< Ezra 6 >

1 Thanne kyng Darius comaundide, and thei rekenyden in the biblet of bokis, that weren kept in Babiloyne.
Kisha Mfalme Dario alitoa amri, nao wakafanya uchunguzi katika kumbukumbu zilizohifadhiwa katika hazina huko Babeli.
2 And o book was foundun in Egbatanys, which is a castel in the prouynce of Medena, and sich a sentence of the kyng was writun therynne.
Karatasi moja ndefu ya maandishi ilipatikana huko Ekbatana katika jimbo la Umedi. Haya ndiyo yaliyokuwa yameandikwa humo: Kumbukumbu:
3 In the first yeer of kyng Cirus, Cirus the kyng demyde, that, `Goddis hows, which is in Jerusalem, schulde be bildid in the place where thei offren sacrifices, and that thei sette foundementis supportynge the heiythe of sixti cubitis, and the lengthe of sixti cubitis, thre ordris of stonys vnpolischid,
Katika mwaka wa kwanza wa kutawala Mfalme Koreshi, mfalme alitoa amri kuhusu Hekalu la Mungu katika Yerusalemu: Hekalu na lijengwe tena mahali palepale Wayahudi walipokuwa wakitoa dhabihu, kwenye msingi ule ule. Iwe na kimo cha mikono sitini, upana wa mikono sitini,
4 and so ordris of newe trees. Sotheli costis schulen be youun of the kyngis hows.
kuta zijengwe kwa safu tatu za mawe makubwa kisha ifuate safu moja ya mbao. Gharama zitalipwa kutoka hazina ya mfalme.
5 But also the goldun and siluerne vessels of Goddis temple, whiche Nabugodonosor took fro the temple of Jerusalem, and brouyte tho in to Babiloyne, be yoldun, and borun ayen in to the temple of Jerusalem, and in to her place, whiche also be set in the temple of God.
Pia, vyombo vya dhahabu na vya fedha vya nyumba ya Mungu, ambavyo Nebukadneza alivichukua kutoka kwenye Hekalu huko Yerusalemu akavileta Babeli, yapasa virudishwe mahali pake ndani ya Hekalu huko Yerusalemu, yapasa viwekwe ndani ya nyumba ya Mungu.
6 Now therfor Tathannai, duyk of the cuntrei which is biyende the flood, and Starbusannai, and youre counseleris, Arphasacei, that ben byyende the flood, departe ye fer fro hem;
Sasa basi, Tatenai, mtawala wa Ngʼambo ya Mto Frati na Shethar-Bozenai pamoja na ninyi, maafisa wenzao wa jimbo hilo kaeni mbali na mahali hapo.
7 and suffre ye, that thilke temple of God be maad of the duyk of Jewis, and of the eldre men of hem; and that thei bilde that hows of God in his place.
Msiingilie kazi ya Hekalu hili la Mungu. Mwacheni mtawala wa Wayahudi na viongozi Wayahudi wajenge upya nyumba hii ya Mungu mahali pake.
8 But also it is comaundid of me, that that bihoueth to be maad of tho preestis of Jewys, that the hows of God be bildid, that is, that costis be youun bisili to tho men of the arke of the kyng, that is, of tributis, that ben youun of the contrei biyende the flood, lest the werk be lettid.
Zaidi ya hayo, hapa natoa amri kuhusu mtakalofanya kwa ajili ya wazee wa Wayahudi katika ujenzi wa nyumba hii ya Mungu: Gharama za watu hawa zitalipwa kikamilifu kutoka hazina ya mfalme, kutoka kwenye mapato ya Ngʼambo ya Mto Frati, ili ujenzi usisimame.
9 That if it be nede, yyue thei bothe calues, and lambren, and kidis in to brent sacrifice to God of heuene; wheete, salt, and wyn, and oile, bi the custom of preestis that ben in Jerusalem, be youun to hem bi ech dai, that no pleynt be in ony thing.
Chochote kinachohitajika kama mafahali wachanga, kondoo dume, wana-kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Mungu wa mbinguni, ngano, chumvi, divai na mafuta kama vitakavyohitajika na makuhani huko Yerusalemu, lazima wapewe kila siku pasipo kukosa,
10 And offre thei offryngis to God of heuene; and preye thei for the lijf of the kyng and of hise sones.
ili waweze kutoa dhabihu inayompendeza Mungu wa mbinguni na kumwombea mfalme na wanawe hali njema.
11 Therfor the sentence is set of me, that if ony man chaungith this comaundement, a tre be takun of his hows, and be reisid, and be he hangid therynne; sotheli his hows be forfetid.
Zaidi ya hayo, ninaamuru kwamba mtu yeyote atakayebadilisha amri hii, boriti itangʼolewa kutoka nyumba yake, ichongwe upande mmoja na atumbuliwe nayo. Kwa ajili ya kosa hili nyumba yake ifanywe lundo la taka.
12 Forsothe God, that makith his name to dwelle there, distrie alle rewmes and puple, that holdith forth her hond to impugne and destrie thilke hows of God, which is in Jerusalem. I Darius haue demyd the sentence, which Y wole be fillid diligentli.
Naye Mungu, aliyeliweka Jina lake huko, amwangushe mfalme yeyote au watu watakaoinua mikono kubadili amri hii au kuharibu Hekalu hili lililoko Yerusalemu. Mimi Dario nimetoa amri hii. Nayo itekelezwe kwa bidii na kwa makini.
13 Therfor Tathannai, duyk of the `cuntrei biyende the flood, and Starbusannai, and hise counseleris, diden execucioun, `ether filliden, so diligentli, bi that that kyng Darius hadde comaundid.
Kwa sababu ya amri aliyotoa Mfalme Dario, Tatenai mtawala wa Ngʼambo ya Mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao wakaitekeleza kwa bidii na kwa makini.
14 Sotheli the eldre men of Jewis bildiden, and hadden prosperite, bi the profesie of Aggey, the profete, and of Zacarie, the sone of Ado; and thei bildiden, and maden, for God of Israel comaundide, and for Cirus, and Darius, and Artaxerses, kyngis of Persis, comaundiden;
Hivyo wazee wa Wayahudi waliendelea kujenga na kustawi kutokana na mahubiri ya manabii Hagai na Zekaria, mwana wa Ido. Wakakamilisha ujenzi wa Hekalu kulingana na agizo la Mungu wa Israeli na amri ya Koreshi, Dario na Artashasta wafalme wa Uajemi.
15 and thei performyden this hows of God `til to the thridde dai of the monethe Adar, which is the sixte yeer of the rewme of king Darius.
Hekalu lilikamilika siku ya kumi na mbili ya mwezi wa Adari, ndio mwezi wa tatu, katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Dario.
16 Forsothe the sones of Israel, the preestis and dekenes, and the othere of the sones of transmygracioun, `that is, that camen fro transmigracioun, `ether caitifte, maden the halewyng of Goddis hows in ioie;
Kisha watu wa Israeli: makuhani, Walawi na wengine wote waliohamishwa, wakaadhimisha kule kuwekwa wakfu nyumba ya Mungu kwa shangwe.
17 and offriden, `in the halewyng of Goddis hows, an hundrid caluys, twei hundryd wetheris, foure hundrid lambren, twelue buckis of geet for the synne of al Israel, bi the noumbre of lynagis of Israel.
Kwa ajili ya kuwekwa wakfu nyumba hii ya Mungu walitoa mafahali mia moja, kondoo dume mia mbili, wana-kondoo mia nne, sadaka kwa ajili ya dhambi ya Israeli yote walitoa mbuzi dume kumi na wawili, mmoja kwa ajili ya kila kabila la Israeli.
18 And thei ordeyneden preestis in her ordris, and dekenes in her whilis, on the werkis of God in Jerusalem, as it is writun in the book of Moises.
Wakawaweka makuhani katika nafasi zao na Walawi wakawekwa katika makundi yao ya huduma kwa Mungu huko Yerusalemu, kulingana na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose.
19 Forsothe the sones of transmygracioun maden pask, in the fourtenthe dai of the firste monethe.
Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, waliorudi kutoka uhamishoni wakaadhimisha Pasaka.
20 For the preestis and dekenes as o man weren clensid, alle weren clene for to offre pask to alle the sones of transmygracioun, and to her britheren preestis, and to hem silf.
Makuhani na Walawi walikuwa wamekwisha kujitakasa nao wamekuwa safi kwa kufuata kawaida za ibada. Walawi wakachinja kondoo wa Pasaka kwa ajili ya wana wa waliorudi kutoka utumwani uhamishoni, kwa ajili ya ndugu zao makuhani na wao wenyewe.
21 And the sones of Israel eeten, that turneden ayen fro transmygracioun, and ech man eet, that hadde departid hym silf fro al the defoulyng of hethene men of the lond, for to seke the Lord God of Israel.
Hivyo Waisraeli waliokuwa wamerudi kutoka utumwani uhamishoni wakaila Pasaka, pamoja na wale waliokuwa wamejitenga na matendo ya unajisi wa Mataifa ya jirani ili kumtafuta Bwana, Mungu wa Israeli.
22 And thei maden solempnyte of therf looues seuene daies in gladnesse; for the Lord hadde maad hem glad, and hadde turned the herte of the kyng of Assur to hem, that he wolde helpe `her hondis in the werk of the hows of the Lord God of Israel.
Kwa muda wa siku saba waliiadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa furaha, kwa sababu Bwana alikuwa amewajaza furaha kwa kubadilisha nia ya mfalme wa Ashuru kwamba awasaidie ujenzi wa nyumba ya Mungu, Mungu wa Israeli.

< Ezra 6 >