< 2 Peter 3 >

1 Lo! ye moost dereworth britheren, Y write to you this secounde epistle, in which Y stire youre clere soule bi monesting togidere,
Wapenzi, huu ndio waraka wangu wa pili ninaowaandikia. Katika nyaraka hizi mbili ninajaribu kuziamsha nia zenu safi kwa mawazo makamilifu.
2 that ye be myndeful of tho wordis, that Y biforseide of the hooli prophetis, and of the maundementis of the hooli apostlis of the Lord and sauyour.
Nataka ninyi mkumbuke maneno yaliyosemwa zamani na manabii watakatifu na ile amri ya Bwana na Mwokozi mliyopewa kupitia kwa mitume wenu.
3 First wite ye this thing, that in the laste daies disseyueris schulen come in disseit, goynge aftir her owne coueityngis,
Kwanza kabisa, ni lazima mfahamu ya kwamba siku za mwisho watakuja watu wenye dhihaka, wakidhihaki na kuzifuata tamaa zao mbaya.
4 seiynge, Where is the biheest, or the comyng of hym? for sithen the fadris dieden, alle thingis lasten fro the bigynnyng of creature.
Watasema, “Iko wapi ile ahadi ya kuja kwake? Tangu baba zetu walipofariki, kila kitu kinaendelea kama kilivyokuwa tangu mwanzo wa kuumbwa.”
5 But it is hid fro hem willynge this thing, that heuenes were bifore, and the erthe of water was stondynge bi watir, of Goddis word;
Lakini wao kwa makusudi hupuuza ukweli huu, ya kwamba kwa neno la Mungu mbingu zilikuwepo tangu zamani, nayo dunia ilifanyizwa kutoka ndani ya maji na kwa maji.
6 bi which that ilke world clensid, thanne bi watir perischide.
Ulimwengu wa wakati ule uligharikishwa kwa hayo maji na kuangamizwa.
7 But the heuenes that now ben, and the erthe, ben kept bi the same word, and ben reseruyd to fier in to the dai of doom and perdicioun of wickid men.
Lakini kwa neno lilo hilo, mbingu za sasa na dunia zimewekwa akiba kwa ajili ya moto, zikihifadhiwa hadi siku ile ya hukumu na ya kuangamizwa kwa watu wasiomcha Mungu.
8 But, ye moost dere, this o thing be not hid to you, that o dai anentis God is as a thousynde yeeris, and a thousynde yeeris ben as o dai.
Lakini wapenzi, msisahau neno hili: kwamba kwa Bwana, siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.
9 The Lord tarieth not his biheest, as summe gessen, but he doith pacientli for you, and wole not that ony men perische, but that alle turne ayen to penaunce.
Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama watu wengine wanavyokudhani kukawia. Badala yake, yeye anawavumilia ninyi, maana hataki mtu yeyote aangamie, bali kila mtu afikilie toba.
10 For the dai of the Lord schal come as a theef, in which heuenes with greet bire schulen passe, and elementis schulen be dissoluyd bi heete, and the erthe, and alle the werkis that ben in it, schulen be brent.
Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwizi. Ndipo mbingu zitatoweka kwa kishindo kikuu; navyo vitu vya asili vitateketezwa kwa moto, nayo dunia na kila kitu kilichomo ndani yake kitaunguzwa.
11 Therfor whanne alle these thingis schulen be dissolued, what manner men bihoueth it you to be in hooli lyuyngis and pitees,
Kwa kuwa vitu vyote vitaharibiwa namna hii, je, ninyi imewapasa kuwa watu wa namna gani? Inawapasa kuishi maisha matakatifu na ya kumcha Mungu,
12 abidinge and hiyynge in to the comyng of the dai of oure Lord Jhesu Crist, bi whom heuenes brennynge schulen be dissoluyd, and elementis schulen faile bi brennyng of fier.
mkingojea na kuhimiza kuja kwa hiyo siku ya Mungu. Siku hiyo italeta mbingu kuchomwa moto na kutoweka, na vitu vya asili vitayeyuka kwa moto.
13 Also we abiden bi hise biheestis newe heuenes and newe erthe, in which riytwisnesse dwellith.
Lakini kufuatana na ahadi yake, sisi tunatazamia mbingu mpya na dunia mpya, ambayo haki hukaa ndani yake.
14 For which thing, ye moost dere, abidynge these thingis, be ye bisye to be foundun to hym in pees vnspottid and vndefoulid.
Kwa sababu hii, wapenzi, kwa kuwa mnatazamia mambo haya, fanyeni bidii ili awakute katika amani, bila mawaa wala dosari.
15 And deme ye long abiding of oure Lord Jhesu Crist youre heelthe, as also oure moost dere brother Poul wroot to you, bi wisdom youun to hym.
Hesabuni uvumilivu wa Bwana kuwa ni wokovu, kama vile ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima ile aliyopewa na Mungu.
16 As and in alle epistlis he spekith `in hem of these thingis; in which ben summe hard thingis to vndurstonde, whiche vnwise and vnstable men deprauen, as also thei don othere scripturis, to her owne perdicioun.
Huandika vivyo hivyo katika nyaraka zake zote, akizungumzia ndani yake mambo haya. Katika nyaraka zake kuna mambo mengine ambayo ni vigumu kuyaelewa, ambayo watu wajinga na wasio thabiti huyapotosha kwa maangamizi yao wenyewe, kama wapotoshavyo pia Maandiko mengine.
17 Therfor ye, britheren, bifor witynge kepe you silf, lest ye be disseyued bi errour of vnwise men, and falle awei fro youre owne sadnesse.
Basi, ninyi wapenzi, kwa kuwa mmekwisha kujua mambo haya, jilindeni msije mkachukuliwa na kosa la watu hao waasi na kuanguka kutoka kwenye uthabiti wenu.
18 But wexe ye in the grace and the knowyng of oure Lord Jhesu Crist and oure Sauyour; to hym be glorie now and in to the dai of euerlastyngnesse. Amen. (aiōn g165)
Bali kueni katika neema na katika kumjua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. Utukufu una yeye sasa na milele! Amen. (aiōn g165)

< 2 Peter 3 >

The World is Destroyed by Water
The World is Destroyed by Water