< Luc 10 >

1 Or, après ces choses, le Seigneur en désigna soixante-dix autres, et les envoya deux par deux devant lui dans toutes les villes et dans tous les lieux où il allait venir.
Baada ya hayo, Bwana aliwachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawiliwawili, wamtangulie katika kila kijiji na mahali ambapo yeye mwenyewe alitaka kwenda.
2 Puis il leur dit: « La moisson est abondante, mais les ouvriers sont peu nombreux. Priez donc le maître de la moisson, afin qu'il envoie des ouvriers dans sa moisson.
Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache. Kwa hivyo, mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake.
3 Allez par là. Voici, je vous envoie comme des agneaux au milieu des loups.
Sasa nendeni; fahamuni kwamba ninawatuma ninyi kama kondoo wanaokwenda kati ya mbwa mwitu.
4 Ne portez ni bourse, ni porte-monnaie, ni sandales. Ne saluez personne en chemin.
Msichukue mfuko wa fedha, mkoba, wala viatu; msimsalimu mtu yeyote njiani.
5 Dans quelque maison que vous entriez, dites d'abord: « Que la paix soit avec cette maison ».
Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza wasalimuni hivi: Amani iwe katika nyumba hii!
6 S'il s'y trouve un fils de paix, votre paix reposera sur lui; sinon, elle reviendra à vous.
Kama akiwako mwenye kupenda amani, amani yenu itakaa naye, la sivyo, itawarudieni.
7 Reste dans cette même maison, mange et bois ce qu'on te donne, car l'ouvrier mérite son salaire. Ne va pas de maison en maison.
Kaeni katika nyumba hiyo mkila na kunywa wanavyowapeni, maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msiende mara nyumba hii mara nyumba ile.
8 Dans quelque ville que vous entriez et où l'on vous reçoit, mangez ce qui vous est présenté.
Kama mkifika mji fulani na watu wakiwakaribisha, kuleni wanavyowapeni.
9 Guérissez les malades qui sont là et dites-leur: « Le Royaume de Dieu s'est approché de vous ».
Ponyeni wagonjwa walioko huko, waambieni watu: Ufalme wa Mungu umekaribia kwenu.
10 Mais dans quelque ville que vous entriez, et où l'on ne vous recevra pas, sortez dans ses rues et dites:
Lakini mkiingia katika mji wowote, wasipowakaribisheni, tokeni; nanyi mpitapo katika barabara zao semeni:
11 « Nous essuyons contre vous la poussière de votre ville qui s'est attachée à nous. Mais sachez que le Royaume de Dieu s'est approché de vous ».
Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu tunawakung'utieni. Lakini, jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
12 Je vous le dis, en ce jour-là, il sera plus supportable pour Sodome que pour cette ville.
Hakika nawaambieni, siku ile mji huo utapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Sodoma.
13 « Malheur à toi, Chorazin! Malheur à toi, Bethsaïda! Car s'il s'était fait à Tyr et à Sidon les miracles qui ont été faits chez vous, il y a longtemps qu'elles se seraient repenties, assises sur le sac et la cendre.
“Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika kule Tiro na Sidoni, watu wake wangalikwishavaa mavazi ya gunia kitambo, na kukaa katika majivu kuonyesha kwamba wametubu.
14 Mais, au jugement, Tyr et Sidon seront plus tolérables que vous.
Hata hivyo, Siku ya Hukumu ninyi mtapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Tiro na Sidoni.
15 Toi, Capharnaüm, qui es élevée jusqu'au ciel, tu seras abaissée jusqu'au séjour des morts. (Hadēs g86)
Na wewe Kafarnaumu, unataka kujikweza mpaka mbinguni? La; utaporomoshwa mpaka Kuzimu.” (Hadēs g86)
16 Celui qui vous écoute m'écoute, et celui qui vous rejette me rejette. Celui qui me rejette rejette celui qui m'a envoyé. »
Halafu akasema, “Anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; na anayekataa kuwapokea ninyi, anakataa kunipokea mimi. Yeyote anayekataa kunipokea, anakataa kumpokea yule aliyenituma.”
17 Les soixante-dix revinrent avec joie, disant: « Seigneur, même les démons nous sont soumis en ton nom! ».
Baadaye, wale sabini na wawili walirudi wamejaa furaha, wakisema, “Bwana, hata pepo wametutii tulipolitaja jina lako.”
18 Il leur dit: « J'ai vu Satan tomber du ciel comme un éclair.
Yeye akawaambia, “Nilimwona Shetani jinsi alivyokuwa anaporomoka kama umeme kutoka mbinguni.
19 Voici, je vous donne le pouvoir de marcher sur les serpents et les scorpions, et sur toute la puissance de l'ennemi. Rien ne pourra vous faire du mal.
Naam, nimewapeni uwezo wa kukanyaga nyoka na ng'e, na uwezo juu ya nguvu zote za yule adui; hakuna chochote kitakachowadhuru.
20 Cependant, ne vous réjouissez pas de ce que les esprits vous sont soumis, mais réjouissez-vous de ce que vos noms sont inscrits dans les cieux. »
Hata hivyo, msifurahi kwa sababu pepo wamewatii, bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.”
21 A cette même heure, Jésus se réjouit dans l'Esprit Saint et dit: « Je te rends grâce, ô Père, Seigneur du ciel et de la terre, d'avoir caché ces choses aux sages et aux intelligents, et de les avoir révélées aux petits enfants. Oui, Père, car c'est ainsi qu'il a été agréable à tes yeux. »
Saa ileile, Yesu akafurahi kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akasema, “Nakushukuru ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa kuwa umewaficha wenye hekima na elimu mambo haya, ukawafumbulia wadogo. Naam, Baba, ndivyo ilivyokupendeza.”
22 Se tournant vers les disciples, il dit: « Toutes choses m'ont été remises par mon Père. Personne ne sait qui est le Fils, si ce n'est le Père, et qui est le Père, si ce n'est le Fils, et celui à qui le Fils veut le révéler. »
Kisha akasema, “Baba yangu ameweka yote mikononi mwangu. Hakuna amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala amjuaye Baba ni nani ila Mwana, na yeyote yule ambaye Mwana anataka kumfunulia hayo.”
23 Se tournant vers les disciples, il leur dit en privé: « Heureux les yeux qui voient les choses que vous voyez,
Halafu akawaelekea wafuasi wake akawaambia, “Heri wanaoona yale mnayoyaona ninyi!
24 car je vous dis que beaucoup de prophètes et de rois ont désiré voir les choses que vous voyez, et ne les ont pas vues, et entendre les choses que vous entendez, et ne les ont pas entendues. »
Hakika, manabii na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona ninyi wasiyaone, na kusikia yale mnayoyasikia wasiyasikie.”
25 Voici qu'un docteur de la loi se leva et l'éprouva, disant: « Maître, que dois-je faire pour hériter la vie éternelle? » (aiōnios g166)
Baadaye mwalimu mmoja wa Sheria alisimama akamwuliza akitaka kumtega, “Mwalimu, nifanye nini ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
26 Il lui dit: « Qu'est-ce qui est écrit dans la loi? Comment la lis-tu? »
Yesu akamwuliza, “Imeandikwa nini katika Sheria? Unaelewaje?”
27 Il répondit: « Tu aimeras le Seigneur ton Dieu de tout ton cœur, de toute ton âme, de toute ta force et de toute ta pensée, et ton prochain comme toi-même. »
Akamjibu, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote. Na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
28 Il lui dit: « Tu as bien répondu. Fais ceci, et tu vivras. »
Yesu akawaambia, “Vema! Fanya hivyo, nawe utaishi.”
29 Mais lui, voulant se justifier, demanda à Jésus: « Qui est mon prochain? »
Lakini yeye akitaka kujihakikishia kuwa mwema akamwuliza Yesu, “Na jirani yangu ni nani?”
30 Jésus répondit: « Un homme descendait de Jérusalem à Jéricho. Il tomba au milieu de brigands qui le dépouillèrent, le battirent, puis s'en allèrent, le laissant à demi mort.
Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anashuka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko. Alipokuwa njiani, alivamiwa na majambazi, wakamnyang'anya mali yake na kumpiga, wakamwacha amelala pale nusu mfu.
31 Par hasard, un prêtre descendait par là. Il le vit et passa de l'autre côté.
Kumbe, kuhani mmoja akawa anapita barabara ileile, akamwona, akapita kando.
32 De même, un lévite, qui était arrivé à cet endroit et l'avait vu, passa de l'autre côté.
Hali kadhalika na Mlawi mmoja, alipofika mahali akamwona, akapita kando.
33 Mais un Samaritain, qui était en voyage, arriva là où il était. Quand il le vit, il fut ému de compassion,
Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa anasafiri, alifika pale yule mtu alipokuwa, naye alipomwona, alimwonea huruma.
34 s'approcha de lui, pansa ses plaies, et versa de l'huile et du vin. Il le fit monter sur sa propre bête, le conduisit dans une auberge, et prit soin de lui.
Akamwendea, akamtibu majeraha yake kwa kumtia mafuta na divai; na kuyafunga halafu akampandisha juu ya punda wake akampeleka katika nyumba moja ya wageni akamuuguza.
35 Le lendemain, en partant, il prit deux deniers, les donna à l'hôte, et lui dit: « Prends soin de lui. Tout ce que tu dépenseras au-delà, je te le rendrai à mon retour ».
Kesho yake akatoa fedha dinari mbili akampa yule mwenye nyumba, akamwambia, Muuguze mtu huyu; na chochote utakachotumia zaidi, nitakulipa nitakaporudi.”
36 Maintenant, lequel de ces trois vous semble être le prochain de celui qui est tombé au milieu des brigands? »
Kisha Yesu akauliza, “Kati ya hao watatu, ni yupi aliyeonyesha kuwa jirani yake yule aliyevamiwa na majambazi?”
37 Il a dit: « Celui qui a eu pitié de lui. » Alors Jésus lui dit: « Va et fais de même. »
Yule mwalimu wa Sheria akamjibu, “Ni yule aliyemwonea huruma.” Yesu akamwambia, “Nenda ukafanye vivyo hivyo.”
38 Comme ils continuaient leur chemin, il entra dans un village, et une femme, nommée Marthe, le reçut dans sa maison.
Walipokuwa safarini, waliingia katika kijiji kimoja na mwanamke mmoja, aitwaye Martha, alimkaribisha nyumbani kwake.
39 Elle avait une sœur, nommée Marie, qui était aussi assise aux pieds de Jésus et écoutait sa parole.
Martha alikuwa na dada yake aitwaye Maria; huyu aliketi karibu na Yesu akisikiliza mafundisho yake.
40 Mais Marthe, distraite par le service, s'approcha de Jésus et lui dit: « Seigneur, ne te soucie-tu pas que ma sœur m'ait laissée seule à servir? Demande-lui donc de m'aider. »
Lakini Martha alikuwa anashughulika na mambo mengi. Basi, akamwendea Yesu, akamwambia, “Bwana, hivi hujali kwamba dada yangu ameniacha nishughulike peke yangu? Mwambie basi, anisaidie.”
41 Jésus lui répondit: « Marthe, Marthe, tu es inquiète et troublée par beaucoup de choses,
Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, unahangaika na kusumbuka kwa mambo mengi.
42 mais une seule chose est nécessaire. Marie a choisi la bonne part, qui ne lui sera pas enlevée. »
Kitu kimoja tu ni muhimu. Maria amechagua kitu bora zaidi ambacho hakuna mtu atakayemnyag'anya.”

< Luc 10 >