< Marc 1 >

1 Commencement de l'Évangile de Jésus-Christ, Fils de Dieu.
Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2 Selon ce qui est écrit dans le prophète Isaïe: " Voilà que j'envoie mon messager devant vous, pour vous frayer le chemin.
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako”:
3 Une voix crie dans le désert: Préparez le chemin du Seigneur, aplanissez ses sentiers. "
“sauti ya mtu aliaye nyikani. ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’”
4 Jean parut, baptisant dans le désert, et prêchant le baptême de pénitence pour la rémission des péchés.
Yohana alikuja, akibatiza huko nyikani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
5 Tout le pays de Judée et tous les habitants de Jérusalem venaient à lui, et, confessant leurs péchés, ils recevaient de lui le baptême dans le fleuve du Jourdain.
Watu kutoka Uyahudi wote na sehemu zote za Yerusalemu walikuwa wakimwendea. Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
6 Or, Jean était vêtu de poils de chameau; il avait autour de ses reins une ceinture de cuir, et se nourrissait de sauterelles et de miel sauvage. Et il prêchait ainsi:
Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
7 " Il vient après moi, celui qui est plus puissant que moi, et je ne suis pas digne de délier, en me baissant, les cordons de sa chaussure.
Naye alihubiri akisema, “Baada yangu atakuja yeye aliye na uwezo kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kuinama na kulegeza kamba za viatu vyake.
8 Moi, je vous ai baptisés dans l'eau, mais lui vous baptisera dans le Saint-Esprit. "
Mimi nawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
9 Or, il arriva en ces jours-là que Jésus vint de Nazareth, ville de Galilée, et il fut baptisé par Jean dans le Jourdain.
Wakati huo Yesu akaja kutoka Nazareti ya Galilaya, naye akabatizwa na Yohana katika Mto Yordani.
10 Et, comme il sortait de l'eau, il vit les cieux s'ouvrir et l'Esprit-Saint descendre sur lui comme une colombe.
Yesu alipokuwa akitoka ndani ya maji, aliona mbingu zikifunguka na Roho akishuka juu yake kama hua.
11 Et du ciel une voix se fit entendre: " Tu es mon Fils bien-aimé, en toi j'ai mis mes complaisances. "
Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
12 Et aussitôt L'Esprit poussa Jésus au désert.
Wakati huo huo, Roho akamwongoza Yesu kwenda nyikani,
13 Et il y demeura quarante jours, tenté par Satan; il était parmi les bêtes sauvages, et les anges le servaient.
naye akawa huko nyikani kwa muda wa siku arobaini, akijaribiwa na Shetani. Alikaa na wanyama wa mwituni, nao malaika wakamhudumia.
14 Après que Jean eut été mis en prison, Jésus vint en Galilée, prêchant l'Évangile du royaume de Dieu.
Baada ya Yohana kukamatwa na kutiwa gerezani, Yesu aliingia Galilaya akaanza kuhubiri habari njema ya Mungu,
15 Il disait: " Le temps est accompli, et le royaume de Dieu est proche; repentez-vous et croyez à l'Évangile. "
akisema, “Wakati umewadia, Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema.”
16 Passant le long de la mer de Galilée, il vit Simon et André son frère qui jetaient leurs filets dans la mer, car ils étaient pêcheurs.
Yesu alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
17 Jésus leur dit: " Venez à ma suite, et je vous ferai devenir pêcheurs d'hommes. "
Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
18 Aussitôt, laissant leurs filets, ils le suivirent.
Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.
19 Un peu plus loin, il vit Jacques, fils de Zébédée, et Jean son frère, qui étaient, eux aussi, dans une barque, réparant leurs filets.
Alipokwenda mbele kidogo, akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa kwenye mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20 Il les appela aussitôt; et, laissant leur père Zébédée dans la barque avec les mercenaires, ils le suivirent.
Papo hapo akawaita, nao wakamwacha Zebedayo baba yao kwenye mashua pamoja na watumishi wa kuajiriwa, nao wakamfuata Yesu.
21 Ils se rendirent à Capharnaüm, et dès le premier sabbat, Jésus entrant dans la synagogue, se mit à enseigner.
Wakaenda mpaka Kapernaumu. Ilipofika siku ya Sabato, mara Yesu akaingia sinagogi, akaanza kufundisha.
22 Et ils étaient frappés de sa doctrine, car il les enseignait comme ayant autorité, et non comme les Scribes.
Watu wakashangaa sana kwa mafundisho yake, kwa maana aliwafundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wa sheria.
23 Or il se trouva dans leur synagogue un homme possédé d'un esprit impur, qui s'écria:
Wakati huo huo katika sinagogi lao palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu,
24 " Qu'avons-nous à faire avec vous, Jésus de Nazareth? Vous êtes venu pour nous perdre! Je sais qui vous êtes, le Saint de Dieu. "
naye akapiga kelele akisema, “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
25 Mais Jésus, lui parlant avec menace: " Tais-toi, dit-il, et sors de cet homme. "
Lakini Yesu akamkemea, akamwambia, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!”
26 Et l'esprit impur, l'agitant violemment, sortit de lui en jetant un grand cri.
Yule pepo mchafu akamtikisatikisa huyo mtu kwa nguvu, kisha akamtoka akipiga kelele kwa sauti kubwa.
27 Tous furent saisis d'étonnement, de sorte qu'ils se demandaient entre eux: " Qu'est-ce que ceci? Quelle est cette doctrine nouvelle? Car il commande en maître, même aux esprits impurs, et ils lui obéissent. "
Watu wote wakashangaa, hata wakaulizana wao kwa wao, “Haya ni mambo gani? Ni mafundisho mapya, tena yenye mamlaka! Anaamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
28 Et sa renommée se répandit aussitôt dans tout le pays qui avoisine la Galilée.
Sifa zake zikaanza kuenea haraka katika eneo lote la karibu na Galilaya.
29 En sortant de la synagogue, ils allèrent aussitôt dans la maison de Simon et d'André, avec Jacques et Jean.
Mara walipotoka katika sinagogi, walikwenda pamoja na Yakobo na Yohana hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea.
30 Or, la belle-mère de Simon était au lit, ayant la fièvre; aussitôt ils parlèrent d'elle à Jésus.
Mama mkwe wa Simoni alikuwa kitandani, ana homa, nao wakamweleza Yesu habari zake.
31 Il s'approcha et la fit lever, en la prenant par la main; au même instant la fièvre la quitta, et elle se mit à les servir.
Hivyo Yesu akamwendea, akamshika mkono na kumwinua. Kisha homa ikamwacha, naye akaanza kuwahudumia.
32 Sur le soir, après le coucher du soleil, il lui amenèrent tous les malades et les démoniaques,
Jioni ile baada ya jua kutua, watu wakamletea Yesu wagonjwa wote na waliopagawa na pepo wachafu.
33 et toute la ville se pressait devant la porte.
Mji wote ukakusanyika mbele ya nyumba hiyo.
34 Il guérit beaucoup de malades affligés de diverses infirmités, et il chassa beaucoup de démons; mais il ne leur permettait pas de parler, parce qu'ils le connaissaient.
Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa ya aina mbalimbali. Akawatoa pepo wachafu wengi, lakini hakuwaacha hao pepo wachafu waseme, kwa sababu walimjua yeye ni nani.
35 Le lendemain, s'étant levé longtemps avant le jour, il sortit, alla dans un lieu solitaire, et il y pria.
Alfajiri na mapema sana kulipokuwa bado kuna giza, Yesu akaamka, akaondoka, akaenda mahali pa faragha ili kuomba.
36 Simon et ceux qui étaient avec lui se mirent à sa recherche;
Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta,
37 et l'ayant trouvé, ils lui dirent: " Tout le monde vous cherche. "
nao walipomwona, wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta!”
38 Il leur répondit: " Allons ailleurs dans les bourgades voisines, afin que j'y prêche aussi; car c'est pour cela que je suis sorti. "
Yesu akawajibu, “Twendeni mahali pengine kwenye vijiji jirani, ili niweze kuhubiri huko pia, kwa sababu hicho ndicho nilichokuja kukifanya.”
39 Et il prêchait dans leurs synagogues, parcourant la Galilée entière, et chassait les démons.
Kwa hiyo akazunguka Galilaya kote, akihubiri katika masinagogi yao na kutoa pepo wachafu.
40 Un lépreux vint à lui, et se jetant à ses genoux, il lui dit d'un ton suppliant: " Si vous voulez, vous pouvez me guérir. "
Mtu mmoja mwenye ukoma alimjia Yesu, akamwomba akipiga magoti, akamwambia, “Ukitaka, waweza kunitakasa.”
41 Emu de compassion, Jésus étendit la main, et le toucha, en disant: " Je le veux, sois guéri. "
Yesu, akiwa amejawa na huruma, akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Nataka. Takasika!”
42 Et dès qu'il eut parlé, la lèpre quitta cet homme, et il fut guéri.
Mara ukoma ukamtoka, naye akatakasika.
43 Aussitôt Jésus le renvoya, en lui disant d'un ton sévère:
Baada ya Yesu kumwonya vikali, akamruhusu aende zake
44 " Garde-toi d'en parler à personne; mais va te montrer au prêtre, et offre pour ta guérison ce que Moïse a ordonné pour l'attester au peuple. "
akimwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote habari hizi, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
45 Mais cet homme étant parti, se mit à raconter et à publier partout ce qui s'était passé: de sorte que Jésus ne pouvait plus entrer publiquement dans une ville; il se tenait dehors, dans des lieux solitaires, et l'on venait à lui de tous côtés.
Lakini yule mtu akaenda akaanza kutangaza habari za kuponywa kwake waziwazi. Kwa hiyo, Yesu hakuweza tena kuingia katika miji waziwazi lakini alikaa sehemu zisizo na watu. Hata hivyo watu wakamfuata huko kutoka kila upande.

< Marc 1 >