< Deuteronomy 6 >

1 These ben the comaundementis, and cerymonyes, and domes, whiche youre Lord God comaundide that Y schulde teche you, and that ye do tho in the lond to which ye passen ouer to welde;
Haya ndiyo maagizo, amri na sheria ambazo Bwana Mungu wenu aliniagiza niwafundishe ninyi ili mpate kuyashika katika nchi ambayo ninyi mnavuka Yordani kuimiliki,
2 that thou drede thi Lord God, and kepe alle hise comaundementis, and heestis, whiche Y comaunde to thee, and to thi sones, and sones of sones, in alle the daies of thi lijf, that thi daies be lengthid.
ili kwamba ninyi, watoto wenu na watoto wao baada yao wamche Bwana Mungu wenu siku zote kwa kushika amri na maagizo yake yote ninayowapa, ili mweze kuyafurahia maisha marefu.
3 Thou Israel, here, and kepe, that thou do tho thingis whiche the Lord comaundide to thee, and that it be wel to thee, and thou be multiplied more, as the Lord God of thi fadris bihiyte, to yyue to thee a lond flowynge with mylk and hony.
Sikia, ee Israeli, nawe uwe mwangalifu kutii ili upate kufanikiwa na kuongezeka sana katika nchi itiririkayo maziwa na asali, kama Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaahidi ninyi.
4 Thou Israel, here, thi Lord God is o God.
Sikia, ee Israeli: Bwana Mungu wako, Bwana ni mmoja.
5 Thou schalt loue thi Lord God of al thin herte, and of al thi soule, and of al thi strengthe.
Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote.
6 And these wordis whiche Y comaunde to thee to dai, schulen be in thin herte;
Amri hizi ninazokupa leo zitakuwa katika moyo wako.
7 and thou schalt telle tho to thi sones, and thou schalt thenke on tho, sittynge in thin hows, and goynge in the weie, slepynge, and rysinge.
Wafundishe watoto wako kwa bidii. Nena kuhusu amri hizi uketipo nyumbani na wakati utembeapo njiani, ulalapo na uamkapo.
8 And thou schalt bynde tho as a signe in thin hond; and tho schulen be, and schulen be moued bifor thin iyen; and thou schalt write tho in the lyntel,
Zifunge kama alama juu ya mkono wako, na uzifunge juu ya paji la uso wako.
9 and in the doris of thin hows.
Ziandike kwenye miimo ya milango ya nyumba yako na juu ya malango yako.
10 And whanne thi Lord God hath brouyt thee in to the lond, for which he swoor to thi fadris, to Abraham, Isaac, and Jacob, and hath youe to thee grete citees, and beeste, whiche thou bildidist not,
Wakati Bwana Mungu wako atakapokuleta katika nchi aliyowaapia baba zako, Abrahamu, Isaki na Yakobo, kukupa wewe, nchi kubwa, ina miji inayopendeza ambayo hukuijenga,
11 housis fulle of alle richessis, whiche thou madist not, and cisternes, which thou diggedist not, `places of vynes, and `places of olyues, whiche thou plauntidist not,
nyumba zilizojaa vitu vizuri vya aina nyingi ambavyo hukuvijaza, visima ambavyo hukuchimba, na mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hukupanda wewe, basi, utakapokula na kushiba,
12 and thou hast ete, and art fillid,
jihadhari usije ukamwacha Bwana, aliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
13 be war diligentli, lest thou foryete the Lord, that ladde thee out of the lond of Egipt, fro the hows of seruage. Thou schalt drede thi Lord God, and thou schalt serue hym aloone, `bi seruyce due to God onely, and thou schalt swere bi his name.
Utamcha Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake na kuapa kwa jina lake.
14 Ye schulen not go aftir alien goddis, of alle hethen men that ben `in youre cumpas;
Usifuate miungu mingine, miungu ya mataifa yanayokuzunguka;
15 for God is a feruent louyere, thi Lord God is in the myddis of thee, lest ony tyme the `strong veniaunce of thi Lord God be wrooth ayens thee, and do awei thee fro `the face of the erthe.
kwa kuwa Bwana Mungu wako, ambaye yuko katikati yako, ni Mungu mwenye wivu na hasira yake itawaka dhidi yako, naye atakuangamiza kutoka uso wa nchi.
16 Thou schalt not tempte thi Lord God, as thou temptidist in the place of temptyng.
Usimjaribu Bwana Mungu wako kama ulivyofanya huko Masa.
17 Kepe thou the comaundementis of thi Lord God, and the witnessyngis, and cerymonyes, whiche he comaundide to thee;
Utayashika maagizo ya Bwana Mungu wako kwa bidii, na masharti na amri alizokupa.
18 and do thou that that is plesaunt and good in the siyt of the Lord, that it be wel to thee, and that thou entre, and welde the beste lond, of which the Lord swoor to thi fadris,
Fanya lililo haki na jema mbele za Bwana, ili upate kufanikiwa, uweze kuingia na kuimiliki nchi nzuri ambayo Bwana aliahidi kwa kiapo kwa baba zako,
19 that he schulde do awey alle thin enemyes bifor thee, as he spak.
kuwafukuza kwa nguvu adui zako mbele yako kama Bwana alivyosema.
20 And whanne thi sone schal axe thee to morewe, that is, in tyme comyng, and schal seie, What wolen these witnessyngis, and cerymonyes, and domes to hem silf, whiche oure Lord God comaundide to vs?
Siku zijazo, mtoto wako atakapokuuliza, “Ni nini maana ya masharti haya, amri na sheria hizi ambazo Bwana Mungu wako alikuagiza wewe?”
21 thou schalt seie to hym, We weren `seruauntis of Farao in Egipt, and the Lord ledde vs out of Egipt, in strong hond;
Mwambie: “Tulikuwa watumwa wa Farao huko Misri, lakini Bwana alitutoa sisi kutoka Misri kwa mkono wenye nguvu.
22 and he dide myraclis, and grete wondris, and werste, `that is, moost peyneful veniaunces, in Egipt, ayens Farao and al his hows, in oure siyt.
Bwana akapeleka mbele yetu ishara za miujiza na maajabu makubwa na ya kutisha mno juu ya Misri na Farao pamoja na nyumba yake yote.
23 And he ledde vs out therof, that he schulde yyue to vs led yn, the lond of which he swoor to oure fadris.
Lakini Mungu akatutoa huko, akatuleta na kutupa nchi hii ambayo aliwaahidi baba zetu kwa kiapo.
24 And the Lord comaundide to vs, that we do alle these lawful thingis, and drede oure Lord God, that it be wel to vs in alle the daies of oure lijf, as it is to dai.
Bwana akatuagiza tutii amri hizi zote na kumcha Bwana Mungu wetu, ili tupate kustawi na kuendelea kuwa hai kama ilivyo leo.
25 And he schal be merciful to vs, if we schulen do and kepe alle hise heestis, bifor oure Lord God, as he comaundide to vs.
Kama tukizitii kwa bidii amri hizi zote mbele za Bwana Mungu wetu, kama alivyotuamuru sisi, hiyo itakuwa haki yetu.”

< Deuteronomy 6 >