< 1 Kings 11 >

1 And king Solomon hath loved many strange women, and the daughter of Pharaoh, females of Moab, Ammon, Edom, Zidon, [and] of the Hittites,
Hata hivyo, Mfalme Solomoni akawapenda wanawake wengi wa kigeni zaidi, mbali na binti Farao: wanawake wa Wamoabu, Waamoni, Waedomu, Wasidoni na Wahiti.
2 of the nations of which Jehovah said unto the sons of Israel, 'Ye do not go in to them, and they do not go in to you; surely they turn aside your heart after their gods;' to them hath Solomon cleaved for love.
Walitoka katika mataifa ambayo Bwana aliwaambia Waisraeli, “Msije mkaoana nao, kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu mgeukie miungu yao.” Hata hivyo, Solomoni akakaza kuwapenda.
3 And he hath women, princesses, seven hundred, and concubines three hundred; and his wives turn aside his heart.
Alikuwa na wake 700 mabinti wa uzao wa kifalme, na masuria 300, nao wake zake wakampotosha.
4 And it cometh to pass, at the time of the old age of Solomon, his wives have turned aside his heart after other gods, and his heart hath not been perfect with Jehovah his God, like the heart of David his father.
Kadiri Solomoni alivyozidi kuzeeka, wake zake wakaugeuza moyo wake kuelekea miungu mingine, na moyo wake haukujitolea kikamilifu kwa Bwana Mungu wake, kama ulivyokuwa moyo wa Daudi baba yake.
5 And Solomon goeth after Ashtoreth god[dess] of the Zidonians, and after Milcom the abomination of the Ammonites;
Solomoni akafuata Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, na Moleki mungu aliyekuwa chukizo la Waamoni.
6 and Solomon doth the evil thing in the eyes of Jehovah, and hath not been fully after Jehovah, like David his father.
Kwa hiyo Solomoni akafanya uovu machoni pa Bwana; hakumfuata Bwana kikamilifu kama alivyofanya Daudi baba yake.
7 Then doth Solomon build a high place for Chemosh the abomination of Moab, in the hill that [is] on the front of Jerusalem, and for Molech the abomination of the sons of Ammon;
Kwenye kilima mashariki mwa Yerusalemu, Solomoni akajenga mahali pa juu kwa ajili ya Kemoshi chukizo la Wamoabu, na kwa Moleki mungu chukizo la Waamoni.
8 and so he hath done for all his strange women, who are perfuming and sacrificing to their gods.
Akafanya hivyo kwa wake zake wote wa kigeni, ambao walifukiza uvumba na kutoa dhabihu kwa miungu yao.
9 And Jehovah sheweth Himself angry with Solomon, for his heart hath turned aside from Jehovah, God of Israel, who had appeared unto him twice,
Bwana akamkasirikia Solomoni kwa sababu moyo wake uligeuka mbali na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye alikuwa amemtokea mara mbili.
10 and given a charge unto him concerning this thing, not to go after other gods; and he hath not kept that which Jehovah commanded,
Ingawa alikuwa amemkataza Solomoni kufuata miungu mingine, Solomoni hakutii amri ya Bwana.
11 and Jehovah saith to Solomon, 'Because that this hath been with thee, and thou hast not kept My covenant and My statutes that I charged upon thee, I surely rend the kingdom from thee, and have given it to thy servant.
Kwa hiyo Bwana akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa hii ndiyo hali yako na hukushika Agano langu na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme kutoka kwako na kumpa mmoja wa walio chini yako.
12 'Only, in thy days I do it not, for the sake of David thy father; out of the hand of thy son I rend it;
Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi baba yako, sitafanya jambo hili wakati wa uhai wako. Nitaurarua kutoka mikononi mwa mwanao.
13 only all the kingdom I do not rend away; one tribe I give to thy son, for the sake of David My servant, and for the sake of Jerusalem, that I have chosen.'
Lakini pia sitaurarua ufalme wote kutoka kwake, bali nitampa kabila moja kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu na kwa ajili ya Yerusalemu, ambao nimeuchagua.”
14 And Jehovah raiseth up an adversary to Solomon, Hadad the Edomite; of the seed of the king [is] he in Edom;
Kisha Bwana akamwinua adui dhidi ya Solomoni, Hadadi, Mwedomu, kutoka ukoo wa ufalme wa Edomu.
15 and it cometh to pass, in David's being with Edom, in the going up of Joab head of the host to bury the slain, that he smiteth every male in Edom —
Huko nyuma wakati Daudi alipokuwa akipigana na Edomu, Yoabu jemadari wa jeshi, aliyekuwa amekwenda kuzika waliouawa, alikuwa amewaua wanaume wote waliokuwako Edomu.
16 for six months did Joab abide there, and all Israel, till the cutting off of every male in Edom —
Yoabu na Waisraeli wote walikaa huko kwa miezi sita, mpaka walipomaliza kuwaangamiza wanaume wote huko Edomu.
17 and Hadad fleeth, he and certain Edomites, of the servants of his father, with him, to go in to Egypt, and Hadad [is] a little youth,
Lakini Hadadi, akiwa bado mvulana mdogo, alikimbilia Misri akiwa na baadhi ya maafisa wa Kiedomu waliokuwa wakimhudumia baba yake.
18 and they rise out of Midian, and come into Paran, and take men with them out of Paran, and come in to Egypt, unto Pharaoh king of Egypt, and he giveth to him a house, and bread hath commanded for him, and land hath given to him.
Wakaondoka Midiani wakaenda Parani. Basi wakichukua pamoja nao wanaume kutoka Parani, wakaenda Misri, kwa Farao mfalme wa Misri, ambaye alimpa Hadadi nyumba, ardhi na akampatia chakula.
19 And Hadad findeth grace in the eyes of Pharaoh exceedingly, and he giveth to him a wife, the sister of his own wife, sister of Tahpenes the mistress;
Farao akapendezwa sana na Hadadi hata akampa ndugu wa mkewe mwenyewe, Malkia Tapenesi, ili aolewe na Hadadi.
20 and the sister of Tahpenes beareth to him Genubath his son, and Tahpenes weaneth him within the house of Pharaoh, and Genubath is in the house of Pharaoh in the midst of the sons of Pharaoh.
Huyo ndugu wa Tapenesi akamzalia mwana aliyeitwa Genubathi, ambaye alilelewa na Tapenesi katika jumba la kifalme. Huko Genubathi aliishi pamoja na watoto wa Farao mwenyewe.
21 And Hadad hath heard in Egypt that David hath lain with his fathers, and that Joab head of the host is dead, and Hadad saith unto Pharaoh, 'Send me away, and I go unto my land.'
Alipokuwa huko Misri, Hadadi alisikia kwamba Daudi amepumzika na baba zake na ya kwamba pia Yoabu aliyekuwa jemadari wa jeshi amekufa. Ndipo Hadadi akamwambia Farao, “Niruhusu niende ili niweze kurudi katika nchi yangu.”
22 And Pharaoh saith to him, 'But, what art thou lacking with me, that lo, thou art seeking to go unto thine own land?' and he saith, 'Nay, but thou dost certainly send me away.'
Farao akauliza, “Umekosa nini hapa, kwamba unataka kurudi katika nchi yako?” Hadadi akajibu, “Hakuna, lakini niruhusu niende!”
23 And God raiseth to him an adversary, Rezon son of Eliadah, who hath fled from Hadadezer king of Zobah, his lord,
Mungu akamwinua adui mwingine dhidi ya Solomoni, Rezoni mwana wa Eliada, ambaye alikuwa amemkimbia bwana wake Hadadezeri, mfalme wa Soba.
24 and gathereth unto himself men, and is head of a troop in David's slaying them, and they go to Damascus, and dwell in it, and reign in Damascus;
Akawakusanya watu, naye akawa kiongozi wa kundi la waasi, wakati Daudi alipoangamiza majeshi ya Soba; waasi walikwenda Dameski, mahali walipokaa na kumiliki.
25 and he is an adversary to Israel all the days of Solomon, (besides the evil that Hadad [did]), and he cutteth off in Israel, and reigneth over Aram.
Rezoni alikuwa adui wa Israeli kwa muda wote alioishi Solomoni, ukiongezea matatizo yaliyosababishwa na Hadadi. Kwa hiyo Rezoni akatawala katika Aramu na alikuwa mkatili kwa Israeli.
26 And Jeroboam son of Nebat, an Ephrathite of Zereda — the name of whose mother [is] Zeruah, a widow woman — servant to Solomon, he also lifteth up a hand against the king;
Pia, Yeroboamu mwana wa Nebati aliasi dhidi ya mfalme. Alikuwa mmoja wa maafisa wa Solomoni, Mwefraimu kutoka Sereda, ambaye mama yake alikuwa mjane aliyeitwa Serua.
27 and this [is] the thing [for] which he lifted up a hand against the king: Solomon built Millo — he shut up the breach of the city of David his father,
Haya ndiyo maelezo ya jinsi alivyomwasi mfalme: Solomoni alikuwa amejenga Milo naye akawa ameziba mwanya katika ukuta wa mji wa Daudi baba yake.
28 and the man Jeroboam [is] mighty in valour, and Solomon seeth the young man that he is doing business, and appointeth him over all the burden of the house of Joseph.
Basi Yeroboamu alikuwa mtu shujaa na hodari, naye Solomoni alipoona jinsi kijana alivyofanya kazi yake, akamweka kuwa kiongozi wa kazi yote ya mikono ya nyumba ya Yosefu.
29 And it cometh to pass, at that time, that Jeroboam hath gone out from Jerusalem, and Ahijah the Shilonite, the prophet, findeth him in the way, and he is covering himself with a new garment; and both of them [are] by themselves in a field,
Karibu na wakati ule Yeroboamu alikuwa anatoka nje ya Yerusalemu, Ahiya nabii Mshiloni akakutana naye njiani, akiwa amevaa joho jipya. Hawa wawili walikuwa peke yao mashambani,
30 and Ahijah layeth hold on the new garment that [is] on him, and rendeth it — twelve pieces,
naye Ahiya akachukua joho jipya alilokuwa amevaa akalirarua vipande kumi na viwili.
31 and saith to Jeroboam, 'Take to thee ten pieces, for thus said Jehovah, God of Israel, lo, I am rending the kingdom out of the hand of Solomon, and have given to thee the ten tribes,
Kisha akamwambia Yeroboamu, “Chukua vipande kumi kwa ajili yako, kwa kuwa hivi ndivyo Bwana, Mungu wa Israeli asemavyo: ‘Tazama, ninakwenda kuuchana ufalme kutoka mikononi mwa Solomoni na kukupa wewe makabila kumi.
32 and the one tribe he hath for My servant David's sake, and for Jerusalem's sake, the city which I have fixed on, out of all the tribes of Israel.
Lakini kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi na mji wa Yerusalemu, ambao nimeuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli, atakuwa na kabila moja.
33 'Because they have forsaken Me, and bow themselves to Ashtoreth, god[dess] of the Zidonians, to Chemosh god of Moab, and to Milcom god of the sons of Ammon, and have not walked in My ways, to do that which [is] right in Mine eyes, and My statutes and My judgments, like David his father.
Nitafanya hivi kwa sababu wameniacha mimi na kuabudu Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, Kemoshi mungu wa Wamoabu, na Moleki mungu wa Waamoni, nao hawakwenda katika njia zangu ili kufanya yaliyo sawa machoni pangu, wala kushika amri na sheria zangu kama Daudi, babaye Solomoni, alivyofanya.
34 'And I do not take the whole of the kingdom out of his hand, for prince I make him all days of his life, for the sake of David My servant whom I chose, who kept My commands and My statutes;
“‘Lakini sitauondoa ufalme wote kutoka mikononi mwa Solomoni, nimemfanya mtawala siku zote za maisha yake kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, niliyemchagua na ambaye aliyatunza maagizo na amri zangu.
35 and I have taken the kingdom out of the hand of his son, and given it to thee — the ten tribes;
Nitauondoa ufalme kutoka mikononi mwa mwanawe na kukupa wewe makabila kumi.
36 and to his son I give one tribe, for there being a lamp to David My servant all the days before Me in Jerusalem, the city that I have chosen to Myself to put My name there.
Nitampa mwanawe kabila moja ili kwamba Daudi mtumishi wangu awe na taa mbele zangu daima katika Yerusalemu, mji ambao nimeuchagua kuweka Jina langu.
37 'And thee I take, and thou hast reigned over all that thy soul desireth, and thou hast been king over Israel;
Hata hivyo, kukuhusu wewe Yeroboamu, nitakutwaa, nawe utatawala juu ya yote yale moyo wako unayotamani, utakuwa mfalme juu ya Israeli.
38 and it hath been, if thou dost hear all that I command thee, and hast walked in My ways, and done that which is right in Mine eyes, to keep My statutes and My commands, as did David My servant, that I have been with thee, and have built for thee a stedfast house, as I built for David, and have given to thee Israel,
Ikiwa utafanya kila nitakalokuamuru, kuenenda katika njia zangu na kufanya yaliyo sawa mbele za macho yangu kwa kuzishika amri zangu na maagizo yangu kama alivyofanya Daudi mtumishi wangu, nitakuwa pamoja nawe. Nitakujengea ufalme utakaodumu kama ule niliomjengea Daudi, nami nitakupa Israeli.
39 and I humble the seed of David for this; only, not all the days.'
Nitawatesa wazao wa Daudi kwa ajili ya hili, lakini siyo milele.’”
40 And Solomon seeketh to put Jeroboam to death, and Jeroboam riseth and fleeth to Egypt, unto Shishak king of Egypt, and he is in Egypt till the death of Solomon.
Solomoni akajaribu kumuua Yeroboamu, lakini Yeroboamu akakimbilia Misri, kwa Mfalme Shishaki, naye akakaa huko mpaka Solomoni alipofariki.
41 And the rest of the matters of Solomon, and all that he did, and his wisdom, are they not written on the book of the matters of Solomon?
Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, yote aliyoyafanya na hekima aliyoionyesha, je hayakuandikwa yote katika kitabu cha matendo cha Solomoni?
42 And the days that Solomon hath reigned in Jerusalem over all Israel [are] forty years,
Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
43 and Solomon lieth with his fathers, and is buried in the city of David his father, and reign doth Rehoboam his son in his stead.
Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 1 Kings 11 >