< 2 Chronicles 28 >

1 Achaz was of twenti yeer, whanne he bigan to regne, and he regnede sixtene yeer in Jerusalem; he dide not riytfulnesse in the siyt of the Lord, as Dauid, his fadir, dide;
Ahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, na akatawala miaka kumi na sita katika Yerusalemu. Hakufanya yaliyoadili katika macho ya Yahwe, kama Daudi babu yake alivyokuwa amefanya.
2 but he yede in the weies of the kyngis of Israel. Ferthermore and he yetyde ymagis to Baalym.
Badala yake, alitembea katika njia za wafalme wa Israeli; pia alitengeneza sanamu za kusubu kwa ajila ya Mabaali.
3 He it is that brente encense in the valey of Beennon, and purgide hise sones bi fier bi the custom of hethene men, whiche the Lord killide in the comyng of the sones of Israel.
Zaidi ya hayo, akafukiza uvumba katika bonde la Beni Hinomu na akawaweka watoto wake ndani ya moto, kwa mjibu wa desturi za uzinzi za watu ambao Yahwe aliwafukuza nje ya nchi zao mbele za watu wa Israeli.
4 Also he made sacrifice, and brente encense in hiy places, and in hillis, and vndur ech tree ful of bowis.
Akatoa sadaka na kufukiza uvumba katika sehemu za juu na juu ya vilima na chini ya kila mti wenye majani mabichi.
5 And `his Lord God bitook hym in the hond of the kyng of Sirie, which smoot Achaz, and took a greet preie of his empire, and brouyten in to Damask. Also Achaz was bitakun to the hondis of the kyng of Israel, and was smytun with a greet wounde.
Kwa hiyo Yahwe Mungu wa Ahazi, akamweka katika mikono ya mfalme wa Shamu. Waaramu wakamshinda na kuchukua kutoka kwake kundi kubwa la mateka, wakawapeleka Damesiki. Ahazi pia aliwekwa katika mikono ya mfalme wa Israeli ambaye alimshinda kwa mauji makuu.
6 And Facee, the sone of Romelie, killide of Juda sixe scoore thousynde in o dai, alle the men werriours; for thei hadden forsake the Lord God of her fadris.
Kwa maana Peka mwana wa Remalia, aliwaua katika Yuda wanajeshi 120, 00 kwa siku moja, wote walikuwa wanaume hodari, kwa maana walikuwa wamemsahau Yahwe, Mungu wa babu zao.
7 In the same tyme Zechry, a myyti man of Effraym, killide Maasie, the sone of Rogloth, the kyng; and `he killide Ezrica, the duyk of his hows, and Elcana, the secounde fro the kyng.
Zikri, mtu mwenye nguvu kutoka Efraimu, akawaua Maaseya mwana wa mfalme, Azrikamu, mwangalizi mkuu wa ikulu, na Elkana, ambaye alikuwa karibu na mfalme.
8 And the sones of Israel token of her britheren two hundrid thousynde of wymmen and of children and of damysels, and prey with out noumbre; and baren it in to Samarie.
Jeshsi la Israeli likachukua mateka kutoka kwa ndugu zao 200, 000 wake, wana, na mabinti. Pia wakachukua nyara nyingi, ambazo walipeleka Samaria.
9 In that tempest a profete of the Lord, Obed bi name, was there, which yede out ayens the oost comynge in to Samarie, and seide to hem, Lo! the Lord God of youre fadris was wrooth ayens Juda, and bitook hem in youre hondis; and ye han slayn hem crueli, so that youre cruelte stretchide forth in to heuene.
Lakini nabii wa Yahwe alikuwapo huko, jina lake aliitwa Odedi. Alikwenda nje kukutana na jeshi likiingia Samaria. Akawaambia, “Kwa sababu Yahwe, Mungu wa babu zenu, alikuwa na hasiri na Yuda, akawatia katika mikono yenu. Lakini mmewaua katika hasira inayofika juu mbinguni.
10 Ferthermore ye wolen make suget to you the sones of Juda and of Jerusalem in to seruauntis and handmaidis; which thing is not nedeful to be doon; for ye han synned on this thing to `youre Lord God.
Sasa ninyi badala ya kuwahifadhi wanaume na wanawake wa Yuda na Yerusalemu kama watumwa wenu. Lakini je hamko na hatia ya dhambi zenu zidi ya Yahwe Mungu wenu?
11 But here ye my councel, and lede ayen the prisounneris, whyche ye han brouyt of youre britheren; for greet veniaunce of the Lord neiyith to you.
Sasa basi, nisikilizeni: warudisheni wafubgwa, ambao mmewachukua wa ndugu zenu, kwa maana ghadhabu ya Yahwe iko juu yenu.”
12 Therfor men of the princes of the sones of Effraym, Azarie, the sone of Johannan, Barachie, the sone of Mosollamoth, Jesechie, the sone of Sellum, and Amasie, the sone of Adali, stoden ayens hem that camen fro the batel;
Kisha baadhi ya viongozi wa watu wa Efraimu—Azaria mwana wa Yohanani, Berekia mwana wa Meshiremothi, na Yehizikia mwana wa Shalumu, na Amasa mwana wa Hadlai, wakasimama kinyume na wale waliorudi kutoka vitani.
13 and seiden to hem, Ye schulen not brynge in hidur the prisoneris, lest we doen synne ayens the Lord; whi wolen ye `ley to on youre synnes, and heepe elde trespassis? For it is greet synne; the ire of the strong veniaunce of the Lord neiyeth on Israel.
Wakasema kwao, “Lazimaa msiwaleta wafungwa hapa, kwa kuwa mlikusudia jambo ambalo litaleta juu yetu dhambi dhidi ya Yahwe, kuongeza dhambi juu yetu na makosa yetu, kwa maana makosa yetu ni makuu, na kuna hasira kali dhidi ya Israeli.”
14 And the men werriouris leften the prey, and alle thingis whiche thei hadden take, bifor the princes and al the multitude.
Hivyo watu wenye silaha wakawaacha wafungwa na mateka mbele ya viongozi wa Israeli na kusanyiko lote
15 And the men stoden, whiche we remembriden bifore, and thei token the prisounneris, and clothiden of the spuylis alle that weren nakid; and whanne thei hadden clothid hem, and hadden schod, and hadden refreschid with mete and drynke, and hadden anoyntid for trauel, and hadden youe cure, `ether medecyn, to hem; `thei puttiden hem on horsis, whiche euere `myyten not go, and weren feble `of bodi, and brouyten to Jerico, a citee of palmes, to `the britheren of hem; and thei turneden ayen in to Samarie.
Watu ambao walipangwa kwa majina wakanyanyuka na kuwachukua wafungwa, na kuwavika wote waliokuwa uchi miongoni mwa mateka. Wakawavika na kuwapa viatu. Wakawapa chakula wale na kunywa. Wakawahudumia majeraha yao na kuwaweka waliodhaifu juu ya punda. Wakawarudisha kwenye familia zao katika Yeriko, (Ulioitwa mji wa mitende). Kisha wakarudi Samaria.
16 In that tyme kyng Achaz sente to the kyng of Assiriens, and axide help.
Wakati huo Mfalme Ahazi akatuma wajumbe kwa wafalme wa Ashuru kuwaomba wamsaidie.
17 And Ydumeis camen, and killiden many men of Juda, and token greet prey.
Kwa maana Waedomu walikuwa wamekuja tena na kuvamia Yuda, wakachukua wafungwa.
18 Also Filisteis weren spred abrood bi citees of the feeldis, and at the south of Juda; and thei token Bethsames, and Hailon, and Gaderoth, and Socoth, and Thannan, and Zamro, with her villagis; and dwelliden in tho.
Wafilisti pia wakavamia miji ya nchi ya chini na ya Negebu ya Yuda. Waliichukua Beth-shemeshi, Ayaloni, Giderothi, SoKo pamoja na vijiji vyake, Timna pamoja na vijiji vyake. Wakaenda kuishi katika sehemu hizo.
19 For the Lord made low Juda for Achaz, the kyng of Juda; for he hadde maad him nakid of help, and hadde dispisid the Lord.
Kwa kuwa Yahwe aliishusha chini Yuda kwa sababu ya Ahazi, mfalme wa Israeli; kwa maana alikuwa ametenda maovu katika Yuda na alikuwa ametenda dhambi nzito sana dhidi ya Yahwe.
20 And the Lord brouyte ayens him Teglat Phalasar, kyng of Assiriens, that turmentide hym, and waastide hym, while no man ayenstood.
Tiglath-pileseri, mfalme wa Ashuru, akaja kwake na akampa tabu badala ya kumpa nguvu.
21 Therfor Achaz, after that he hadde spuylid the hows of the Lord, and the hows of the kyng and of princes, yaf yiftis to the kyng of Assiriens, and netheles it profitide `no thing to hym.
Kwa kuwa Ahazi aliteka nyara nyumba ya Yahwe na nyumba ya mfalme na viongozi, kwa ajili ya kuvitoa vitu vya thamani kwa mfalme wa Ashuru. Lakini kufanya hivyo hakukumfaidisha yeye.
22 Ferthermore also in the tyme of his angwisch he encreesside dispit ayens God; thilke kyng Achaz bi
Mfalme Ahazi huyu huyu akatenda dhambi hata zaidi dhidi ya Yahwe katika muda wa mateso yake.
23 hym silf offride sacrifices to the goddis of Damask, hise smyteris, and seide, The goddis of the kyngis of Sirie helpen hem, whiche goddis Y schal plese bi sacrifices, and thei schulen help me; whanne ayenward thei weren fallyng to hym, and to al Israel.
Kwa maana aliwatolea dhabihu mingu wa Dameski, miungu ambao walimshinda. Akasema, “Kwa sababu miungu wa mfalme wa Aramu waliwasaidia, nitawatolea sadaka ili wanisaidie.” Lakini walikuwa watesi wake na Israeli yote.
24 Therfor aftir that Achaz hadde take awei, and broke alle the vessels of the hows of God, he closide the yatis of Goddis temple, and made auteris to hym silf in alle the corneris of Jerusalem.
Ahazi akazikusanya pamoja samani za nyumba ya Mungu na kuzikata vipande vipande. Akaifunga milango ya nyumba ya Yahwe na kuzitengeneza madhabahu kwa ajili yake mwenyewe katika kila kona ya Yerusalemu.
25 And in alle citees of Juda he bildide auteris to brenne encence, and he stiride the Lord God of hise fadris to wrathfulnesse.
Katika kila mji wa Yuda akafanya sehemu za juu kwa ajili ya kutolea sadaka za kuteketezwa kwa miungu wengine. Akamfanya Yahwe, Mungu wa babu zake, akasirike.
26 Sotheli the residue of hise wordis and of alle hise werkis, the formere and the laste, ben writun in the book of kyngis of Juda and of Israel.
Sasa matendo yake yaliyobaki, na njia zake zote, mwanzo na mwisho, ona, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
27 And Achaz slepte with hise fadris, and thei birieden hym in the citee of Jerusalem; for thei resseyueden not hym in the sepulcris of the kyngis of Israel; and Ezechie, his sone, regnede for hym.
Ahazi akalala pamoja na babu zake, na wakamzika katika mji, katika Yerusalemu, lakini hawakumleta kwenye makaburi ya wafalme wa Israeli. Hezekia, mwanaye, akawa mfamle katika nafasi yake.

< 2 Chronicles 28 >