< Luke 19 >

1 And Jesus having entred Jericho passed through the city,
Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2 and behold, there was a man named Zaccheus, who was the chief publican, and very rich.
Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 And he sought to see Jesus who He was; but he could not for the croud; for he was little of stature.
Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4 And he ran before and got up into a sycamore-tree that he might see Him; for He was to pass by that way.
Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5 And when Jesus came to the place, He looked up and saw him, and said to him, Zaccheus, make haste and come down; for to-day I must abide at thy house.
Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
6 And he made haste and came down, and received Him with joy.
Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7 And when they saw it, they all murmured, saying, He is gone to be guest with a wicked man.
Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
8 But Zaccheus stood up and said unto Jesus, Behold, Lord, the half of my substance I give to the poor; and if I have taken any thing from any one wrongfully, I restore him fourfold.
Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
9 Then said Jesus, This day is salvation come to this house, for as much as he also is a son of Abraham.
Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10 For the Son of man is come to seek and to save that which was lost.
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
11 And as they listened to these things, He proceeded and spake a parable; because He was nigh to Jerusalem, and they thought that the kingdom of God would immediately be manifested.
Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12 He said therefore, A certain nobleman went into a distant country to receive the investiture of a kingdom and then to return.
Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13 And he called ten of his servants, and delivered to them ten pounds, and said, Trade with them till I come.
Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14 But his citizens hated him, and sent an embassy after him, saying, We will not have this man to reign over us.
Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15 And when he was returned, having received the kingdom, he ordered these servants to be called to him, to whom he had delivered the money, that he might know what use each had made of it.
“Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16 Then came the first and said, Lord, thy pound hath gained ten pounds.
Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17 And he said to him, Well done, thou good servant, as thou hast been faithful in a very little, thou shalt be governor over ten cities.
Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18 And the second came, saying, Lord, thy pound hath produced five pounds:
Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19 and he said to this likewise, Be thou also over five cities.
Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20 And another came, and said, Behold, my Lord, thy pound, which I have kept laid up in a napkin:
“Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21 for I was afraid of thee, because thou art an austere man, who takest up what thou didst not lay down, and reapest what thou didst not sow.
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22 But he said to him, Out of thy own mouth will I judge thee, thou wicked servant, Thou knewest that I am an austere man, taking up what I laid not down, and reaping what I did not sow;
Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23 and why then didst thou not put my money into the bank, that when I came I might have received it with interest?
Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24 And he said to them that stood by, Take away the pound from him, and give it to him that hath the ten pounds.
Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25 (And they said unto him, Lord, he hath ten pounds already: )
Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26 for I tell you, that to every one that hath shall be given; but from him that hath not, even what he seemingly hath shall be taken away.
Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 But those mine enemies, who would not have me to reign over them, bring hither, and slay them before me.
Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
28 And when He had said these things, He went forward, going up to Jerusalem.
Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29 And when He was nigh to Bethphage and Bethany, at the mount called the mount of Olives, He sent two of his disciples,
Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 saying, Go into the opposite village, in which, at your entring, ye will find a colt tied, on which no man ever yet sat; loose him and bring him hither.
akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31 And if any one ask you, Why do ye loose him? thus shall ye say unto him, The Lord hath need of him.
Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
32 And they that were sent, went away and found it as He had told them.
Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33 But as they were untying the colt, the owners of it said to them, Why do ye untie the colt?
Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
34 and they answered, The Lord hath need of him.
Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 And they brought him to Jesus: and throwing their garments upon the colt they set Jesus thereon.
Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36 And as He went along they spread their clothes under Him in the way.
Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 And when He was now come near to the foot of the mount of Olives, the whole multitude of the disciples rejoicing began to praise God with a loud voice for all the mighty works which they had seen,
Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38 saying, Blessed be the king that cometh in the name of the Lord: peace in heaven, and glory in the highest!
wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
39 And some of the pharisees from among the multitude said to Him, Master, rebuke thy disciples.
Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
40 And He answered them, I tell you, that if these were silent, the very stones would cry out.
Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
41 And as He drew near, beholding the city, He wept over it,
Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42 saying, If thou hadst known, even thou, at lest in this thy day, the things relating to thy peace--- but now they are hid from thine eyes.
akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 For the days shall come upon thee, that thine enemies shall cast up a trench about thee, and surround thee, and keep thee in on every side,
Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44 and shall lay thee to the ground, and thy children within thee; and they shall not leave in thee one stone upon another: because thou didst not regard the time of thy visitation.
Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
45 And He went into the temple, and cast out those that were buying and selling in it,
Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46 saying unto them, It is written, "my house is the house of prayer: but ye have made it a den of thieves."
akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
47 And He was teaching daily in the temple: but the chief priests and the scribes and the rulers of the people sought to destroy Him;
Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48 and could not find how to effect it: for all the people were attentive to hear Him.
lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.

< Luke 19 >