< Psalms 81 >

1 For the Chief Musician. On an instrument of Gath. By Asaph. Sing aloud to God, our strength! Make a joyful shout to the God of Jacob!
Mwimbieni Mungu aliye nguvu yetu kwa sauti; pigeni kelele za furaha kwa Mungu wa Yakobo.
2 Raise a song, and bring here the tambourine, the pleasant lyre with the harp.
Imbeni wimbo na pigeni matari, kinubi chenye sauti nzuri pamoja na kinanda.
3 Blow the shofar at the New Moon, at the full moon, on our feast day.
Pigeni panda mwandamo wa mwezi, katika siku ya mbalamwezi, mwanzoni mwa sikukuu.
4 For it is a statute for Israel, an ordinance of the God of Jacob.
Kwa kuwa ni agizo kwa Israeli, amri iliyotolewa na Mungu wa Yakobo.
5 He appointed it in Joseph for a covenant, when he went out over the land of Egypt, I heard a language that I didn’t know.
Aliitoa kama maelekezo kwa Yusufu alipoenda katika nchi ya Misri, ambako nilisikia sauti ambayo sikuweza kuitambua:
6 “I removed his shoulder from the burden. His hands were freed from the basket.
“Niliutua mzigo kutoka mabegani mwake; mikono yake ilipumzishwa kubeba kikapu.
7 You called in trouble, and I delivered you. I answered you in the secret place of thunder. I tested you at the waters of Meribah.” (Selah)
Katika dhiki yako uliniita, nami nikakusaidia; nilikujibu kutoka katika wingu jeusi la radi. Nilikujaribu kwenye maji ya Meriba. (Selah)
8 “Hear, my people, and I will testify to you, Israel, if you would listen to me!
Sikilizeni, watu wangu, nami nitawaonya, Israeli, kama tu ugalinisikiliza!
9 There shall be no strange god in you, neither shall you worship any foreign god.
Lazima kati yenu kusiwepo na mungu wa kigeni; haupaswi kumwabudu mungu wa kigeni.
10 I am the LORD, your God, who brought you up out of the land of Egypt. Open your mouth wide, and I will fill it.
Mimi ni Yahwe niliyekutoa katika nchi ya Misri, fungua sana kinywa chako, nami nitakijaza.
11 But my people didn’t listen to my voice. Israel desired none of me.
Lakini watu wangu hawakusikiliza maneno yangu; Israeli hawakunitii.
12 So I let them go after the stubbornness of their hearts, that they might walk in their own counsels.
Nikawaacha waende katika katika njia yao wenyewe ya ukaidi ili kwamba waweze kufanya kinachoonekana sahihi kwao.
13 Oh that my people would listen to me, that Israel would walk in my ways!
Oh, laiti watu wangu wangenisikiliza mimi; oh, watu wangu wangelitembea katika njia yangu.
14 I would soon subdue their enemies, and turn my hand against their adversaries.
Kisha ningewatiisha adui zao haraka na kugeuzia mkono wangu dhidi ya watesi wao.
15 The haters of the LORD would cringe before him, and their punishment would last forever.
Wale wanaomchukia Yahwe katika hofu na waanguke chini mbele zake! Wawe wanyonge milele.
16 But he would have also fed them with the finest of the wheat. I will satisfy you with honey out of the rock.”
Ningewalisha Israeli kwa ngano bora; Ningewatosheleza kwa asali itokayo mwambani.”

< Psalms 81 >