< Leviticus 7 >

1 And this is the lawe of sacrifice for trespas; it is hooli `of the noumbre of hooli thingis.
“‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya hatia, ambayo ni takatifu sana:
2 Therfor where brent sacrifice is offrid, also the sacrifice for trespas schal be slayn; the blood therof schal be sched bi the cumpas of the auter.
Sadaka ya hatia itachinjiwa mahali pale ambapo sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, nayo damu yake itanyunyizwa pande zote za madhabahu.
3 Thei schulen offre the tail therof, and the fatnesse that hilith the entrailis,
Mafuta yake yote yatatolewa sadaka: mafuta ya mkia na mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani,
4 the twei litle reynes, and the fatnesse which is bisidis ilioun, and the calle of the mawe, with the litle reynes.
figo zote mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo yataondolewa pamoja na hizo figo.
5 And the preest schal brenne tho on the auter; it is encense of the Lord, for trespas.
Kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kuwa sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto. Hii ni sadaka ya hatia.
6 Ech male of the preestis kyn schal ete these fleischis in the hooli place, for it is hooli `of the noumbre of hooli thingis.
Mwanaume yeyote katika jamaa ya kuhani aweza kuila, lakini lazima iliwe mahali patakatifu; ni takatifu sana.
7 As a sacrifice is offrid for synne, so and for trespas, o lawe schal be of euer eithir sacrifice; it schal perteyne to the preest, that offrith it.
“‘Sheria hii ya sadaka ya hatia ni sawasawa na ile ya sadaka ya dhambi: Nyama ya yule mnyama aliyetolewa sadaka ni ya yule kuhani anayesimamia ibada ya upatanisho.
8 The preest that offrith the beeste of brent sacrifice, schal haue the skyn therof.
Kuhani anayetoa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya mtu yeyote anaweza kuichukua ngozi ya mnyama yule aliyetolewa iwe yake.
9 And ech sacrifice of wheete flour, which is bakun in an ouene, and what euer is maad redi in a gridile, ethir in a friyng panne, it schal be that preestis, of whom it is offrid,
Kila sadaka ya nafaka iliyookwa jikoni au kupikwa katika sufuria au katika kikaangio itakuwa ya kuhani anayeitoa.
10 whether it is spreynt with oile, ethir is drye. To alle the sones of Aaron euene mesure schal be departyd, `to ech `bi hem silf.
Nayo kila sadaka ya nafaka, iwe imechanganywa na mafuta au iko kavu, itakuwa ya wana wa Aroni, nayo itagawanywa sawa kati yao.
11 This is the lawe of `the sacrifice of pesible thingis, which is offrid to the Lord.
“‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya amani ambayo mtu aweza kuileta kwa Bwana:
12 If the offryng is for doyng of thankyngis, thei schulen offre looues without sour dow spreynt with oile, and `therf looues sodun in watir, that ben anoyntid with oile; and thei schulen offre wheete flour bakun, and thinne looues spreynt to gidere with the medlyng of oile.
“‘Ikiwa mtu atatoa sadaka ya amani kwa ajili ya kuonyesha shukrani, pamoja na sadaka hii ya shukrani, atatoa maandazi yasiyotiwa chachu yaliyochanganywa na mafuta, mikate myembamba isiyotiwa chachu iliyopakwa mafuta, maandazi ya unga laini uliokandwa vizuri na kuchanganywa na mafuta.
13 Also thei schulen offre `looues diyt with sour dow, with the sacrifice of thankyngis which is offrid for pesible thingis;
Pamoja na sadaka hii ya amani ya shukrani ataleta sadaka ya maandazi yaliyotengenezwa kwa chachu.
14 of whiche o loof schal be offrid to the Lord for the firste fruytis, and it schal be the preestis that schal schede the blood of the sacrifice,
Ataleta moja ya kila aina ya andazi kama sadaka, matoleo kwa Bwana; hii ni ya kuhani anayenyunyiza damu ya sadaka ya amani.
15 whose fleischis schulen be etun in the same dai, nether ony thing of tho schal dwelle til the morewtid.
Nyama ya sadaka ya amani kwa ajili ya shukrani lazima iliwe siku iyo hiyo inapotolewa; hutabakiza kitu chochote mpaka asubuhi.
16 If a man offrith a sacrifice bi a vow, ethir bi fre wille, it schal be etun in lijk maner in the same dai; but also if ony thing dwellith `in to the morew, it is leueful to ete it;
“‘Lakini kama sadaka yake ni kwa ajili ya nadhiri au ni sadaka ya hiari, sadaka hiyo italiwa siku hiyo inapotolewa, lakini chochote kinachobakia kinaweza kuliwa kesho yake.
17 sotheli fier schal waaste, whateuer thing the thridde day schal fynde.
Nyama yoyote ya sadaka inayobaki mpaka siku ya tatu lazima iteketezwe kwa moto.
18 If ony man etith in the thridde dai of the fleischis of sacrifice of pesible thingis, his offryng schal be maad voide, nethir it schal profite to the offerere; but rather whateuer soule defoulith hym silf with suche mete, he schal be gilti of `brekyng of the lawe.
Kama nyama yoyote ya sadaka ya amani italiwa siku ya tatu, Bwana hataikubali. Haitahesabiwa kwake huyo aliyeitoa, kwa kuwa ni najisi. Mtu atakayekula sehemu yake yoyote atahesabiwa hatia.
19 Fleisch that touchith ony vnclene thing, schal not be etun, but it schal be brent bi fier; he that is clene, schal ete it.
“‘Nyama ile inayogusa chochote ambacho ni najisi kwa kawaida ya ibada kamwe haitaliwa, ni lazima iteketezwe kwa moto. Kuhusu nyama nyingine, mtu yeyote aliye safi kwa kawaida ya ibada anaweza kuila.
20 A pollutid soule, that etith of the fleischis of the sacrifice of pesible thingis, which is offrid to the Lord, schal perische fro hise puplis.
Lakini kama mtu yeyote najisi akila nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, huyo mtu lazima akatiliwe mbali na watu wake.
21 And he that touchith vnclennesse of man, ether of beeste, ether of alle thing that may defoule, and etith of suche fleischis, schal perische fro hise puplis.
Kama mtu yeyote akigusa kitu kilicho najisi, iwe ni uchafu wa mwanadamu, au mnyama najisi, au kitu chochote kilicho najisi, kitu cha kuchukiza, kisha akala nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.’”
22 And the Lord spak to Moises,
Bwana akamwambia Mose,
23 and seide, Speke thou to the sones of Israel, Ye schulen not ete the ynnere fatnesse of a scheep, of an oxe, and of a geet;
“Waambie Waisraeli: ‘Msile mafuta yoyote ya ngʼombe, kondoo wala mbuzi.
24 ye schulen haue in to dyuerse vsis the ynnere fatnesse of a carkeis deed by it silf, and of that beeste which is takun of a rauenus beeste.
Mafuta ya mnyama aliyekutwa amekufa au ameraruliwa na mnyama pori yanaweza kutumika kwa kazi nyingine yoyote, lakini kamwe msiyale.
25 If ony man etith the ynnere fatnesse, that owith to be offrid in to encense of the Lord, he schal perische fro his puple.
Mtu yeyote alaye mafuta ya mnyama ambaye ametolewa sadaka kwa Bwana kwa moto ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
26 Also ye schulen not take in mete the blood of ony beeste, as wel of briddis as of beestis;
Popote mtakapoishi, kamwe msinywe damu ya ndege yeyote wala ya mnyama.
27 ech man that etith blood schal perische fro his puplis.
Ikiwa mtu yeyote atakunywa damu, mtu huyo lazima akatiliwe mbali na watu wake.’”
28 And the Lord spak to Moises,
Bwana akamwambia Mose,
29 and seide, Speke thou to the sones of Israel, He that offrith a sacrifice of pesible thingis to the Lord, offre togidere also a sacrifice, that is, fletynge offryngis therof.
“Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote aletaye sadaka ya amani kwa Bwana ataleta sehemu ya sadaka hiyo kama dhabihu yake kwa Bwana.
30 He schal holde in the hondis the ynnere fatnesse of the sacrifice, and the brest; and whanne he hath halewid bothe offrid to the Lord, he schal yyue to the preest,
Ataleta sadaka kwa mikono yake mwenyewe iliyotolewa kwa Bwana kwa moto; ataleta mafuta ya huyo mnyama pamoja na kidari, naye atainua hicho kidari mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
31 which schal brenne the ynnere fatnesse on the auter; sotheli the brest schal be Aarons and hise sones;
Kuhani atayateketeza hayo mafuta juu ya madhabahu, lakini kidari kitakuwa cha Aroni na wanawe.
32 and the riyt schuldur of the sacrifices of pesible thingis schal turne in to the firste fruytis of the preest.
Paja la kulia la sadaka zako za amani utampa kuhani kama matoleo.
33 He that of Aarons sones offrith the blood, and the ynnere fatnesse, schal haue also the riyt schuldur in his porcioun.
Mwana wa Aroni atoaye damu na mafuta ya sadaka ya amani ndiye atakayepewa paja hilo la kulia kuwa fungu lake.
34 For Y haue take fro the sones of Israel the brest of reisyng, and the schuldur of departyng, of the pesible sacrifices `of hem, and Y haue youe to Aaron the preest and to hise sones, bi euerlastynge lawe, of al the puple of Israel.
Kutoka kwenye sadaka za amani za Waisraeli, mimi Mungu nimepokea kidari kile kilichoinuliwa pamoja na lile paja lililotolewa, nami nimevitoa kwa kuhani Aroni na wanawe kuwa fungu lao la kawaida kutoka kwa Waisraeli.’”
35 This is the anoyntyng of Aaron, and of hise sones, in the cerymonyes of the Lord, in the dai where ynne Moises offride hem that thei schulden be set in preesthod,
Hii ndiyo sehemu ya sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, ambazo zilitengwa kwa ajili ya Aroni na wanawe siku ile walipowekwa wakfu ili kumtumikia Bwana katika kazi ya ukuhani.
36 and whiche thingis the Lord comaundide to be youun to hem of the sones of Israel, bi euerlastynge religioun in her generaciouns.
Siku ile walipotiwa mafuta, Bwana aliagiza kwamba Waisraeli wawape hili kama fungu lao la kawaida kwa vizazi vijavyo.
37 This is the lawe of brent sacrifice, and of sacrifice for synne, and for trespas, and for halewyng, and for the sacrifices of pesible thingis;
Basi haya ndiyo masharti kuhusu sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia, sadaka ya kuwekwa wakfu, na sadaka ya amani,
38 which lawe the Lord ordeynede to Moises in the hil of Synay, whanne he comaundide to the sones of Israel that thei schulden offre her offryngis to the Lord, in the deseert of Synay.
ambayo Bwana alimpa Mose juu ya Mlima Sinai siku ile alipowaagiza Waisraeli walete sadaka zao kwa Bwana, katika Jangwa la Sinai.

< Leviticus 7 >