< 1 Aikakirja 9 >

1 Ja koko Israel luettiin polviluvun jälkeen, ja katso, he ovat kirjoitetut Israelin kuningasten kirjaan; ja Juuda vietiin Babeliin pahain tekoinsa tähden.
Waisraeli wote waliorodheshwa katika koo zilizoandikwa kwenye kitabu cha wafalme wa Israeli. Watu wa Yuda walichukuliwa mateka kwenda Babeli kwa sababu ya kukosa uaminifu kwa Mungu.
2 Mutta ne ensimäiset asujamet, jotka tulivat perintöönsä ja kaupunkeihinsa, olivat Israel, papit, Leviläiset ja Netinimit.
Basi watu wa kwanza kurudi kukaa kwenye milki zao katika miji yao walikuwa baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi na watumishi wa Hekalu.
3 Ja silloin asuivat Jerusalemissa Juudan lapsista, Benjaminin lapsista, ja Ephraimin ja Manassen lapsista:
Wale waliotoka Yuda, Benyamini, Efraimu na Manase ambao waliishi Yerusalemu walikuwa:
4 Utal Ammihudin poika, Omrin pojan, Imrin pojan, Banin pojan, Peretsin Juudan pojan lapsista.
Uthai mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imri, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.
5 Mutta Silonilaisista Asaja ensimäinen poika, ja hänen poikansa.
Wazao wa Washiloni waliorudi ni: Asaya mzaliwa wa kwanza na wanawe.
6 Seran lapsista, Jeguel veljinensä; kuusisataa ja yhdeksänkymmentä.
Kwa wana wa Zera: Yeueli. Watu wa Yuda jumla yao walikuwa watu 690.
7 Benjaminin lapsista, Sallu Mesullamin poika, Hodavian pojan, Hassenuan pojan,
Kwa Benyamini walikuwa: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Hodavia, mwana wa Hasenua;
8 Ja Jibneja Jerohamin poika, ja Ela Ussin poika, Mikrin pojan, ja Mesullam Sephatian poika, Reguelin pojan, Jibnejan pojan;
Ibneya mwana wa Yerohamu, Ela mwana wa Uzi, mwana wa Mikri; na Meshulamu mwana wa Shefatia, mwana wa Reueli, mwana wa Ibniya.
9 Niin myös heidän veljensä sukukuntainsa jälkeen yhdeksänsataa ja kuusikuudettakymmentä: nämät kaikki ovat olleet isäin päämiehet heidän isäinsä huoneessa.
Watu kutoka Benyamini kama walivyoorodheshwa katika koo zao jumla yao ni 956. Watu hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao.
10 Papeista: Jedaja, Jojarib ja Jakin,
Wa jamaa za makuhani walikuwa: Yedaya, Yehoyaribu na Yakini;
11 Ja Asaria Hilkian poika, Mesullamin pojan, Zadokin pojan, Merajotin pojan, Ahitobin pojan, Jumalan huoneen päämies,
Azaria mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu aliyekuwa afisa kiongozi wa nyumba ya Mungu.
12 Ja Adaja Jerohamin poika, Pashurin pojan, Malkian pojan, ja myös Maesai Adielin poika, Jahseran pojan, Mesullamin pojan. Mesillemitin pojan, Immerin pojan;
Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya; Maasai, mwana wa Adieli, mwana wa Yahzera, mwana wa Meshulamu, mwana wa Meshilemithi, mwana wa Imeri.
13 Niin myös heidän veljeinsä päämiehet isäinsä huoneessa, tuhannen seitsemänsataa ja kuusikymmentä väkevää miestä, toimittamaan viran menoja Jumalan huoneessa.
Makuhani waliokuwa viongozi wa jamaa zao walikuwa 1,760. Walikuwa watu wenye uwezo, waliowajibika kuhudumu katika nyumba ya Mungu.
14 Mutta Leviläisistä, jotka olivat Merarin lapsia, Semaja Hassubin poika, Asrikamin pojan, Hasabian pojan;
Jamaa za Walawi walikuwa: Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, wa wana wa Merari.
15 Ja Bakbakkar, Heres, ja Galal, ja Mattania Miikan poika, Sikrin pojan, Asaphin pojan;
Bakbakari, Hereshi, Galali na Matania mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu.
16 Ja Obadia Semajan poika, Galalin pojan, Jedutunin pojan, ja Berekia Asan poika, Elkanan pojan, joka asui Netophatilaisten kylissä.
Obadia mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni. Berekia mwana wa Asa, mwana wa Elikana, ambao waliishi katika vijiji vya Wanetofathi.
17 Ja ovenvartiat olivat Sallum, Akkub, Talmon, Ahiman ja heidän veljensä: Sallum oli ylimmäinen.
Mabawabu katika Hekalu la Bwana waliorudi walikuwa: Shalumu, Akubu, Talmoni, Ahimani na ndugu zao. Shalumu alikuwa mlinzi wao mkuu.
18 Sillä he olivat tähän saakka vartioineet itäisellä puolella kuninkaan porttia: ne olivat ovenvartiat Levin poikain seassa.
Walikuwa wamewekwa katika lango la mfalme lililokuwa upande wa mashariki, mpaka wakati huu. Hawa walikuwa mabawabu wa kutoka kwenye kambi ya Walawi.
19 Ja Sallum Koren poika Ebjasaphin pojan, Koran pojan ja hänen veljensä hänen isänsä huoneesta, ne Korhilaiset, heidän virkansa menoissa, vartioitsemaan seurakunnan majan ovipieleen; ja heidän isänsä pitää vartioitseman Herran leirissä sisällekäymistä.
Shalumu mwana wa Kore, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora, pamoja na mabawabu wenzake kutoka jamaa yake ya Kora waliwajibika kulinda malango ya Hema, kama vile baba zao walivyokuwa wamewajibika kulinda ingilio la Maskani ya Bwana.
20 Mutta Pinehas Eleasarin poika oli ennen ollut heidän päämiehensä; sillä Herra oli hänen kanssansa.
Hapo zamani Finehasi mwana wa Eleazari alikuwa kiongozi wa mabawabu, naye Bwana alikuwa pamoja naye:
21 Ja Sakaria Meselemian poika oli vartia seurakunnan majan ovella.
Zekaria mwana wa Meshelemia alikuwa bawabu katika ingilio la Hema la Kukutania.
22 Kaikki nämät olivat valitut ovea vartioitsemaan, kaksisataa ja kaksitoistakymmentä, jotka olivat luetut polviluvun jälkeen heidän kylissänsä. Ja David ja Samuel, näkiä, asettivat heitä virkaan heidän uskollisuudessansa,
Jumla ya waliochaguliwa kuwa mabawabu katika sakafu za kupuria nafaka walikuwa watu 212. Waliandikishwa kwa koo zao kwenye vijiji vyao. Mabawabu hawa waliwekwa katika nafasi zao za kuaminiwa na Daudi pamoja na mwonaji Samweli.
23 Niin että he ja heidän lapsensa ottivat Herran huoneesta vaarin, seurakunnan majan huoneesta, että he sitä vartioitsivat.
Wao na wazao wao walikuwa viongozi wa kulinda malango ya nyumba ya Bwana, nyumba iliyoitwa Hema.
24 Ja ovenvartiat olivat asetetut neljää ilmaa kohden: itään, länteen, pohjaan ja etelään päin.
Mabawabu walikuwa pande zote nne: mashariki, magharibi, kaskazini na kusini.
25 Mutta heidän veljensä olivat maakylissänsä, niin kuitenkin, että heidän piti tuleman sisälle seitsemäntenä päivänä, ja ajasta niin aikaan heidän tykönänsä oleman.
Ndugu zao katika vijiji vyao walikuwa wakija mara kwa mara na kuwasaidia katika kazi zao kwa vipindi mbalimbali vya siku saba.
26 Sillä Leviläiset olivat uskotut olemaan neljäksi ylimmäiseksi ovenvartiaksi; ja he olivat myös kätkyin ja Herran huoneen tavarain päällä.
Lakini mabawabu wanne wakuu, waliokuwa Walawi, walikabidhiwa wajibu kwa ajili ya vyumba na hazina katika nyumba ya Mungu.
27 Ja he olivat yötä Jumalan huoneen ympärillä; sillä heidän piti sitä vartioitseman, ja avajaman joka aamu.
Walikesha mahali walipowekwa kuizunguka nyumba ya Mungu, kwa sababu iliwapasa kuilinda. Pia walitunza funguo kwa ajili ya kufungua mlango kila siku asubuhi.
28 Ja muutamat olivat heistä viran asetten päällä; sillä heidän piti ne kantaman ulos ja sisälle luvun jälkeen.
Baadhi yao walikuwa viongozi wa kutunza vifaa vilivyotumika katika huduma ndani ya Hekalu; walivihesabu kila vilipoingizwa ndani na kila vilipotolewa.
29 Ja muutamat heistä olivat asetetut astiain ja pyhäin kaluin päälle, sämpyläjauhoin, viinan, öljyn, pyhän savun ja myös yrttein päälle.
Wengine walipangiwa kutunza mapambo na vifaa vingine vya patakatifu, pamoja na unga, divai, mafuta, uvumba na vikolezo.
30 Mutta muutamat pappein lapsista tekivät hyvin valmistettuja voiteita.
Lakini baadhi ya makuhani walifanya kazi ya kuchanganya vikolezo.
31 Ja Mattitjalle Leviläisistä, Sallumin Korhilaisten ensimäiselle pojalle oli uskottu mitä pannuissa valmistettiin.
Mlawi aliyeitwa Matithia, mwana mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, wa ukoo wa Kora, alikabidhiwa wajibu kwa ajili ya kuoka mikate ya sadaka.
32 Ja Kahatilaisista heidän veljistänsä olivat asetetut katsomusleipäin yli, että he niitä valmistaisivat joka sabbattina.
Baadhi ya ndugu zao wa ukoo wa Kohathi walikuwa viongozi wa kuandaa mikate ya Wonyesho kwa ajili ya kila Sabato, mikate iliyokuwa inawekwa mezani.
33 Nämät ovat veisaajat, Leviläisten isäin päämiehet vapaat heidän kammioissansa; sillä he olivat siellä askareissansa päivää ja yötä.
Wale waliokuwa waimbaji, viongozi wa jamaa za Walawi, waliishi katika vyumba vya Hekalu, nao hawakufanya shughuli nyingine yoyote kwa sababu iliwapasa kuwajibika kwa kazi hiyo usiku na mchana.
34 Nämät olivat ylimmäiset Leviläisten isät, päämiehet sukukunnissansa; he asuivat Jerusalemissa.
Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa za Walawi, wakuu kama walivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.
35 Jegil Gibeonin isä asui Gibeonissa; hänen emäntänsä nimi oli Maeka,
Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka,
36 Ja hänen ensimäinen poikansa Abdon, Zur, Kis, Baal, Ner ja Nadab,
mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
37 Gedor, Ahio, Sakaria ja Miklot.
Gedori, Ahio, Zekaria na Miklothi.
38 Mutta Miklot siitti Simeamin; jotka myös asuivat veljeinsä kohdalla, veljinensä Jerusalemissa.
Miklothi akamzaa Shimeamu. Wao pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.
39 Ja Ner siitti Kisin; Kis siitti Saulin; Saul siitti Jonatanin, Malkisuan, Abinadabin, Esbaalin.
Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli. Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.
40 Ja Meribbaal oli Jonatanin poika; ja Meribbaal siitti Miikan.
Yonathani akamzaa Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.
41 Miikan pojat olivat Piton, Melek ja Tahrea.
Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea, na Ahazi.
42 Ahas siitti Jaeran; Jaera siitti Alemetin, Asmavetin ja Simrin; Simri siitti Motsan.
Ahazi akamzaa Yara, Yara akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.
43 Motsa siitti Binejan; ja Rephaja oli hänen poikansa, Eleasa hänen poikansa, Atsel hänen poikansa.
Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Refaya, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.
44 Ja Atselilla oli kuusi poikaa, ja nämät olivat heidän nimensä: Asrikam, Bokru, Ismael, Searia, Obadia ja Hanan: ne olivat Atselin pojat.
Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Aseli.

< 1 Aikakirja 9 >