< Psalms 63 >

1 A Psalm by David, when he was in the desert of Judah. God, you are my God. I will earnestly seek you. My soul thirsts for you. My flesh longs for you, in a dry and weary land, where there is no water.
Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
2 So I have seen you in the sanctuary, watching your power and your glory.
Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
3 Because your loving kindness is better than life, my lips shall praise you.
Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
4 So I will bless you while I live. I will lift up my hands in your name.
Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
5 My soul shall be satisfied as with the richest food. My mouth shall praise you with joyful lips,
Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
6 when I remember you on my bed, and think about you in the night watches.
nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
7 For you have been my help. I will rejoice in the shadow of your wings.
Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
8 My soul stays close to you. Your right hand holds me up.
Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
9 But those who seek my soul to destroy it shall go into the lower parts of the earth.
Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
10 They shall be given over to the power of the sword. They shall be jackal food.
watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 But the king shall rejoice in God. Everyone who swears by him will praise him, for the mouth of those who speak lies shall be silenced.
Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.

< Psalms 63 >