< Luke 3 >

1 And in the fifteenth year of the government of Tiberius Caesar — Pontius Pilate being governor of Judea, and Herod tetrarch of Galilee, and Philip his brother, tetrarch of Ituraea and of the region of Trachonitis, and Lysanias tetrarch of Abilene —
Sasa, katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberia, wakati Pontio Pilato alikuwa gavana wa Uyahudi, Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo ndugu yake alikuwa mkuu wa mkoa wa Iturea na Trakoniti, na Lisania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
2 Annas and Caiaphas being chief priests — there came a word of God unto John the son of Zacharias, in the wilderness,
na wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, Neno la Mungu lilimjia Yohana mwana wa Zakaria, jangwani.
3 and he came to all the region round the Jordan, proclaiming a baptism of reformation — to remission of sins,
Alisafiri katika mkoa wote kuzunguka Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi
4 as it hath been written in the scroll of the words of Isaiah the prophet, saying, 'A voice of one crying in the wilderness, Prepare ye the way of the Lord, straight make ye His paths;
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha maneno ya Isaya nabii, “sauti ya mtu aliaye nyikani, “Itengenezeni tayari njia ya Bwana, yatengenezeni mapito yake yaliyoonyoka.
5 every valley shall be filled, and every mountain and hill shall be made low, and the crooked shall become straightness, and the rough become smooth ways;
Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa, barabara zilizopinda zitanyoshwa, na njia zilizoparaza zitalainishwa.
6 and all flesh shall see the salvation of God.'
Watu wote watauona wokovu wa Mungu.”
7 Then said he to the multitudes coming forth to be baptised by him, 'Brood of vipers! who did prompt you to flee from the coming wrath?
Hivyo, Yohana akawaambia makutano makubwa ya watu waliomjia wapate kubatizwa na yeye, “Ninyi uzao wa nyoka wenye sumu, nani aliwaonya kuikimbia gadhabu inayokuja?
8 make, therefore, fruits worthy of the reformation, and begin not to say within yourselves, We have a father — Abraham; for I say to you, that God is able out of these stones to raise children to Abraham;
Zaeni matunda yanayoedana na toba, na msianze kusema ndani yenu, “Tunaye Ibarahimu ambaye ni baba yetu; kwa sababu nawaambia ya kwamba, Mungu anaweza kumwinulia Ibrahimu watoto hata kutokana na mawe haya.
9 and already also the axe unto the root of the trees is laid, every tree, therefore, not making good fruit is cut down, and to fire it is cast.'
Tayari shoka limeshawekwa kwenye mzizi wa miti. Hivyo, kila mti usiozaa matunda mema, hukatwa na kutupwa motoni.
10 And the multitudes were questioning him, saying, 'What, then, shall we do?'
Kisha watu katika makutano walimuuliza wakisema, “Sasa tunatakiwa tufanyeje?”
11 and he answering saith to them, 'He having two coats — let him impart to him having none, and he having victuals — in like manner let him do.'
Alijibu na kuwaambia, “kama mtu ana kanzu mbili anatakiwa atoe kanzu moja kwa mwingine ambaye hana kabisa, na ambaye ana chakula na afanye vivyo hivyo.”
12 And there came also tax-gatherers to be baptised, and they said unto him, 'Teacher, what shall we do?'
Kisha baadhi ya watoza ushuru walikuja pia kubatizwa, na wakamwambia, “Mwalimu, tunatakiwa kufanya nini?
13 and he said unto them, 'Exact no more than that directed you.'
Akawaambia, “Msikusanye fedha zaidi kuliko mnachotakiwa kukusanya.”
14 And questioning him also were those warring, saying, 'And we, what shall we do?' and he said unto them, 'Do violence to no one, nor accuse falsely, and be content with your wages.'
Baadhi ya maaskari pia wakamuuliza wakisema, “Na sisi je? Tunatakiwa tufanye nini?” Akawambia, “Msichukue fedha kwa mtu yeyote kwa nguvu, na msimtuhumu mtu yeyote kwa uongo. Ridhikeni na mishahara yenu.”
15 And the people are looking forward, and all are reasoning in their hearts concerning John, whether or not he may be the Christ;
Sasa, kwa kuwa watu walikuwa na shauku ya kumngojea Kristo atakaye kuja, kila mmoja alikuwa anawaza moyoni mwake kuhusu Yohana kama yeye ndiye Kristo.
16 John answered, saying to all, 'I indeed with water do baptise you, but he cometh who is mightier than I, of whom I am not worthy to loose the latchet of his sandals — he shall baptise you with the Holy Spirit and with fire;
Yohana akajibu kwa kuwaambia wote, “Mimi nawabatiza ninyi kwa maji, lakini kuna mmoja ajaye ambaye ana nguvu kuliko mimi, na sisitahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Atawabatiza ninyi kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 whose winnowing shovel [is] in his hand, and he will thoroughly cleanse his floor, and will gather the wheat to his storehouse, and the chaff he will burn with fire unquenchable.'
Pepeto lake liko mkononi mwake ili kusafisha vizuri uwanda wake wa kupepetea ngano na kuikusanya ngano ghalani mwake. Lakini, atayateketeza makapi kwa moto ambao hauwezi kuzimika.
18 And, therefore, indeed with many other things, exhorting, he was proclaiming good news to the people,
Kwa maonyo mengine mengi pia, alihubiri habari njema kwa watu.
19 and Herod the tetrarch, being reproved by him concerning Herodias the wife of Philip his brother, and concerning all the evils that Herod did,
Yohana alimkemea pia Herode mkuu wa mkoa kwa kumuoa Herodia, mke wa ndugu yake na kwa maovu mengine mengi ambayo Herode alikuwa ameyatenda.
20 added also this to all, that he shut up John in the prison.
Lakini baadaye Herode alifanya uovu mwingine mbaya sana. Alimfunga Yohana gerezani.
21 And it came to pass, in all the people being baptised, Jesus also being baptised, and praying, the heaven was opened,
Kisha ilitokea kwamba, wakati watu wote walipokuwa wakibatizwa na Yohana, naye Yesu alibatizwa pia. Wakati alipokuwa akiomba, mbingu zikafunguka.
22 and the Holy Spirit came down in a bodily appearance, as if a dove, upon him, and a voice came out of heaven, saying, 'Thou art My Son — the Beloved, in thee I did delight.'
Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili kama njiwa, wakati huo huo sauti ikaja kutoka mbinguni ikisema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa sana na wewe.”
23 And Jesus himself was beginning to be about thirty years of age, being, as was supposed, son of Joseph,
Sasa Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa na umri upatao miaka thelathini. Alikuwa ni mwana (kama ilivyotadhaniwa) wa Yusufu, mwana wa Eli,
24 the [son] of Eli, the [son] of Matthat, the [son] of Levi, the [son] of Melchi, the [son] of Janna, the [son] of Joseph,
mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yana, mwana wa Yusufu,
25 the [son] of Mattathias, the [son] of Amos, the [son] of Naum, the [son] of Esli,
mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Esli, mwana wa Nagai,
26 the [son] of Naggai, the [son] of Maath, the [son] of Mattathias, the [son] of Semei, the [son] of Joseph, the [son] of Juda,
mwana wa Maati, mwana wa Matathia, mwana wa Semeini, mwana wa Yusufu, mwana wa Yuda,
27 the [son] of Joanna, the [son] of Rhesa, the [son] of Zerubbabel, the [son] of Shealtiel,
mwana wa Yoanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
28 the [son] of Neri, the [son] of Melchi, the [son] of Addi, the [son] of Cosam, the [son] of Elmodam, the [son] of Er,
mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
29 the [son] of Jose, the [son] of Eliezer, the [son] of Jorim, the [son] of Matthat,
mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Matathi, mwana wa Lawi,
30 the [son] of Levi, the [son] of Simeon, the [son] of Juda, the [son] of Joseph, the [son] of Jonan, the [son] of Eliakim,
mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yusufu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliyakimu,
31 the [son] of Melea, the [son] of Mainan, the [son] of Mattatha, the [son] of Nathan,
mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
32 the [son] of David, the [son] of Jesse, the [son] of Obed, the [son] of Booz, the [son] of Salmon, the [son] of Nahshon,
mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
33 the [son] of Amminadab, the [son] of Aram, the [son] of Esrom, the [son] of Pharez,
mwana wa Abinadabu, mwana wa Aramu, mwana wa Hesroni, mwana wa Peresi, mwana wa Yuda,
34 the [son] of Judah, the [son] of Jacob, the [son] of Isaac, the [son] of Abraham, the [son] of Terah, the [son] of Nahor,
mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Ibrahimu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
35 the [son] of Serug, the [son] of Reu, the [son] of Peleg, the [son] of Eber,
mwana wa Seruig, mwana wa Ragau, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
36 the [son] of Salah, the [son] of Cainan, the [son] of Arphaxad, the [son] of Shem, the [son] of Noah, the [son] of Lamech,
mwana wa Kenani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Nuhu, mwana wa Lameki,
37 the [son] of Methuselah, the [son] of Enoch, the [son] of Jared, the [son] of Mahalaleel,
mwana wa Methusela, mwana wa Henoko, mwana wa Yaredi, mwana Mahalalei, mwana wa Kenani,
38 the [son] of Cainan, the [son] of Enos, the [son] of Seth, the [son] of Adam, the [son] of God.
mwana wa Enoshi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, mwana wa Mungu.

< Luke 3 >