< Luke 5 >

1 And it came to pass, in the multitude pressing on him to hear the word of God, that he was standing beside the lake of Gennesaret,
Basi ilitokea wakati watu walipomkusanyikia na kumzunguka Yesu na kusikiliza neno la Mungu, ambapo alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti.
2 and he saw two boats standing beside the lake, and the fishers, having gone away from them, were washing the nets,
Aliona mashua mbili zimetia nanga pembeni mwa ziwa. Wavuvi walikuwa wametoka na walikuwa wakiosha nyavu zao.
3 and having entered into one of the boats, that was Simon's, he asked him to put back a little from the land, and having sat down, was teaching the multitudes out of the boat.
Yesu akaingia katika mojawapo ya zile mashua, ambayo ilikuwa ya Simoni na kumwomba aipeleke majini mbali kidogo na nchi kavu. Kisha akakaa na kufundisha kutokea kwenye mashua.
4 And when he left off speaking, he said unto Simon, 'Put back to the deep, and let down your nets for a draught;'
kuongea, akamwambia Simoni, “Ipeleke mashua yako mpaka kwenye kilindi cha maji nakushusha nyavu zako ili kuvua samaki.”
5 and Simon answering said to him, 'Master, through the whole night, having laboured, we have taken nothing, but at thy saying I will let down the net.'
Simon akajibu na kusema, Bwana, tumefanya kazi usiku wote, na hatukukamata chochote, lakini kwa neno lako, nitazishusha nyavu.
6 And having done this, they enclosed a great multitude of fishes, and their net was breaking,
Walipofanya hivyo walikusanya kiasi kikubwa cha samaki na nyavu zao zikaanza kukatika.
7 and they beckoned to the partners, who [are] in the other boat, having come, to help them; and they came, and filled both the boats, so that they were sinking.
Hivyo wakawaashiria washirika wao kwenye mashua nyingine ili waja na kuwasaidia. Walikuja wakazijaza mashua zote, kiasi kwamba zikaanza kuzama.
8 And Simon Peter having seen, fell down at the knees of Jesus, saying, 'Depart from me, because I am a sinful man, O lord;'
Lakini Simoni Petro, alipoona hivyo, alianguka magotini pa Yesu akisema,”Ondoka kwangu, kwa sababu mimi ni mtu mwenye dhambi Bwana.”
9 for astonishment seized him, and all those with him, at the draught of the fishes that they took,
Kwa sababu alishangazwa, na wote waliokuwa pamoja naye, kwa uvuvi wa samaki waliokuwa wameufanya.
10 and in like manner also James and John, sons of Zebedee, who were partners with Simon; and Jesus said unto Simon, 'Fear not, henceforth thou shalt be catching men;'
Hili liliwajumuisha Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo, ambao walikuwa washirika wa Simoni. Na Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, kwa sababu kuanzia sasa na kuendelea utavua watu.”
11 and they, having brought the boats upon the land, having left all, did follow him.
Walipokwishazileta mashua zao nchi kavu, waliacha kila kitu na kumfuata yeye.
12 And it came to pass, in his being in one of the cities, that lo, a man full of leprosy, and having seen Jesus, having fallen on [his] face, he besought him, saying, 'Sir, if thou mayest will, thou art able to cleanse me;'
Ilitokea kwamba alipokuwa katika mji mmojawapo, mtu aliyekuwa amejaa ukoma alikuwa huko. Wakati alipomuona Yesu, alianguka akiinamisha uso kwake mpaka chini na kumuomba, akisema, “Bwana, ikiwa unataka, waweza kunitakasa.”
13 and having stretched forth [his] hand, he touched him, having said, 'I will; be thou cleansed;' and immediately the leprosy went away from him.
Kisha Yesu alinyoosha mkono wake na kumgusa, akisema, “Nataka. Takasika.” Na saa ileile ukoma ukamwacha.
14 And he charged him to tell no one, 'But, having gone away, shew thyself to the priest, and bring near for thy cleansing according as Moses directed, for a testimony to them;'
“Alimwagiza asimwambie mtu yeyote, lakini alimwambia, “Nenda zako, na ukajionyeshe kwa makuhani na utoe sadaka ya utakaso wako, sawasawa na kile Musa alichokiamuru, kwa ushuhuda kwao.”
15 but the more was the report going abroad concerning him, and great multitudes were coming together to hear, and to be healed by him of their infirmities,
Lakini habari kumuhusu yeye zikaenea mbali zaidi, na umati mkubwa wa watu ukaja pamoja kumsikiliza akifundisha na kuponywa magonjwa yao.
16 and he was withdrawing himself in the desert places and was praying.
Lakini mara kwa mara alijitenga faraghani na kuomba.
17 And it came to pass, on one of the days, that he was teaching, and there were sitting by Pharisees and teachers of the Law, who were come out of every village of Galilee, and Judea, and Jerusalem, and the power of the Lord was — to heal them.
Ilitokea siku moja kati ya hizo siku alikuwa akifundisha, na walikuwapo Mafarisayo na waalimu wa sheria wamekaa hapo ambao walikuja wakitokea vijiji vingi tofauti katika mkoa wa Galilaya na Yudea, na pia kutokea katika mji wa Yerusalemu. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kuponya.
18 And lo, men bearing upon a couch a man, who hath been struck with palsy, and they were seeking to bring him in, and to place before him,
watu kadhaa walikuja, wamembeba kwenye mkeka mtu aliyepooza, na wakatafuta njia ya kumwingiza ndani ili kumlaza chini mbele ya Yesu.
19 and not having found by what way they may bring him in because of the multitude, having gone up on the house-top, through the tiles they let him down, with the little couch, into the midst before Jesus,
Hawakupata njia ya kumwingiza ndani kwa sababu ya umati, hivyo walipanda juu ya paa la nyumba na kumshusha yule mtu chini kupitia kwenye vigae, juu mkeka wake katikati ya watu, mbele kabisa ya Yesu.
20 and he having seen their faith, said to him, 'Man, thy sins have been forgiven thee.'
Akiangalia imani yao, Yesu alisema, “Rafiki, dhambi zako umesamehewa.”
21 And the scribes and the Pharisees began to reason, saying, 'Who is this that doth speak evil words? who is able to forgive sins, except God only?'
Waandishi na Mafarisayo waliaanza kuhoji hilo, wakisema, “Huyu ni nani anayeongea makufuru? Ni nani anaweza kusamehe dhambi ila Mungu pekee yake?”
22 And Jesus having known their reasonings, answering, said unto them, 'What reason ye in your hearts?
Lakini Yesu, akitambua nini walichokuwa wakifikiri, aliwajibu na kuwaambia, “Kwa nini mnaulizana hili mioyoni mwenu?
23 which is easier — to say, Thy sins have been forgiven thee? or to say, Arise, and walk?
Kipi ni rahisi kusema, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama utembee?'
24 'And that ye may know that the Son of Man hath authority upon the earth to forgive sins — (he said to the one struck with palsy) — I say to thee, Arise, and having taken up thy little couch, be going on to thy house.'
Lakini mjue ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani ya kusamehe dhambi, Nakwambia wewe, 'Amka, chukua mkeka wako na uende nyumbani kwako.'”
25 And presently having risen before them, having taken up [that] on which he was lying, he went away to his house, glorifying God,
Wakati huo huo akaamka mbele yao na akachukua mkeka wake aliokuwa ameulalia. Kisha akariudi nyumbani kwake akimtukuza Mungu.
26 and astonishment took all, and they were glorifying God, and were filled with fear, saying — 'We saw strange things to-day.'
Kila mmoja alishangazwa na wakamtukuza Mungu. Walijawa na hofu, wakisema, “Tumeona mambo yasiyo ya kawaida leo.”
27 And after these things he went forth, and beheld a tax-gatherer, by name Levi, sitting at the tax-office, and said to him, 'Be following me;'
Baada ya mambo haya kutokea, Yesu alitoka huko na akamwona mtoza ushuru aliyeitwa Lawi amekaa eneo la kukusanyia kodi. Akamwambia, “Nifuate.”
28 and he, having left all, having arisen, did follow him.
Hivyo Lawi akanyanyuka na kumfuata, akiacha kila kitu nyuma.
29 And Levi made a great entertainment to him in his house, and there was a great multitude of tax-gatherers and others who were with them reclining (at meat),
Kisha Lawi akaandaa nyumbani kwake karamu kubwa kwa ajili ya Yesu. Walikuwapo watozaushuru wengi kule na watu wengi walioketi mezani wakila pamoja nao.
30 and the scribes and the Pharisees among them were murmuring at his disciples, saying, 'Wherefore with tax-gatherers and sinners do ye eat and drink?'
Lakini Mafarisayo na waandishi wao walikuwa wakiwanung'unikia wanafunzi, wakisema, “Kwa nini mnakula na kunywa na watoza ushuru pamoja na watu wengine wenye dhambi?”
31 And Jesus answering said unto them, 'They who are well have no need of a physician, but they that are ill:
Yesu akawajibu, “Watu walio katika afya njema hawahitaji tabibu, ni wale tu wanaoumwa ndiyo watakao mhitaji mmoja.
32 I came not to call righteous men, but sinners, to reformation.'
Sikuja kuwaita watu wenye haki haki wapate kutubu, bali kuwaita wenye dhambi wapate kutubu.”
33 And they said unto him, 'Wherefore do the disciples of John fast often, and make supplications — in like manner also those of the Pharisees — but thine do eat and drink?'
Wakamwambia, “Wanafunzi wa Yohana mara nyingi hufunga na kuomba, na wanafunzi wa Mafarisayo nao hufanya vivyo hivyo. Lakini wanafunzi wako hula na kunywa.”
34 And he said unto them, 'Are ye able to make the sons of the bride-chamber — in the bridegroom being with them — to fast?
Yesu akawaambia, “Inawezekana mtu yeyote akawafanya waliohudhuria harusi ya Bwana Arusi kufunga wakati Bwana Arusi bado yu pamoja nao?
35 but days will come, and, when the bridegroom may be taken away from them, then they shall fast in those days.'
Lakini siku zitakuja wakati Bwana Arusi atakapoondolewa kwao, ndipo katika siku hizo watafunga.”
36 And he spake also a simile unto them — 'No one a patch of new clothing doth put on old clothing, and if otherwise, the new also doth make a rent, and with the old the patch doth not agree, that [is] from the new.
Kisha Yesu aliongea pia kwao kwa mfano. “Hakuna anayechana kipande cha nguo kutoka kwenye vazi jipya na kukitumia kurekebisha vazi la zamani. Kama akifanya hivyo, ataichana nguo mpya, na kipande cha nguo kutoka vazi jipya kisengefaa kutumika na nguo ya vazi la zamani.
37 'And no one doth put new wine into old skins, and if otherwise, the new wine will burst the skins, and itself will be poured out, and the skins will be destroyed;
pia, hakuna mtu ambaye huweka divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai mpya ingepasua kile chombo, na divai ingemwagika, na viriba vingeharibika.
38 but new wine into new skins is to be put, and both are preserved together;
Lakini divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
39 and no one having drunk old [wine], doth immediately wish new, for he saith, The old is better.'
Na hakuna mtu baada ya kunywa divai ya zamani, hutataka mpya, kwa sababu husema, 'Ya zamani ni bora.”'

< Luke 5 >