< 2 Chronicles 1 >

1 Therfor Salomon, the sone of Dauid, was coumfortid in his rewme, and the Lord was with hym, and magnefiede hym an hiy.
Solomoni mwana wa Daudi alijiimarisha kwenye milango yote! Katika ufalme wake, kwa kuwa Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye, naye akamfanya mkuu mno.
2 And Salomon comaundide to al Israel, to tribunes, and centuriouns, and to duykis, and domesmen of al Israel, and to the princes of meynees;
Ndipo Solomoni akasema na Israeli wote, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, waamuzi na viongozi wote katika Israeli, pamoja na wakuu wa jamaa.
3 and he yede with al the multitude in to the hiy place of Gabaon, where the tabernacle of boond of pees of the Lord was, which tabernacle Moyses, the seruaunt of the Lord, made in wildirnesse.
Naye Solomoni na kusanyiko lote wakakwea mpaka mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni, kwa kuwa huko ndiko Hema la Kukutania la Mungu lilipokuwa, ambalo Mose mtumishi wa Bwana alikuwa amelitengeneza huko jangwani.
4 Forsothe Dauid hadde brouyt the arke of God fro Cariathiarym in to the place which he hadde maad redy to it, and where he hadde set a tabernacle to it, that is, in to Jerusalem.
Basi Daudi alikuwa amelipandisha Sanduku la Mungu kutoka Kiriath-Yearimu mpaka mahali alipokuwa amepatengeneza kwa ajili yake, kwa sababu alikuwa amesimamisha hema kwa ajili ya hilo Sanduku huko Yerusalemu.
5 And the brasun auter, which Beseleel, the sone of Vri, sone of Vr, hadde maad, was there bifor the tabernacle of the Lord; whiche also Salomon and al the chirche souyte.
Lakini yale madhabahu ya shaba ambayo Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, alikuwa ametengeneza yalikuwa huko Gibeoni mbele ya Maskani ya Bwana Mungu, hivyo Solomoni na kusanyiko lote walimtafuta Mungu huko.
6 And Salomon stiede to the brasun autir, bifor the tabernacle of boond of pees of the Lord, and offride in it a thousynde sacrifices.
Solomoni akapanda huko yalikokuwa madhabahu ya shaba mbele za Bwana katika Hema la Kukutania, na kutoa dhabihu 1,000 za sadaka za kuteketezwa juu yake.
7 Lo! `forsothe in that nyyt God apperide to hym, `and seide, Axe that that thou wolt, that Y yyue to thee.
Usiku ule Mungu akamtokea Solomoni na kumwambia, “Omba lolote utakalo nikupe.”
8 And Salomon seide to God, Thou hast do greet mersi with Dauid, my fadir, and hast ordeyned me kyng for hym.
Solomoni akamjibu Mungu, “Umemwonyesha baba yangu Daudi fadhili nyingi, nawe umeniweka niwe mfalme mahali pake.
9 Now therfor, Lord God, thi word be fillid, which thou bihiytist to Dauid, my fadir; for thou hast maad me kyng on thi greet puple, which is so vnnoumbrable as the dust of erthe.
Sasa, Bwana Mungu, ahadi yako kwa baba yangu Daudi na ithibitike, kwa kuwa umenifanya mimi mfalme juu ya watu ambao ni wengi kama mavumbi ya nchi.
10 Yiue thou to me wisdom and vndurstondyng, that Y go in and go out bifor thi puple; for who may deme worthili this thi puple, which is so greet?
Nakuomba unipe mimi hekima na maarifa, ili niweze kuongoza watu hawa, kwa kuwa ni nani awezaye kutawala hawa watu wako walio wengi hivi?”
11 Sotheli God seide to Salomon, For this thing pleside more thin herte, and thou axidist not richessis, and catel, and glorie, nether the lyues of them that hatiden thee, but nether ful many daies of lijf; but thou axidist wisdom and kunnyng, that thou maist deme my puple, on which Y ordeynede thee kyng,
Mungu akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa jambo hili ndilo shauku ya moyo wako na hukuomba mali, utajiri au heshima, wala kifo kwa ajili ya adui zako, nawe kwa kuwa hukuomba maisha marefu, bali umeomba hekima na maarifa ili kuongoza watu wangu ambao nimekufanya uwe mfalme juu yao,
12 wisdom and kunnyng ben youun to thee; forsothe Y schal yyue to thee richessis, and catel, and glorie, so that noon among kyngis, nether bifor thee nethir aftir thee, be lijk thee.
kwa hiyo utapewa hekima na maarifa. Tena nitakupa pia mali, utajiri na heshima, ambavyo hakuna mfalme yeyote aliyekuwepo kabla yako amewahi kuwa navyo, na hakuna yeyote baada yako atakayekuwa navyo.”
13 Therfor Salomon cam fro the hiy place of Gabaon in to Jerusalem, bifor the tabernacle of boond of pees, and he regnede on Israel.
Ndipo Solomoni akaenda mpaka Yerusalemu kutoka mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni, kutoka mbele ya Hema la Kukutania. Naye akatawala Israeli.
14 And he gaderide to hym chaaris and knyytis, and a thousynde and foure hundrid charis weren maad to hym, and twelue thousynde of knyytis; and he made hem to be in the citees of cartis, and with the kyng in Jerusalem.
Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu.
15 And the kyng yaf in Jerusalem gold and siluer as stoonys, and cedris as sicomoris, that comen forth in feeldi places in greet multitude.
Mfalme akafanya fedha na dhahabu kuwa vitu vya kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
16 Forsothe horsis weren brouyt to hym fro Egipt, and fro Choa, bi the marchauntis of the kyng, whiche yeden, and bouyten bi prijs,
Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue.
17 `a foure `horsid carte for sixe hundrid platis of siluer, and an hors for an hundrid and fifti. In lijk maner biyng was maad of alle the rewmes of citees, and of the kingis of Sirie.
Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 600 za fedha, na farasi kwa shekeli 150. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.

< 2 Chronicles 1 >