< Luc 4 >

1 Jésus, rempli de l'Esprit-Saint, revint du Jourdain, et il fut poussé par l'Esprit dans le désert,
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
2 pendant quarante jours, en butte aux tentations du diable. Il ne mangea rien durant ces jours-là, et quand ils furent passés, il eut faim.
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
3 Alors le diable lui dit: " Si vous êtes Fils de Dieu, commandez à cette pierre de se changer en pain. "
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
4 Jésus lui répondit: " Il est écrit: L'homme ne vit pas seulement de pain, mais de toute parole de Dieu. "
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
5 Et le diable l'ayant emmené sur une haute montagne, lui montra en un instant tous les royaumes de la terre,
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
6 et lui dit: " Je vous donnerai toute cette puissance et toute la gloire de ces royaumes; car elle m'a été livrée, et je la donne à qui je veux.
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7 Si donc vous vous prosternez devant moi, elle sera toute à vous. "
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
8 Jésus lui répondit: " Il est écrit: Tu adoreras le Seigneur ton Dieu, et tu le serviras lui seul. "
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
9 Le démon le conduisit encore à Jérusalem, et l'ayant placé sur le pinacle du temple, il lui dit: " Si vous êtes Fils de Dieu, jetez-vous d'ici en bas.
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
10 Car il est écrit: Il a été donné pour vous l'ordre à ses anges de vous garder,
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
11 et ils vous prendront entre leurs mains, de peur que votre pied ne heurte contre la pierre. "
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
12 Jésus lui répondit: " Il a été écrit: Tu ne tenteras point le Seigneur ton Dieu. "
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 Après l'avoir ainsi tenté de toutes manières, le diable se retira de lui pour un temps.
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
14 Alors Jésus retourna en Galilée, dans la puissance de l'Esprit, et sa renommée se répandit dans tout le pays d'alentour.
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15 Il enseignait dans leurs synagogues, et tous publiaient ses louanges.
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16 Etant venu à Nazareth, où il avait été élevé, il entra, selon sa coutume, le jour du sabbat dans la synagogue, et se leva pour faire la lecture.
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
17 On lui remit le livre du prophète Isaïe; et l'ayant déroulé, il trouva l'endroit où il était écrit:
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18 " L'Esprit du Seigneur est sur moi, parce qu'il m'a consacré par son onction, pour porter la bonne nouvelle aux pauvres, et il m'a envoyé guérir ceux qui ont le cœur brisé,
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
19 annoncer aux captifs la délivrance, aux aveugles le retour à la vue, pour rendre libres les opprimés, publier l'année favorable du Seigneur. "
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20 Ayant roulé le livre, il le rendit au ministre et s'assit; et tous, dans la synagogue, avaient les yeux attachés sur lui.
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21 Alors, il commença à leur dire: " Aujourd'hui vos oreilles ont entendu l'accomplissement de cet oracle. "
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
22 Et tous lui rendaient témoignage, et admirant les paroles de grâce qui sortaient de sa bouche, ils disaient: " N'est-ce pas là le fils de Joseph? "
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
23 Et il leur dit: " Sans doute, vous m'alléguerez cet adage: Médecin, guéris-toi toi-même; et vous me direz: Les grandes choses que nous avons ouï dire que vous avez faites à Capharnaüm, faites-les ici dans votre patrie. "
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
24 Et il ajouta: " En vérité, je vous le dis, aucun prophète n'est bien reçu dans sa patrie.
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
25 Je vous le dis, en vérité, il y avait beaucoup de veuves en Israël aux jours d'Elie, lorsque le ciel fut fermé pendant trois ans et six mois, et qu'il y eut une grande famine dans toute la terre;
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 et pourtant Elie ne fut envoyé à aucune d'elles, mais à une veuve de Sarepta, dans le pays de Sidon.
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
27 Il y avait de même beaucoup de lépreux en Israël au jours du prophète Elisée; et pourtant aucun d'eux ne fut guéri, mais bien Naaman le Syrien. "
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
28 En entendant cela, ils furent tous remplis de colère dans la synagogue.
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
29 Et s'étant levés, ils le poussèrent hors de la ville, et le menèrent jusqu'à un escarpement de la montagne sur laquelle leur ville était bâtie pour le précipiter en bas.
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
30 Mais lui, passant au milieu d'eux, s'en alla.
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
31 Il descendit à Capharnaüm, ville de Galilée, et là il enseignait les jours de sabbat.
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
32 Et sa doctrine les frappait d'étonnement, parce qu'il parlait avec autorité.
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
33 Il y avait dans la synagogue un homme possédé d'un démon impur, lequel jeta un grand cri,
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
34 disant: " Laissez-moi, qu'avons-nous à faire avec vous, Jésus de Nazareth? Etes-vous venu pour nous perdre? Je sais qui vous êtes: le Saint de Dieu. "
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
35 Mais Jésus lui dit d'un ton sévère: " Tais-toi, et sors de cet homme. " Et le démon l'ayant jeté par terre au milieu de l'assemblée, sortit de lui sans lui avoir fait aucun mal.
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
36 Et tous, saisis de stupeur, se disaient entre eux: " Quelle est cette parole? Il commande avec autorité et puissance aux esprits impurs, et ils sortent! "
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
37 Et sa renommée se répandait de tous côtés dans le pays.
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
38 S'étant alors levé, Jésus quitta la synagogue, et entra dans la maison de Simon. Or, la belle-mère de Simon était atteinte d'une grosse fièvre, et ils le prièrent pour elle.
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
39 Se penchant sur la malade, il commanda à la fièvre, et la fièvre la quitta; et s'étant levée aussitôt, elle se mit à les servir.
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
40 Lorsque le soleil fut couché, tous ceux qui avaient chez eux des malades, quel que fût leur mal, les lui amenèrent; et Jésus, imposant la main à chacun d'eux, les guérit.
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
41 Des démons aussi sortaient de plusieurs, criant et disant: " Tu es le Fils de Dieu "; et il les réprimandait pour leur imposer silence, parce qu'ils savaient qu'il était le Christ.
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
42 Dès que le jour parut, il sortit et s'en alla en un lieu désert. Une foule de gens se mirent à sa recherche, et étant arrivés jusqu'à lui, ils voulaient le retenir, pour qu'il ne les quittât point.
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
43 Mais il leur dit: " Il faut que j'annonce aussi aux autres villes le royaume de Dieu, car je suis envoyé pour cela. "
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
44 Et Jésus prêchait dans les synagogues de la Galilée.
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.

< Luc 4 >