< Psalms 45 >

1 For the Chief Musician. Set to “The Lilies.” A contemplation by the sons of Korah. A wedding song. My heart overflows with a noble theme. I recite my verses for the king. My tongue is like the pen of a skillful writer.
Moyo wangu unafurika kwa neno zuri; nitasoma kwa sauti maneno niliyo yaandika kuhusu mfalme; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mwenye ustadi.
2 You are the most excellent of the sons of men. Grace has anointed your lips, therefore God has blessed you forever.
Wewe u mzuri sana kuliko mwanadamu yeyote; neema imemiminwa midomoni mwako; Kwa hiyo tunajua ya kuwa Mungu amekubariki milele.
3 Strap your sword on your thigh, O mighty one, in your splendor and your majesty.
Weka upanga wako upande wako, wewe uliye mwenye nguvu, katika utukufu wako na enzi yako.
4 In your majesty ride on victoriously on behalf of truth, humility, and righteousness. Let your right hand display awesome deeds.
Katika enzi yako enenda katika ushindi kwa sababu ya uaminifu, upole, na haki; mkono wako wa kuume utakufundisha mambo ya kutisha.
5 Your arrows are sharp. The nations fall under you, with arrows in the heart of the king’s enemies.
Mishale yako ni mkali; watu huanguka chini yako; mishale yako imo ndani ya mioyo ya adui za mfalme.
6 Your throne, God, is forever and ever. A scepter of equity is the scepter of your kingdom.
Kiti chako cha enzi, Mungu ni cha milele na milele; na fimbo ya haki ni fimbo ya utawala wako.
7 You have loved righteousness, and hated wickedness. Therefore God, your God, has anointed you with the oil of gladness above your fellows.
Umeipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekupaka mafuta ya furaha kuliko wenzako.
8 All your garments smell like myrrh, aloes, and cassia. Out of ivory palaces stringed instruments have made you glad.
Mavazi yako yote hunukia manemane, udi, na mdalasini; kukoka katika majumba ya pembe vyombo vya muziki wa nyuzi vimekufurahisha.
9 Kings’ daughters are among your honorable women. At your right hand the queen stands in gold of Ophir.
Binti za wafalme ni kati ya wake zako waheshimiwa; na mkono wako wa kuume amesimama malikia aliye vaa mavazi ya dhahabu ya Ofiri.
10 Listen, daughter, consider, and turn your ear. Forget your own people, and also your father’s house.
Sikiliza, mwanangu, tafakari na utege sikio lako; uwasahahu watu wako na watu wa nyumba ya baba yako.
11 So the king will desire your beauty, honor him, for he is your lord.
Hivyo mfalme atautamani uzuri wako; yeye ni Bwana wako; umstahi.
12 The daughter of Tyre comes with a gift. The rich among the people entreat your favor.
Binti wa Tiro atakuwepo akiwa na zawadi; matajiri kati wa watu watajipendekeza kwako.
13 The princess inside is all glorious. Her clothing is interwoven with gold.
Binti mfalme katika jumba la kifahari ana utukufu wote; mavazi yake yametengenezwa kwa dhahabu.
14 She shall be led to the king in embroidered work. The virgins, her companions who follow her, shall be brought to you.
Naye ataongozwa kwa mfalme akiwa katika mavazi ya dhahabu; mabikra, wenzake wanoumfuata, wataletwa kwako mafalme.
15 With gladness and rejoicing they shall be led. They shall enter into the king’s palace.
Wao wataongozwa kwa furaha na shangwe; wataingia mahali pa mfalme.
16 Your sons will take the place of your fathers. You shall make them princes in all the earth.
Katika mahali pa baba zako watoto wako watakuwepo, ambao wewe utawafanya kuwa wakuu katika nchi yote.
17 I will make your name to be remembered in all generations. Therefore the peoples shall give you thanks forever and ever.
Nami nitalifanya jina lako kukumbukwa katika uzao wote; kwa hiyo watu watakushukuru milele na milele.

< Psalms 45 >