< Psalms 34 >

1 By David; when he pretended to be insane before Abimelech, who drove him away, and he departed. I will bless the LORD at all times. His praise will always be in my mouth.
Nitamsifu Yahwe wakati wote, siku zote sifa zake zitakuwa mdomoni mwangu.
2 My soul shall boast in the LORD. The humble shall hear of it and be glad.
Nitamsifu Yahwe! walio onewa wasikie na kufurahi.
3 Oh magnify the LORD with me. Let’s exalt his name together.
Msifuni Yahwe pamoja nami, kwa pamoja tuliinue jina lake.
4 I sought the LORD, and he answered me, and delivered me from all my fears.
Nilimuomba Yahwe msaada naye akanijibu, akanipa ushindi juu ya hofu yangu yote.
5 They looked to him, and were radiant. Their faces shall never be covered with shame.
Wale wanao mtazama yeye wana furaha, na nyuso zao hazina aibu.
6 This poor man cried, and the LORD heard him, and saved him out of all his troubles.
Huyu mtu aliye onewa alilia na Yahwe akamsikia na kumuokoa kwenye matatizo yake yote.
7 The LORD’s angel encamps around those who fear him, and delivers them.
Malaika wa Yahwe huweka kambi wakiwazunguka wale wanao muogopa yeye na kuwaokoa.
8 Oh taste and see that the LORD is good. Blessed is the man who takes refuge in him.
Onjeni muone Yahwe ni mzuri. Amebarikiwa mtu yule ambaye Yahwe ni kimbilio lake.
9 Oh fear the LORD, you his holy ones, for there is no lack with those who fear him.
Muogopeni Yahwe, ninyi watu watakatifu wake. Hakuna kupungukikwa kwa wale wanao mhofu yeye.
10 The young lions do lack, and suffer hunger, but those who seek the LORD shall not lack any good thing.
Simba wadogo wakati mwingine hukosa chakula na kuteseka kwa njaa, bali wale wamtafutao Yahwe hawatapungukiwa chochote kilicho kizuri.
11 Come, you children, listen to me. I will teach you the fear of the LORD.
Njoni, wana, mnisikilize mimi. nitawafundisha ninyi hofu ya Yahwe.
12 Who is someone who desires life, and loves many days, that he may see good?
Mtu nani aliyepo ambaye anatamani maisha na anapenda kuwa na siku nyingi, ili kwamba aweze kuona vizuri?
13 Keep your tongue from evil, and your lips from speaking lies.
Hivyo uepushe ulimi wako na uovu na uilinde midomo yako kuongea uongo.
14 Depart from evil, and do good. Seek peace, and pursue it.
Uache uovu na utende mema. Uitafute amani na kuiendea amani.
15 The LORD’s eyes are toward the righteous. His ears listen to their cry.
Macho ya Yahwe yako kwenye haki na masikio yake huelekea kulia kwao.
16 The LORD’s face is against those who do evil, to cut off their memory from the earth.
Uso wa Yahwe uko kinyume na wale watendao uovu, kuikatilia mbali kumbukumbu yao duniani.
17 The righteous cry, and the LORD hears, and delivers them out of all their troubles.
Wenye haki hulia na Yahwe husikia na kuwaokoa kwenye matatizo yao yote.
18 The LORD is near to those who have a broken heart, and saves those who have a crushed spirit.
Yahwe yu karibu nao waliovunjika moyo, naye huwaokoa waliogandamizwa rohoni.
19 Many are the afflictions of the righteous, but the LORD delivers him out of them all.
Mateso ya wenye haki ni mengi, bali Yahwe huwaokoa nayo yote.
20 He protects all of his bones. Not one of them is broken.
Yeye huitunza mifupa yake yote, hakuna hata mmoja wao utavunjika.
21 Evil shall kill the wicked. Those who hate the righteous shall be condemned.
Uovu utawauwa waovu. Wale wachukiao haki watahukumiwa.
22 The LORD redeems the soul of his servants. None of those who take refuge in him shall be condemned.
Yahwe huokoa maisha ya watumishi wake. Hakuna atakaye hukumiwa hata mmoja atafutaye usalama katika yeye.

< Psalms 34 >