< Ezra 1 >

1 In the firste yeer of Cirus, kyng of Persis, that the word of the Lord bi the mouth of Jeremye schulde be fillid, the Lord reiside the spirit of Cyrus, kyng of Persis; and he pupplischide a vois in al his rewme, ye, bi the scripture, and seide, Cirus,
Katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, Yahwe akatimiza neno lake ambalo Yeremia alisema, na kuinua roho ya Koreshi. Sauti ya Koreshi ikasambaa na kusikika katika ufalme wake. Hiki ndicho kilichoandikwa na kusemwa:
2 the kyng of Persis, seith these thingis, The Lord God of heuene yaf to me alle the rewmes of erthe, and he comaundide to me, that Y schulde bilde to hym an hows in Jerusalem, which is in Judee.
“Koreshi, mfalme wa Uajemi, anasema: Yahwe, Mungu wa mbinguni, amenipa mimi ufalme wote wa dunia, na ameniteua mimi kumjengea yeye nyumba katika Yerusalem ya Yuda.
3 Who is among you of al his puple? his God be with hym; stie he in to Jerusalem, which is in Judee, and bilde he the hows of the Lord God of Israel; he is God, which is in Jerusalem.
Yeyote katika watu wake (Mungu awe pamoja naye) anaweza kwenda Yerusalem na kujenga nyumba kwa ajili ya Yahwe, Mungu wa Israel, Mungu ambaye yuko Yerusalem.
4 And alle othere men, `that dwellen where euere in alle places, helpe hym; the men of her place helpe in siluer, and gold, and catel, and scheep, outakun that that thei offren wilfulli to the temple of God, which is in Jerusalem.
Watu wa kila sehemu katika ufalme waliosalia katika nchi na kuishi wanapaswa kuwapa wao fedha na dhahabu, mali na wanyama, pamoja na kutoa kwa hiari kwenye nyumba ya Mungu Yerusalem.”
5 And the princis of fadris of Juda and of Beniamyn risiden, and the preestis, and dekenes, and ech man whos spirit God reiside, for to stie to bilde the temple of the Lord, that was in Jerusalem.
Ndipo wakuu wa jamii ya Yuda na Benjamini, makuhani na walawi, na kila mmoja ambaye Roho wa Mungu alimwinua kuondoka na kujenga nyumba yake alisimama.
6 And alle men that weren `in cumpas helpiden the hondis of hem, in vesselis of siluer, and of gold, `in catel, in purtenaunce of houshold, and in alle werk beestis, outakun these thingis which thei offriden bi fre wille.
Wale waliowazunguka karibu waliwasaidia kwa kuwapa fedha na vitu vya dhahabu, mali, wanyama, vitu vya thamani, na kutoa kwa hiari.
7 Forsothe kyng Cyrus brouyte forth the vessels of the temple of the Lord, whiche Nabugodonosor hadde take fro Jerusalem, and hadde set tho in the temple of his god.
Mfalme Koreshi akarusu vitu ambavyo vilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe, ambavyo Nebukadreza alitoa kutoka Yerusalem na kuviweka katika nyumba ya miungu yake.
8 Sotheli Cyrus, the kyng of Persis, brouyte forth tho bi the hond of Mytridatis, sone of Gazabar; and noumbride tho to Sasabazar, the prince of Juda.
Koreshi akavikabidhi kwenye mikono ya Mithredathi mtunza fedha, ambaye akavitoa na kuhesabu kwa Sheshbaza, kiongozi wa Yuda
9 And this is the noumbre of tho vessels; goldun violis, thritti; siluerne viols, a thousynde; `grete knyues, nyne and twenti; goldun cuppis, thritti; siluerne cuppis,
Hii ilikuwa idadi yake: beseni thelathini za dhahabu, beseni elfu moja za fedha, beseni zingine ishirini na tisa,
10 two thousynde foure hundrid and ten; othere vessels, a thousynde;
mabakuli thelathini ya dhahabu, mabakuli madogo ya fedha 410, na vitu elfu moja vya kuongezea.
11 alle the vessels of gold and siluere weren fyue thousynde foure hundrid. Sasabazar took alle vessels, with hem that stieden fro the transmygracioun of Babiloyne, in to Jerusalem.
Kulikuwa na vitu 5, 400 vya fedha na dhahabu. Sheshbaza akavileta vyote wakati wa uhamisho kutoka Babeli kwenda Yerusalem.

< Ezra 1 >