< Psalms 101 >

1 A Psalm by David. I will sing of loving kindness and justice. To you, LORD, I will sing praises.
Nitaimba uaminifu wa agano lako na hukumu; kwako, Ee Yahwe, Nitakuimbia sifa.
2 I will be careful to live a blameless life. When will you come to me? I will walk within my house with a blameless heart.
Nitatembea katika njia ya uadilifu. Oh, ni lini utakuja kwangu? Nitatembea kwa uadilifu ndani ya nyumba yangu.
3 I will set no vile thing before my eyes. I hate the deeds of faithless men. They will not cling to me.
Sitaweka matendo maovu mbele ya macho yangu; ninachukia uovu usio na maana; hauta shikamana nami.
4 A perverse heart will be far from me. I will have nothing to do with evil.
Watu waliopotoka wataniacha mimi; mimi sichangamani na uovu.
5 I will silence whoever secretly slanders his neighbor. I won’t tolerate one who is arrogant and conceited.
Nitamwangamiza yeyote amsengenyaye jirani yake kwa siri. Sitamvumilia yeyote mwenye kiburi.
6 My eyes will be on the faithful of the land, that they may dwell with me. He who walks in a perfect way, he will serve me.
Nitawachagua walio waaminifu katika nchi wakae upande wangu. Wale watembeao katika njia ya uhadilifu watanitumikia.
7 He who practices deceit won’t dwell within my house. He who speaks falsehood won’t be established before my eyes.
Watu wadanganyifu hawatabaki ndani ya nyumba yangu; waongo hawatakaribishwa mbele ya macho yangu.
8 Morning by morning, I will destroy all the wicked of the land, to cut off all the workers of iniquity from the LORD’s city.
Asubuhi hata asubuhi nitawaangamiza waovu wote kutoka nchini; nitawaondoa watendao maovu wote katika mji wa Yahwe.

< Psalms 101 >