< Joshua 1 >

1 And it cometh to pass after the death of Moses, servant of Jehovah, that Jehovah speaketh unto Joshua son of Nun, minister of Moses, saying,
Sasa ilitokea baada ya kufa kwa Musa, mtumishi wa Yahweh, Yahweh alimwambia Yoshua, mwana wa Nuni, msaidizi mkuu wa Musa, kusema,
2 'Moses my servant is dead, and now, rise, pass over this Jordan, thou, and all this people, unto the land which I am giving to them, to the sons of Israel.
“Musa, mtumishi wangu amekufa. Sasa basi inuka, vuka mto huu wa Yordani, wewe na watu hawa wote, kuingia katika nchi ambayo ninawapa - watu waisraeli.
3 'Every place on which the sole of your foot treadeth, to you I have given it, as I have spoken unto Moses.
Nimewapa ninyi kila sehemu ambapo nyayo za miguu yenu itakanyaga. Nimewapa ninyi, kama nilivyomwahidi Musa.
4 From this wilderness and Lebanon, and unto the great river, the river Phrath, all the land of the Hittites, and unto the great Sea — the going in of the sun — is your border.
kuanzia jangwani na Lebanoni, hadi mto mkubwa wa Frati, nchi yote ya Wahiti, na hata Bahari kuu, ambako jua huzama, itakuwa nchi yenu.
5 'No man doth station himself before thee all days of thy life; as I have been with Moses, I am with thee, I do not fail thee, nor forsake thee;
Hakuna mtu awaye yote atakayeweza kusimama kinyume chako siku zote za maisha yako. Nitakuwa pamoja nawe kama nilivyokuwa na Musa. Sitakupungukia wala kukuacha.
6 be strong and courageous, for thou — thou dost cause this people to inherit the land which I have sworn to their fathers to give to them.
Uwe hodari na jasiri. Wewe utawafanya watu hawa wairithi nchi ambayo niliwaahidi baba zao kuwa ningewapa.
7 'Only, be strong and very courageous, to observe to do according to all the law which Moses My servant commanded thee; thou dost not turn aside from it right or left, so that thou dost act wisely in every [place] whither thou goest;
Uwe hodari na jasiri sana. uwe makini kutii sheria zote ambazo Musa mtumishi wangu alikuagiza. Usikengeuke upande wa kulia au wa kushoto, ili uweze kufanikiwa kila mahali utakapoenda.
8 the book of this law doth not depart out of thy mouth, and thou hast meditated in it by day and by night, so that thou dost observe to do according to all that is written in it, for then thou dost cause thy way to prosper, and then thou dost act wisely.
Siku zote uuongee juu ya kitabu hiki cha sheria. Utakitafakari mchana na usiku ili kwamba uweze kutii yote yaliyoandikwa humo. Kisha utastawi na kufanikiwa.
9 'Have not I commanded thee? be strong and courageous; be not terrified nor affrighted, for with thee [is] Jehovah thy God in every [place] whither thou goest.'
Je si mimi niliyekuagiza? Uwe hadori na jasiri! Usiogope. Usivunjike moyo. Yahweh Mungu wako yuko pamoja nawe kila uendeko.
10 And Joshua commandeth the authorities of the people, saying,
Kisha Yoshua akawaagiza viongozi wa watu,
11 'Pass over into the midst of the camp, and command the people, saying, Prepare for yourselves provision, for within three days ye are passing over this Jordan, to go in to possess the land which Jehovah your God is giving to you to possess it.'
“Nendeni katika kambi na waagizeni watu, 'andaeni chakula kwa ajili yenu. Baada ya siku tatu mtavuka mto huu wa Yordani na kuingia ndani na kuimiliki nchi ambayo Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi ili kuimiliki.””
12 And to the Reubenite, and to the Gadite, and to the half of the tribe of Manasseh, hath Joshua spoken, saying,
Yoshua akawaambia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase,
13 'Remember the word which Moses, servant of Jehovah, commanded you, saying, Jehovah your God is giving rest to you, and He hath given to you this land;
“Kumbukeni maneno ambayo Musa, mtumishi wa Yahweh, aliwaaagiza aliposema, 'Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi pumziko, naye awapeni ninyi nchi hii.'
14 your wives, your infants, and your substance, abide in the land which Moses hath given to you beyond the Jordan, and ye — ye pass over by fifties, before your brethren, all the mighty ones of valour, and have helped them,
Wake zenu, na watoto wenu na mifugo yenu itakaa katika nchi ambayo Musa aliwapa ninyi ng'ambo ya Yordani. Lakini watu wenu wa vita wataenda pamoja na ndugu zao na kuwasaidia.
15 till that Jehovah giveth rest to your brethren as to yourselves, and they have possessed, even they, the land which Jehovah your God is giving to them; then ye have turned back to the land of your possession, and have possessed it, which Moses, servant of Jehovah, hath given to you beyond the Jordan, [at] the sun-rising.'
Mpaka hapo Yahweh atakapowapa ndugu zenu pumziko kama alivyowapa ninyi. Na wao pia watamiliki nchi ambayo Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi. Kisha mtarudi katika nchi yenu na kuimiliki, nchi ambayo Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa ninyi ng'ambo ya Yordani, mahali pa mapambazuko ya jua.”
16 And they answer Joshua, saying, 'All that thou hast commanded us we do; and unto every [place] whither thou dost send us, we go;
Nao wakamjibu Yoshua, na kusema, “Mambo yote uliyotuagiza tutayafanya, na kila mahali utakapotutuma tutaenda.
17 according to all that we hearkened unto Moses [in], so we hearken unto thee; surely Jehovah thy God is with thee as He hath been with Moses.
Tutakutii kama tulivyomtii Musa. Yahweh Mungu wako na awe pamoja nawe tu kama aliyokuwa pamoja na Musa.
18 Any man who doth provoke thy mouth, and doth not hear thy words, in all that thou dost command him, is put to death; only, be strong and courageous.'
Yeyote anayeasi maagizo yako na kutotii maneno yako atauawa. Uwe hodari na jasiri tu.

< Joshua 1 >