< Psalms 57 >

1 For the Chief Musician. To the tune of “Do Not Destroy.” A poem by David, when he fled from Saul, in the cave. Be merciful to me, God, be merciful to me, for my soul takes refuge in you. Yes, in the shadow of your wings, I will take refuge, until disaster has passed.
Unihurumie, Mungu, unihurumie mimi, kwa maana ninakukimbilia wewe mpaka matatizo haya yaishe. Ninakaa chini ya mbawa za zako kwa ajili ya ulinzi mpaka huu uharibifu utakapoisha.
2 I cry out to God Most High, to God who accomplishes my requests for me.
Nitakulilia Mungu uliye hai, kwa Mungu, afanyaye mambo yote kwa ajili yangu.
3 He will send from heaven, and save me, he rebukes the one who is pursuing me. (Selah) God will send out his loving kindness and his truth.
Yeye atatuma msaada kutoka mbinguni na kuniokoa, ana hasira na wale wanaonishambulia. (Selah) Mungu atanitumia upendo wake mwema na uaminifu wake.
4 My soul is among lions. I lie among those who are set on fire, even the sons of men, whose teeth are spears and arrows, and their tongue a sharp sword.
Uhai wangu uko katikati ya simba; niko katikati ya wale walio tayari kunila. Niko katikati ya watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, na ambao ndimi zao ni kali kama upanga.
5 Be exalted, God, above the heavens! Let your glory be above all the earth!
Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu, utukufu wako uwe juu ya nchi yote.
6 They have prepared a net for my steps. My soul is bowed down. They dig a pit before me. They fall into the middle of it themselves. (Selah)
Wao walisambaza nje wavu kwa ajili ya miguu yangu; nilikuwa na shida sana. Walichimba shimo mbele yangu. Wao wenyewe wameangukia katikati ya shimo! (Selah)
7 My heart is steadfast, God. My heart is steadfast. I will sing, yes, I will sing praises.
Moyo wangu umeponywa, Mungu, moyo wangu umeponywa, nitaimba, ndiyo, nitaimba sifa.
8 Wake up, my glory! Wake up, lute and harp! I will wake up the dawn.
Inuka, moyo wa thamani; inuka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
9 I will give thanks to you, Lord, among the peoples. I will sing praises to you among the nations.
Nitakushukuru wewe, Bwana, kati ya watu; Kati ya mataifa nitakuimbia sifa.
10 For your great loving kindness reaches to the heavens, and your truth to the skies.
Maana upendo wako usiokwisha, huzifikia mbingu; na uaminifu wako mawinguni.
11 Be exalted, God, above the heavens. Let your glory be over all the earth.
Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu; na utukufu wako uinuliwe juu ya nchi yote.

< Psalms 57 >