< Psalms 1 >

1 Blessed is the man who doesn’t walk in the counsel of the wicked, nor stand on the path of sinners, nor sit in the seat of scoffers;
Amebarikiwa mtu yule asiye enenda katika ushauri wa waovu, au kusimama katika njia ya wenye dhambi, au kukaa katika kusanyiko la wenye mizaha.
2 but his delight is in the LORD’s law. On his Torah he meditates day and night.
Bali yeye huifurahia sheria ya Yahwe, na huitafakari sheria yake mchana na usiku.
3 He will be like a tree planted by the streams of water, that produces its fruit in its season, whose leaf also does not wither. Whatever he does shall prosper.
Atakuwa kama mti uliopandwa karibu na mkondo wa maji ambao huzaa matunda yake kwa majira yake, ambao majani yake hayakauki; lolote afanyalo litafanikiwa.
4 The wicked are not so, but are like the chaff which the wind drives away.
Waovu hawako hivyo, wao badala yake ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 Therefore the wicked shall not stand in the judgment, nor sinners in the congregation of the righteous.
Kwa hivyo waovu hawatasimama katika hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 For the LORD knows the way of the righteous, but the way of the wicked shall perish.
Kwa kuwa Yahweh huikubali njia ya wenye haki, njia ya waovu itaangamizwa.

< Psalms 1 >