< Jeremiah 28 >

1 And it was don in that yeer, in the bigynnyng of the rewme of Sedechie, kyng of Juda, in the fourthe yeer, in the fyuethe monethe, Ananye, the sone of Azur, a profete of Gabaon, seide to me in the hous of the Lord, bifor the preestis, and al the puple,
Ilitokea katika mwaka ule, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne na mwezi wa tano, Hanania mwana wa Azuri nabii, alikuwa wa Gibeoni, alisema kwangu katika nyumba ya Yahwe mbele za makuhani na watu wote. Alisema,
2 `and seide, The Lord of oostis, God of Israel, seith these thingis, Y haue al to-broke the yok of the kyng of Babiloyne.
“Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nimeivunja nira iliyowekwa na mfalme wa Babeli.
3 Yit twei yeeris of daies ben, and Y schal make to be brouyt ayen to this place alle the vessels of the Lord, whiche Nabugodonosor, kyng of Babiloyne, took fro this place, and translatide tho in to Babiloyne.
Ndani ya miaka miwili nitavirudisha katika sehemu hii vyombo vyote vya nyumba ya Yahwe ambavyo Nebukadreza mfalme wa Babeli livichukua kutoka sehemu hii na kuvisafirisha hadi Babeli.
4 And Y schal turne to this place, seith the Lord, Jeconye, the sone of Joachym, the kyng of Juda, and al the passyng ouer of Juda, that entriden in to Babiloyne; for Y schal al to-breke the yok of the kyng of Babiloyne.
Kisha nitawarudisha katika sehemu hii Yekonia mwana wa Yehotakimu, mfalme wa Yuda, na mateka wote wa Yuda ambao walipelekwa Babeli—hili ni tangazo la Yahwe—kwa maana nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.”
5 And Jeremye, the profete, seide to Ananye, the profete, bifore the iyen of preestis, and bifore the iyen of al the puple that stoden in the hous of the Lord.
Kwa hiyo Yeremia nabii akasema kwa Hanania nabii mbele ya makuhani na kwa watu wote waliosimama katika nyumba ya Yahwe.
6 And Jeremye, the profete, seide to Ananye, Amen! so do the Lord; the Lord reise thi wordis whiche thou profesiedist, that the vessels be brouyt ayen in to the hous of the Lord, and al the passyng ouer fro Babiloyne, to this place.
Yeremia nabii akasema, “Yahwe afanye hivi! Yahwe ayathibitishe maneno ambayao ulitabiri na kuvirudisha katika sehemsu hii vyombo vya nyumb a ya Yahwe, na mateka wote kutoka Babeli.
7 Netheles here thou this word, which Y speke in thin eeris, and in the eeris of al the puple.
Vile vile, sikilizeni neno ambaloo ninalitangaza katika masikio yenu na katika masikio ya watu wote.
8 Profetis that weren bifore me, and bifor thee, fro the bigynnyng, and profesieden on many londis, and on many rewmes, of batel, and of turment, and of hungur.
Manabii ambao walikuwepo mbele yangu na na mbele yenu muda mrefu uliopita pia walitabiri kuhusu mataifa mengi na juu ya falme kuu, kuhusu vita, njaa, na mapigo.
9 The profete that profesiede pees, whanne his word cometh, shal be knowun the profete whom the Lord sente in treuthe.
Kwa hiyo nabii anayetabiri kwamba kutakuwa na amani—kama neno lake litatimia, basi itajulikana kwamba yeye ni nabii kweli aliyetumwa na Yahwe.”
10 And Ananye, the profete, took the chayne fro the necke of Jeremye, the profete, and brak it.
Lakini Hanania nabii akaichukua nira kutoka kwenye shingo ya Yeremia na kuivunja.
11 And Ananye, the profete, seide in the siyt of al the puple, `and seide, The Lord seith these thingis, So Y schal breke the yok of Nabugodonosor, kyng of Babiloyne, aftir twei yeeris of daies, fro the necke of alle folkis.
Kisha Hanania akanena mbele ya watu wote na kusema, “Yahwe anasema hivi: Kama hivi tu, ndani ya miaka miwili nitaivunja nira iliyowekwa na Nebukadreza mfalme wa Babeli kutoka kwenye shingo ya kila taifa.” Kisha Yeremia nabii akaenda njia yake.
12 And Jeremye, the profete, yede in to his weie. And the word of the Lord was maad to Jeremye, aftir that Ananye, the profete, brak the chayne fro the necke of Jeremye; and the Lord seide,
Baada ya Hanania nabii kuivunja nira kutoka kwenye shingo ya Yeremia nabii, neno la Yahwe likamjia Yeremia. likisema,
13 Go thou, and seie to Ananye, The Lord seith these thingis, Thou hast al to-broke the chaynes of tre, and thou schalt make yrun chaynes for tho.
Nenda na ukaseme kwa Hanania na useme, Yahwe anasema hivi: Uliivunja nira ya mbao, lakini badala yake nitafanya nira ya chuma.'
14 For the Lord of oostis, God of Israel, seith these thingis, Y haue set an yrun yok on the necke of alle these folkis, that thei serue Nabugodonosor, the king of Babiloyne, and thei schulen serue hym; ferthermore and Y yaf to hym the beestis of erthe.
Kwa maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nimeweka nira ya chuma shingoni mwa mataifa haya yote ili wamtumikea Nebukadreza mfalme wa Babeli, na watamtumikia. Pia nimempa wanyama wa mashambani awatawale.”
15 And Jeremye, the profete, seide to Ananye, the profete, Ananye, here thou; the Lord sente not thee, and thou madist this puple for to triste in a leesyng.
Kisha nabii Yeremia akamwambia Hanania nabii, “Sikiliza Hanania! Yahwe hajakutuma, bali wewe mwenyewe umewasababisha watu hawa kuamini katika uongo.
16 Therfor the Lord seith these thingis, Lo! Y schal sende thee out fro the face of erthe; in this yeer thou schalt die, for thou spakest ayens the Lord.
Kwa hiyo Yahwe anasema hivi: Angalia, niko karibu kukutuma nje ya dunia. Mwaka huu utakufa.”
17 And Ananye, the profete, diede in that yeer, in the seuenthe monethe.
Katika mwezi wa saba wa mwaka ule ule, Hanania nabii akafa.

< Jeremiah 28 >