< Numbers 9 >

1 And the Lord spak to Moises, in the deseert of Synay, in the secounde yeer aftir that thei yeden out of the lond of Egipt, in the firste moneth,
Bwana akasema na Mose katika Jangwa la Sinai katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka Misri. Akasema,
2 and seide, The sones of Israel make pask in his tyme,
“Waamuru Waisraeli waadhimishe Pasaka katika wakati ulioamriwa.
3 in the fourtenthe day of this monethe, at the euentid, bi alle the cerymonyes and iustifiyngis therof.
Adhimisheni wakati ulioamriwa, yaani wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi huu, kufuatana na desturi zake zote na masharti yake.”
4 And Moises comaundide to the sones of Israel, that thei schulden make pask;
Hivyo Mose akawaambia Waisraeli waiadhimishe Pasaka,
5 whiche maden in his tyme, in the fourtenthe dai of the monethe, at euentid, in the hil of Synai; bi alle thingis whiche the Lord comaundide to Moises, the sones of Israel diden.
nao wakafanya hivyo kwenye Jangwa la Sinai wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza. Waisraeli wakafanya kila kitu kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
6 Lo! forsothe summen vncleene on the soule of man, that myyten not make pask in that dai, neiyiden to Moises and Aaron,
Lakini baadhi yao hawakuweza kuadhimisha Pasaka siku ile kwa sababu walikuwa najisi kwa taratibu za kiibada kwa ajili ya kugusa maiti. Kwa hiyo wakamwendea Mose na Aroni siku ile ile,
7 and seiden to hem, We ben vncleene `on the soule of man; whi ben we defraudid, that we moun not offre an offryng to the Lord in his tyme, among the sones of Israel?
wakamwambia Mose, “Tumekuwa najisi kwa sababu tumegusa maiti, lakini kwa nini tuzuiliwe kumtolea Bwana sadaka yake pamoja na Waisraeli wengine katika wakati ulioamriwa?”
8 To whiche Moises answeride, Stonde ye, that Y take counseil, what the Lord comaundith of you.
Mose akawajibu, “Ngojeni mpaka nitafute kile Bwana anachoagiza kuwahusu ninyi.”
9 And the Lord spak to Moises, and seide,
Ndipo Bwana akamwambia Mose,
10 Speke thou to the sones of Israel, A man of youre folk which is vncleene `on the soule, ether in the weie fer, make he pask to the Lord in the secounde monethe,
“Waambie Waisraeli: ‘Wakati mmoja wenu au wazao wenu wanapokuwa najisi kwa sababu ya maiti au wakiwa safarini, hata hivyo wanaweza kuadhimisha Pasaka ya Bwana.
11 in the fourtenthe dai of the monethe, at euentid; with therf looues and letusis of the feeld he schal ete it.
Wataiadhimisha wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Watamla mwana-kondoo, pamoja na mkate usiotiwa chachu, na mboga chungu.
12 Thei schulen not leeue ony thing therof til the morewtid, and thei schulen not breke a boon therof; thei schulen kepe al the custom of pask.
Wasibakize chochote hadi asubuhi wala wasivunje mifupa ya mwana-kondoo. Wakati wanapoadhimisha Pasaka, hawana budi kufuata masharti yote.
13 Forsothe if ony man is bothe cleene, and is not in the weie, and netheles made not pask, thilke man schal be distried fro hise puplis, for he offeride not sacrifice to the Lord in his tyme; he schal bere his synne.
Lakini kama mtu ni safi kwa taratibu za kiibada naye hayuko safarini, asipoadhimisha Pasaka, mtu huyo hana budi kukatiliwa mbali na watu wake kwa sababu hakutoa sadaka ya Bwana kwa wakati ulioamriwa. Mtu huyo atawajibika kubeba matokeo ya dhambi yake.
14 Also if a pilgrym and comelyng is anentis you, make he pask to the Lord, bi the cerymonyes and iustifiyngis therof; the same comaundement schal be anentis you, as wel to a comelyng as to a man borun in the loond.
“‘Mgeni anayeishi miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana, lazima afanye hivyo kwa kufuata desturi na masharti. Lazima masharti yawe sawasawa kwa mgeni na mzawa.’”
15 Therfore in the dai in which the tabernacle was reisid, a cloude hilide it; sotheli as the licnesse of fier was on the tente fro euentid til the morewtid.
Katika siku hiyo ambayo Maskani, Hema la Ushuhuda, iliposimamishwa, wingu liliifunika. Kuanzia jioni mpaka asubuhi wingu lililokuwa juu ya Maskani lilionekana kama moto.
16 Thus it was don continueli, a cloude hilide it bi dai, and as the licnesse of fier bi nyyt.
Hivyo ndivyo lilivyoendelea kuwa; wingu liliifunika wakati wa mchana, na usiku lilionekana kama moto.
17 And whanne the cloude that hilide the tabernacle was takun awei, thanne the sones of Israel yeden forth, and in the place where the cloude stood, there thei settiden tentis.
Wakati wowote wingu lilipoinuka kutoka juu ya Hema, nao Waisraeli waliondoka; mahali popote wingu liliposimama, Waisraeli walipiga kambi.
18 At the comaundement of the Lord thei yeden forth, and at his comaundement thei settiden the tabernacle. In alle daies in whiche the cloude stood on the tabernacle, thei dwelliden in the same place.
Kwa amri ya Bwana Waisraeli waliondoka, na kwa amri yake walipiga kambi. Kwa muda wote wingu liliposimama juu ya Maskani, Waisraeli walibaki wamepiga kambi.
19 And if it bifelde that it dwellide in myche tyme on the tabernacle, the sones of Israel weren in the watchis of the Lord, and thei yeden not forth,
Wakati wingu lilipobaki juu ya Maskani kwa muda mrefu, Waisraeli walitii amri ya Bwana nao hawakuondoka.
20 in hou many euer daies the cloude was on the tabernacle. At the comaundement of the Lord thei reisiden tentis, and at his comaundement thei diden doun.
Wakati mwingine wingu lilikuwa juu ya Maskani kwa siku chache tu; kwa amri ya Bwana wangelipiga kambi na kisha kwa amri yake wangeliondoka.
21 If the cloude was fro euentid `til to the morewtid, and anoon in the morewtid hadde left, thei yeden forth; and if aftir a dai and nyyt it hadde go awei, thei scateriden, `ether diden doun, tentis.
Wakati mwingine wingu lilikuwepo kuanzia jioni mpaka asubuhi tu, na lilipoinuka asubuhi, nao waliondoka. Ikiwa ni mchana au usiku, wakati wowote wingu lilipoinuka, waliondoka.
22 Whether in two monethis, ether in o monethe, ether in lengere tyme, `the cloude hadde be on the tabernacle, the sones of Israel dwelliden in the same place, and yeden not forth; but anoon as it hadde go awey, thei moueden tentis.
Ikiwa wingu lilikaa juu ya Maskani kwa siku mbili au mwezi au mwaka, Waisraeli wangebaki wamepiga kambi na hawakuondoka; lakini lilipoinuka, wangeondoka.
23 Bi the word of the Lord thei settiden tentis, and bi his word thei wenten forth; and thei weren in the watchis of the Lord, bi his comaundement, bi the hond of Moyses.
Kwa amri ya Bwana walipiga kambi, na kwa amri ya Bwana waliondoka. Walitii amri ya Bwana, kufuatana na agizo lake kupitia Mose.

< Numbers 9 >