< Psalms 78 >

1 A contemplation by Asaph. Hear my teaching, my people. Turn your ears to the words of my mouth.
Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 I will open my mouth in a parable. I will utter dark sayings of old,
Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
3 which we have heard and known, and our fathers have told us.
Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
4 We will not hide them from their children, telling to the generation to come the praises of the LORD, his strength, and his wondrous deeds that he has done.
Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
5 For he established a covenant in Jacob, and appointed a teaching in Israel, which he commanded our fathers, that they should make them known to their children;
Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
6 that the generation to come might know, even the children who should be born; who should arise and tell their children,
Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
7 that they might set their hope in God, and not forget God’s deeds, but keep his commandments,
Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
8 and might not be as their fathers— a stubborn and rebellious generation, a generation that didn’t make their hearts loyal, whose spirit was not steadfast with God.
Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
9 The children of Ephraim, being armed and carrying bows, turned back in the day of battle.
Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
10 They didn’t keep God’s covenant, and refused to walk by his Torah.
Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
11 They forgot his doings, his wondrous deeds that he had shown them.
Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
12 He did marvelous things in the sight of their fathers, in the land of Egypt, in the field of Zoan.
Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
13 He split the sea, and caused them to pass through. He made the waters stand as a heap.
Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
14 In the daytime he also led them with a cloud, and all night with a light of fire.
Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
15 He split rocks in the wilderness, and gave them drink abundantly as out of the depths.
Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
16 He brought streams also out of the rock, and caused waters to run down like rivers.
Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
17 Yet they still went on to sin against him, to rebel against the Most High in the desert.
Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
18 They tempted God in their heart by asking food according to their desire.
Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
19 Yes, they spoke against God. They said, “Can God prepare a table in the wilderness?
Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
20 Behold, he struck the rock, so that waters gushed out, and streams overflowed. Can he give bread also? Will he provide meat for his people?”
Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
21 Therefore the LORD heard, and was angry. A fire was kindled against Jacob, anger also went up against Israel,
Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
22 because they didn’t believe in God, and didn’t trust in his salvation [yeshuat].
kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
23 Yet he commanded the skies above, and opened the doors of heaven.
Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
24 He rained down manna on them to eat, and gave them food from the sky.
Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
25 Man ate the bread of angels. He sent them food to the full.
Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
26 He caused the east wind to blow in the sky. By his power he guided the south wind.
Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
27 He also rained meat on them as the dust, winged birds as the sand of the seas.
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
28 He let them fall in the middle of their camp, around their habitations.
Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
29 So they ate, and were well filled. He gave them their own desire.
Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
30 They didn’t turn from their cravings. Their food was yet in their mouths,
Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
31 when the anger of God went up against them, killed some of their strongest, and struck down the young men of Israel.
Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
32 For all this they still sinned, and didn’t believe in his wondrous works.
Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33 Therefore he consumed their days in vanity, and their years in terror.
Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34 When he killed them, then they inquired after him. They returned and sought God earnestly.
Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
35 They remembered that God was their rock, the Most High God, their redeemer.
Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
36 But they flattered him with their mouth, and lied to him with their tongue.
Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
37 For their heart was not right with him, neither were they faithful in his covenant.
Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
38 But he, being merciful, forgave iniquity, and didn’t destroy them. Yes, many times he turned his anger away, and didn’t stir up all his wrath.
Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
39 He remembered that they were but flesh, a wind that passes away, and doesn’t come again.
Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
40 How often they rebelled against him in the wilderness, and grieved him in the desert!
Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
41 They turned again and tempted God, and provoked the Holy One of Israel.
Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
42 They didn’t remember his hand, nor the day when he redeemed them from the adversary;
Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
43 how he set his signs in Egypt, his wonders in the field of Zoan,
alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
44 he turned their rivers into blood, and their streams, so that they could not drink.
Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
45 He sent among them swarms of flies, which devoured them; and frogs, which destroyed them.
Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
46 He also gave their increase to the caterpillar, and their labor to the locust.
Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
47 He destroyed their vines with hail, their sycamore fig trees with frost.
Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
48 He also gave over their livestock to the hail, and their flocks to hot thunderbolts.
Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
49 He threw on them the fierceness of his anger, wrath, indignation, and trouble, and a band of angels of evil.
Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
50 He made a path for his anger. He didn’t spare their soul from death, but gave their life over to the pestilence,
Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
51 and struck all the firstborn in Egypt, the chief of their strength in the tents of Ham.
Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
52 But he led out his own people like sheep, and guided them in the wilderness like a flock.
Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
53 He led them safely, so that they weren’t afraid, but the sea overwhelmed their enemies.
Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
54 He brought them to the border of his sanctuary, to this mountain, which his right hand had taken.
Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
55 He also drove out the nations before them, allotted them for an inheritance by line, and made the tribes of Israel to dwell in their tents.
Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
56 Yet they tempted and rebelled against the Most High God, and didn’t keep his testimonies,
Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
57 but turned back, and dealt treacherously like their fathers. They were twisted like a deceitful bow.
Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
58 For they provoked him to anger with their high places, and moved him to jealousy with their engraved images.
Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59 When God heard this, he was angry, and greatly abhorred Israel,
Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60 so that he abandoned the tent of Shiloh, the tent which he placed among men,
Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61 and delivered his strength into captivity, his glory into the adversary’s hand.
Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
62 He also gave his people over to the sword, and was angry with his inheritance.
Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
63 Fire devoured their young men. Their virgins had no wedding song.
Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
64 Their priests fell by the sword, and their widows couldn’t weep.
Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
65 Then the Lord awakened as one out of sleep, like a mighty man who shouts by reason of wine.
Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
66 He struck his adversaries backward. He put them to a perpetual reproach.
Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
67 Moreover he rejected the tent of Joseph, and didn’t choose the tribe of Ephraim,
Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68 But chose the tribe of Judah, Mount Zion which he loved.
Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
69 He built his sanctuary like the heights, like the earth which he has established forever.
Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
70 He also chose David his servant, and took him from the sheepfolds;
Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
71 from following the ewes that have their young, he brought him to be the shepherd of Jacob, his people, and Israel, his inheritance.
Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
72 So he was their shepherd according to the integrity of his heart, and guided them by the skillfulness of his hands.
Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.

< Psalms 78 >