le sache; car il n'y a personne avant toi qui ait le droit de rachat; moi, je viens après toi. " Il répondit: " Je rachèterai. "
Nami niliwaza nikujulishe wewe na kukuambia uinunue mbele ya hawa waliopo hapa, na mbele ya wazee wa watu wangu. Kama wewe utaikomboa, haya fanya hivyo. Lakini kama hutaikomboa, uniambie, ili nijue. Kwa kuwa hakuna mtu mwingine mwenye haki ya kuikomboa ila wewe na baada yako ni mimi.” Naye akasema, “Nitaikomboa mimi.”
5 Et Booz dit: " Le jour où tu acquerras le champ de la main de Noémi, tu l'acquerras en même temps de Ruth la Moabite, femme du défunt, pour faire revivre le nom du défunt dans son héritage. "
Ndipo Boazi akasema “Siku utakaponunua hiyo ardhi kutoka kwa Naomi na Ruthu, Mmoabu, itakubidi kumchukua pia huyo mjane, ili kudumisha jina la marehemu pamoja na mali yake.”
6 Celui qui avait le droit de rachat répondit: " Je ne puis pas le racheter pour mon compte, de peur de détruire mon propre héritage. Fais usage de mon droit de rachat, car je ne puis racheter. "
Aliposikia hili, yule jamaa wa karibu wa kukomboa akasema, “Basi mimi sitaweza kuikomboa, kwa sababu inaonekana nitauhatarisha urithi wangu. Wewe ikomboe mwenyewe. Mimi sitaweza.”
7 C'était autrefois la coutume en Israël, en cas de rachat et d'échange, pour valider toute affaire, que l'homme ôtât son soulier et le donnât à l'autre cela servait de témoignage en Israël.
(Basi katika siku za kale huko Israeli, ili kukamilisha tendo la kukomboa na kukabidhiana mali, mmoja huvua kiatu chake na kumpatia mwingine. Hii ilikuwa ni njia ya kuhalalisha mabadilishano katika Israeli.)
8 Celui qui avait le droit de rachat dit à Booz " Acquiers pour ton compte. " Et il ôta son soulier.
Basi yule jamaa wa karibu wa kukomboa akamwambia Boazi, “Wewe inunue mwenyewe.” Naye huyo jamaa akavua kiatu chake.
9 Et Booz dit aux anciens et à tout le peuple: " Vous êtes témoins aujourd'hui que j'ai acquis de la main de Noémi tout ce qui appartenait à Elimélech, et tout ce qui appartenait à Cheljon et à Mahalon,
Kisha Boazi akawatangazia wazee na watu wote waliokuwepo, “Leo ninyi ni mashahidi kwamba mimi nimenunua kutoka kwa Naomi yote yaliyokuwa mali ya Elimeleki, Kilioni na Maloni.
10 et que j'ai acquis en même temps pour femme Ruth la Moabite, femme de Mahalon, pour faire revivre le nom du défunt dans son héritage, afin que le nom du défunt ne soit point retranche d'entre ses frères et de la porte de son lieu. Vous en êtes témoins en ce jour! "
Nimemchukua pia Ruthu, Mmoabu, mjane wa Maloni, awe mke wangu, ili kuendeleza jina la marehemu pamoja na mali zake, ili jina lake marehemu lisitoweke miongoni mwa jamaa yake, wala katika kumbukumbu za mji wake. Leo hivi ninyi ni mashahidi!”
11 Tout le peuple qui était à la porte et les anciens dirent: " Nous en sommes témoins. Que Yahweh rende la femme qui entre dans ta maison semblable à Rachel et à Lia, qui toutes les deux ont bâti la maison d'Israël! Sois fort dans Ephrata, et fais-toi un nom dans Bethléem!
Kisha wazee pamoja na watu wote waliokuwa langoni wakasema, “Sisi ni mashahidi. Bwana na amfanye mwanamke huyu aingiaye nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea, wale wanawake wawili ambao pamoja waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe ufanikiwe katika Efrathi na uwe mashuhuri katika Bethlehemu.
12 Puisse ta maison être semblable à la maison de Pharès, — que Thamar enfanta à Juda, — par la postérité que Yahweh te donnera de cette jeune femme! "
Kupitia kwa watoto ambao Bwana atakupa kutokana na huyu mwanamwali, jamaa yako na ifanane na ya Peresi, ambaye Tamari alimzalia Yuda.”
13 Booz prit Ruth, et elle fut sa femme, et il alla vers elle. Yahweh donna à Ruth de concevoir, et elle enfanta un fils.
Basi Boazi akamwoa Ruthu, naye akawa mke wake. Alipoingia kwake, Bwana akamjalia Ruthu, naye akapata mimba, akamzaa mtoto wa kiume.
14 Les femmes dirent à Noémi: " Béni soit Yahweh, qui ne t'a point laissé manquer aujourd'hui d'un rédempteur! Que son nom devienne célèbre en Israël!
Wanawake wakamwambia Naomi: “Ahimidiwe Bwana, asiyekuacha bila kuwa na jamaa wa karibu wa kukomboa. Na awe mashuhuri katika Israeli yote!
15 Il restaurera ton âme et sera le soutien de ta vieillesse! Car ta belle-fille, qui t'aime, l'a enfanté, elle qui vaut mieux pour toi que sept fils. "
Atakurejeshea uhai wako na kukuangalia katika siku za uzee wako. Kwa maana mkweo ambaye anakupenda, na ambaye kwako ni bora zaidi ya watoto wa kiume saba, ndiye alimzaa.”
16 Noémi prit l'enfant, le mit sur son sein, et elle lui servit de nourrice.
Basi Naomi akamchukua yule mtoto, akampakata na akawa mlezi wake.
17 Les voisines lui donnèrent un nom, en disant: " Un fils est né à Noémi! " Et elles l'appelèrent Obed. Ce fut le père d'Isaï, père de David.
Wanawake waliokuwa jirani zake wakasema, “Naomi ana mtoto wa kiume.” Wakamwita jina lake Obedi. Yeye ndiye baba yake Yese, aliye baba yake Daudi.
18 Voici la postérité de Pharès: Pharès engendra Esron;
Hivi ndivyo vizazi vya Peresi: Peresi alimzaa Hesroni,
19 Esron engendra Aram; Aram engendra Aminadab;
Hesroni akamzaa Ramu, Ramu akamzaa Aminadabu,
20 Aminadab engendra Nahasson; Nahasson engendra Salmon;
Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,
21 Salmon engendra Booz; Booz engendra Obed;
Salmoni akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obedi,
22 Obed engendra Isaï: Isaï engendra David. "
Obedi akamzaa Yese, na Yese akamzaa Daudi.

< Ruth 4 >