< Psalms 50 >

1 A Psalm by Asaph. The Mighty One, God, the LORD, speaks, and calls the earth from sunrise to sunset.
Mungu, Mwenye nguvu, Yahwe, amenena naye aliita nchi toka mawio ya jua mpaka machweo yake.
2 Out of Zion, the perfection of beauty, God shines out.
Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
3 Our God comes, and does not keep silent. A fire devours before him. It is very stormy around him.
Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
4 He calls to the heavens above, to the earth, that he may judge his people:
Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
5 “Gather my holy ones together to me, those who have made a covenant with me by sacrifice.”
Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
6 The heavens shall declare his righteousness, for God himself is judge. (Selah)
Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
7 “Hear, my people, and I will speak. Israel, I will testify against you. I am God, your God.
Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
8 I don’t rebuke you for your sacrifices. Your burnt offerings are continually before me.
Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
9 I have no need for a bull from your stall, nor male goats from your pens.
Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
10 For every animal of the forest is mine, and the livestock on a thousand hills.
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
11 I know all the birds of the mountains. The wild animals of the field are mine.
Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
12 If I were hungry, I would not tell you, for the world is mine, and all that is in it.
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
13 Will I eat the meat of bulls, or drink the blood of goats?
Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
14 Offer to God the sacrifice of thanksgiving. Pay your vows to the Most High.
Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.
15 Call on me in the day of trouble. I will deliver you, and you will honor me.”
Mniite katika siku ya shida; nami nitawaokoa
16 But to the wicked God says, “What right do you have to declare my statutes, that you have taken my covenant on your lips,
Lakini kwa waovu Mungu anasema, “Inawahusu nini kuitangaza hali yangu, kwamba ninyi mmeliweka agano langu mdomoni mwenu,
17 since you hate instruction, and throw my words behind you?
wakati ninyi mnayachukia maelekezo na mnayatupa maneno yangu?
18 When you saw a thief, you consented with him, and have participated with adulterers.
Mumuanapo mwizi, ninyi hukubaliana naye; ninyi na mnashirikiana na wale wafanyao uasherati.
19 “You give your mouth to evil. Your tongue frames deceit.
Mwautoa mdomo wenu kwa mabaya, huelezea udanganyifu.
20 You sit and speak against your brother. You slander your own mother’s son.
Mnakaa na kuongea dhidi ya ndugu yenu; na kukashfu mwana wa mama yenu.
21 You have done these things, and I kept silent. You thought that I was just like you. I will rebuke you, and accuse you in front of your eyes.
Mmefanya mambo haya, lakini nimekaa kimya, hivyo mlidhani kuwa ni mtu flani nilliye kama ninyi mlivyo. Lakini nitawakaripia ninyi na kuwafunua, mbele ya macho yenu, mambo yote miliyofanya.
22 “Now consider this, you who forget God, lest I tear you into pieces, and there be no one to deliver.
Mlitilie maanani hili, ninyi mnao msahau Mungu, vinginevyo nitawakata ninyi vipande vipande, na hatakuwepo yeyote wakuja kuwasaidia!
23 Whoever offers the sacrifice of thanksgiving glorifies me, and prepares his way so that I will show God’s salvation to him.”
Yule atoaye sadaka ya shukurani hunitukuza, na yeyote apangaye njia zake katika namna iliyo sahihi nitamuonesha wokovu wa Mungu.”

< Psalms 50 >