< Numbers 13 >

1 And there the Lord spak to Moises,
Bwana akamwambia Mose,
2 and seide, Sende thou men that schulen biholde the lond of Canaan, which Y schal yyue to the sones of Israel, of ech lynage o man of the princes.
“Watume baadhi ya watu wakaipeleleze nchi ya Kanaani, ambayo ninawapa Waisraeli. Kutoka kwa kila kabila la baba zao, tuma mmoja wa viongozi wao.”
3 Moises dide that that the Lord comaundide, and sente fro the deseert of Pharan princes, men of whiche these ben the names.
Hivyo kwa agizo la Bwana Mose akawatuma kutoka Jangwa la Parani. Wote walikuwa viongozi wa Waisraeli.
4 Of the lynage of Ruben, Semmya, the sone of Zectur.
Haya ndiyo majina yao: kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;
5 Of the lynage of Symeon, Saphat, the sone of Hury.
kutoka kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;
6 Of the lynage of Juda, Caleph, the sone of Jephone.
kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune;
7 Of the lynage of Isachar, Igal, the sone of Joseph.
kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yosefu;
8 Of the lynage of Effraym, Osee, the sone of Nun.
kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
9 Of the lynage of Beniamyn, Phalti, the sone of Raphu.
kutoka kabila la Benyamini, Palti mwana wa Rafu;
10 Of the lynage of Zabulon, Gediel, the sone of Sodi.
kutoka kabila la Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi,
11 Of the lynage of Joseph, of the gouernaunce of Manasses, Gaddi, the sone of Susy.
kutoka kabila la Manase (kabila la Yosefu), Gadi mwana wa Susi;
12 Of the lynage of Dan, Amyel, the sone of Gemalli.
kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemali;
13 Of the lynage of Aser, Sur, the sone of Mychael.
kutoka kabila la Asheri, Sethuri mwana wa Mikaeli;
14 Of the lynage of Neptalym, Nabdi, the sone of Napsi.
kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Wofsi;
15 Of the lynage of Gad, Guel, the sone of Machi.
kutoka kabila la Gadi, Geueli mwana wa Maki.
16 These ben the names of men, which Moises sente to biholde the lond of Canaan; and he clepide Osee, the sone of Nun, Josue.
Haya ndiyo majina ya watu ambao Mose aliwatuma kuipeleleza nchi. (Mose akampa Hoshea mwana wa Nuni jina Yoshua.)
17 Therfor Moises sente hem to biholde the lond of Canaan, and seide to hem, `Stie ye bi the south coost; and whanne ye comen to the hillis,
Mose alipowatuma wakaipeleleze Kanaani, alisema, “Pandeni kupitia Negebu, mwende mpaka nchi ya vilima.
18 biholde ye the lond, what maner lond it is; and biholde ye the puple which is the dwellere therof, whether it is strong, ethir feble, `whether thei ben fewe in noumbre, ether manye;
Mwone nchi ni ya namna gani, na kama watu waishio humo wana nguvu au ni wadhaifu, iwapo ni wachache au wengi.
19 whether that lond is good, ethir yuel; what maner citees ben, wallid, ether without wallis;
Wanaishi katika nchi ya namna gani? Je, ni nzuri au mbaya? Wanaishi katika miji ya namna gani? Je, haina kuta au ngome?
20 whether the lond is fat, ether bareyn, `whether it is ful of woodis, ethir without trees. Be ye coumfortid, and `brynge ye to vs of the fruytis of that lond. Sotheli the tyme was, whanne grapis first ripe myyten be etun thanne.
Ardhi iko aje? Ina rutuba au la? Je, kuna miti ndani yake au la? Jitahidini kadiri mwezavyo kuleta baadhi ya matunda ya nchi.” (Ulikuwa msimu wa kuiva zabibu za kwanza.)
21 And whanne thei hadden stied, thei aspieden the lond, fro the deseert of Syn `til to Rohob, as men entryth to Emath.
Hivyo wakapanda na kuipeleleza nchi kutoka Jangwa la Sini hadi Rehobu, kuelekea Lebo-Hamathi.
22 And thei stieden to the south, and camen in to Ebron, where Achyman, and Sisai, and Tholmai, the sones of Enach, weren; for Hebron was maad bi seuen yeer bifor Thamnys, the citee of Egipt.
Wakapanda kupitia Negebu hadi wakafika Hebroni, mahali ambapo Ahimani, Sheshai na Talmai, wazao wa Anaki, waliishi. (Hebroni ulikuwa umejengwa miaka saba kabla ya mji wa Soani ulioko Misri.)
23 And thei yeden til to the stronde of clustre, and kittiden doun a sioun with his grape, which twei men baren in a barre; also thei token of pumgarnadis, and of the figis of that place which is clepid Nehelescol,
Walipofika katika Bonde la Eshkoli, walivunja tawi lililokuwa na kishada kimoja cha zabibu. Wawili wao wakalichukua lile tawi kwenye mti, pamoja na komamanga na tini.
24 that is, the stronde of grape, for the sones of Israel baren a clustre fro thennus.
Eneo lile likaitwa Bonde la Eshkoli kwa sababu ya kile kishada cha zabibu ambacho Waisraeli walikikata huko.
25 And the aspieris of the lond, whanne thei hadden cumpassid al the cuntrey, after fourti daies camen to Moises and Aaron,
Mwishoni mwa siku arobaini wakarudi kutoka kuipeleleza nchi.
26 and to al the cumpany of the sones of Israel, in to the deseert of Pharan which is in Cades. And `the aspieris spaken to hem, and schewiden the fruytis of the lond to al the multitude, and telden,
Wakarudi kwa Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli huko Kadeshi kwenye Jangwa la Parani. Hapo ndipo walipotoa habari kwao na kwa kusanyiko lote na kuwaonyesha matunda ya hiyo nchi.
27 and seiden, We camen to the lond, to which thou sentest vs, which lond treuli flowith with mylk and hony, as it may be knowun bi these fruytis;
Wakampa Mose taarifa hii: “Tuliingia katika nchi uliyotutuma, nayo inatiririka maziwa na asali! Hili hapa tunda lake.
28 but it hath strongeste inhabiteris, and grete cytees, and wallid; we sien there the kynrede of Anachym; Amalech dwellith in the south;
Lakini watu wanaoishi huko ni wenye nguvu, na miji yao ina ngome na ni mikubwa sana. Huko tuliona hata wazao wa Anaki.
29 Ethei, and Jebusei, and Amorey dwellen in the hilli placis; forsothe Cananey dwellith bisidis the see, and bisidis the floodis of Jordan.
Waamaleki wanaishi Negebu; Wahiti, Wayebusi na Waamori wanaishi katika nchi ya vilima; nao Wakanaani wanaishi karibu na bahari na kando ya Yordani.”
30 Among thes thingis Caleph peeside the grutchyng of the puple, that was maad ayens Moises, and seide, `Stie we, and welde we the lond, for we moun gete it.
Kisha Kalebu akawanyamazisha watu mbele ya Mose na kusema, “Imetupasa kupanda na kuimiliki nchi, kwa maana hakika tunaweza kufanya hivyo.”
31 Forsothe other aspieris, that weren with hym, seiden, We moun not stie to this puple, for it is strongere than we.
Lakini watu waliokuwa wamepanda pamoja naye wakasema, “Hatuwezi kuwashambulia wale watu; wana nguvu kutuliko sisi.”
32 And thei deprauyden the lond which thei hadden biholde, anentis the sones of Israel, and seiden, The lond which we cumpassiden deuourith hise dwelleris; the puple which we bihelden is of large stature; there we syen summe wondris ayens kynde,
Wakaeneza taarifa mbaya miongoni mwa Waisraeli kuhusu nchi waliyoipeleleza. Wakasema, “Nchi tuliyoipeleleza hula watu waishio ndani yake. Watu wote tuliowaona huko ni majitu.
33 of the sones of Enach, of the kynde of geauntis, to whiche we weren comparisound, and weren seien as locustis.
Tuliwaona Wanefili huko (wazao wa Anaki wanatokana na Wanefili.) Tulijiona kama panzi machoni petu wenyewe, nao ndivyo walivyotuona.”

< Numbers 13 >