< Jacques 2 >

1 Mes frères, n'alliez aucune acception de personnes avec la foi en Jésus-Christ notre Seigneur de gloire.
Ndugu zangu, kama waaminio katika imani ya Bwana wetu Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, msiwe na upendeleo kwa watu.
2 Si, par exemple, il entre dans votre assemblée un homme qui ait un anneau d'or et un vêtement magnifique, et qu'il y entre aussi un pauvre avec un habit sordide;
Kwa maana kama akija mtu katika kusanyiko lenu akiwa amevaa pete ya dhahabu na mavazi mazuri, pia akaingia mtu maskini mwenye mavazi yaliyochakaa,
3 et que tournant vos regards vers celui qui est magnifiquement vêtu, vous lui disiez: " Vous, asseyez-vous ici, à cette place d'honneur ", et que vous disiez au pauvre: " Toi, tiens-toi là debout, ou assieds-toi ici, au bas de mon marchepied: "
nanyi mkampa heshima yule aliyevaa mavazi mazuri na kumwambia, “Keti hapa mahali pazuri,” lakini yule maskini mkamwambia, “Wewe simama pale,” au “Keti hapa sakafuni karibu na miguu yangu,”
4 n'est-ce pas faire entre vous des distinctions, et vous établir juges aux pensées perverses?
je, hamjawabagua na kuwa mahakimu mioyoni mwenu mkihukumu kwa mawazo yenu maovu?
5 Ecoutez, mes frères bien-aimés: Dieu n'a-t-il pas choisi ceux qui sont pauvres aux yeux du monde, pour être riches dans la foi et héritiers du royaume qu'il a promis à ceux qui l'aiment?
Ndugu zangu, sikilizeni: Je, Mungu hakuwachagua wale walio maskini machoni pa ulimwengu kuwa matajiri katika imani na kuurithi Ufalme aliowaahidi wale wampendao?
6 Et vous, vous faites affront au pauvre! Ne sont-ce pas les riches qui vous oppriment et qui vous traînent devant les tribunaux?
Lakini ninyi mmemdharau yule aliye maskini. Je, hao matajiri si ndio wanaowadhulumu na kuwaburuta mahakamani?
7 Ne sont-ce pas eux qui outragent le beau nom que vous portez?
Je, si wao wanaolikufuru Jina lile lililo bora sana mliloitiwa?
8 Que si vous accomplissez la loi royale, selon ce passage de l'Ecriture: " Tu aimeras ton prochain comme toi-même ", vous faites bien.
Kama kweli mnaitimiza ile sheria ya kifalme inayopatikana katika Maandiko isemayo, “Mpende jirani yako kama unavyoipenda nafsi yako,” mnafanya vyema.
9 Mais si vous faites acception des personnes, vous commettez un péché, et la loi elle-même vous condamne comme transgresseurs.
Lakini kama mnakuwa na upendeleo kwa watu, mnatenda dhambi, na sheria inawahukumu kuwa ninyi ni wakosaji.
10 Car quiconque aura observé toute la loi, s'il vient à faillir en un seul point, est coupable de tous.
Kwa maana mtu yeyote anayeishika sheria yote lakini akajikwaa katika kipengele kimoja tu, ana hatia ya kuivunja sheria yote.
11 En effet, celui qui a dit: " Tu ne commettras point d'adultère ", a dit aussi: " Tu ne tueras point. " Si donc tu tues, quoique tu ne commettes point d'adultère, tu es transgresseur de la loi.
Kwa sababu yeye aliyesema, “Usizini,” alisema pia, “Usiue.” Basi kama huzini lakini unaua, umekuwa mvunjaji wa sheria.
12 Parlez et agissez comme devant être jugés par la loi de liberté.
Hivyo semeni na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria ile iletayo uhuru.
13 Car le jugement sera sans miséricorde pour celui qui n'aura pas fait miséricorde; la miséricorde triomphe du jugement.
Kwa kuwa hukumu bila huruma itatolewa kwa mtu yeyote asiyekuwa na huruma. Huruma huishinda hukumu.
14 Que sert-il, mes frères, à un homme de dire qu'il a la foi, s'il n'a pas les œuvres? Est-ce que cette foi pourra le sauver?
Ndugu zangu, yafaa nini ikiwa mtu atadai kuwa anayo imani lakini hana matendo? Je, imani kama hiyo yaweza kumwokoa?
15 Si un frère ou une sœur sont dans la nudité et n'ont pas ce qui leur est nécessaire chaque jour de nourriture,
Ikiwa ndugu yako au dada hana mavazi wala chakula,
16 et que l'un de vous leur dise: " Allez en paix, chauffez-vous et vous rassasiez ", sans leur donner ce qui est nécessaire à leur corps, à quoi cela sert-il?
mmoja wenu akamwambia, “Enenda zako kwa amani, ukaote moto na kushiba,” pasipo kumpatia yale mahitaji ya mwili aliyopungukiwa, yafaa nini?
17 Il en est de même de la foi: si elle n'a pas les œuvres, elle est morte en elle-même.
Vivyo hivyo, imani peke yake kama haikuambatana na matendo, imekufa.
18 Mais on pourrait même dire: " Tu as la foi, et moi, j'ai les œuvres. " Montre-moi ta foi sans les œuvres et moi, je te montrerai ma foi par mes œuvres.
Lakini mtu mwingine atasema, “Wewe unayo imani; mimi ninayo matendo.” Nionyeshe imani yako pasipo matendo nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo.
19 Tu crois qu'il y a un seul Dieu, tu fais bien; les démons le croient aussi..., et ils tremblent!
Unaamini kwamba kuna Mungu mmoja. Vyema! Hata mashetani yanaamini hivyo na kutetemeka.
20 Mais veux-tu te convaincre, ô homme vain, que la foi sans les œuvres est sans vertu?
Ewe mpumbavu! Je, wataka kujua kwamba imani bila matendo haifai kitu?
21 Abraham, notre père, ne fut-il pas justifié par les œuvres, lorsqu'il offrit son fils Isaac sur l'autel?
Je, Abrahamu baba yetu hakuhesabiwa haki kwa kile alichotenda, alipomtoa mwanawe Isaki madhabahuni?
22 Tu vois que la foi coopérait à ses œuvres, et que par les œuvres sa foi fut rendue parfaite.
Unaona jinsi ambavyo imani yake na matendo yake vilikuwa vinatenda kazi pamoja, nayo imani yake ikakamilishwa na kile alichotenda.
23 Et la parole de l'Ecriture s'accomplit: " Abraham crut à Dieu, et cela lui fut imputé à justice ", et il fut appelé ami de Dieu.
Kwa njia hiyo yakatimizwa yale Maandiko yasemayo, “Abrahamu alimwamini Mungu na ikahesabiwa kwake kuwa haki,” naye akaitwa rafiki wa Mungu.
24 Vous voyez que l'homme est justifié par les œuvres, et non par la foi seulement.
Mnaona ya kwamba mtu huhesabiwa haki kwa yale anayotenda wala si kwa imani peke yake.
25 De même Rahab, la courtisane, ne fut-elle pas justifiée par les œuvres, quand elle reçut les envoyés de Josué et les fit partir par un autre chemin?
Vivyo hivyo, hata Rahabu, yule kahaba, hakuhesabiwa haki kwa yale aliyotenda alipowapokea wale wapelelezi na kuwaambia waende njia nyingine?
26 De même que le corps sans âme est mort, ainsi la foi sans les œuvres est morte.
Kama vile ambavyo mwili pasipo roho umekufa, kadhalika nayo imani pasipo matendo imekufa.

< Jacques 2 >