< Numbers 1 >

1 The LORD spoke to Moses in the wilderness of Sinai, in the Tent of Meeting, on the first day of the second month, in the second year after they had come out of the land of Egypt, saying,
Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
2 “Take a census of all the congregation of the children of Israel, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, every male, one by one,
“Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
3 from twenty years old and upward, all who are able to go out to war in Israel. You and Aaron shall count them by their divisions.
Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
4 With you there shall be a man of every tribe, each one head of his fathers’ house.
Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
5 These are the names of the men who shall stand with you: Of Reuben: Elizur the son of Shedeur.
Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
6 Of Simeon: Shelumiel the son of Zurishaddai.
kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
7 Of Judah: Nahshon the son of Amminadab.
kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
8 Of Issachar: Nethanel the son of Zuar.
kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
9 Of Zebulun: Eliab the son of Helon.
kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
10 Of the children of Joseph: of Ephraim: Elishama the son of Ammihud; of Manasseh: Gamaliel the son of Pedahzur.
kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
11 Of Benjamin: Abidan the son of Gideoni.
kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
12 Of Dan: Ahiezer the son of Ammishaddai.
kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
13 Of Asher: Pagiel the son of Ochran.
kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
14 Of Gad: Eliasaph the son of Deuel.
kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
15 Of Naphtali: Ahira the son of Enan.”
kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
16 These are those who were called of the congregation, the princes of the tribes of their fathers; they were the heads of the thousands of Israel.
Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
17 Moses and Aaron took these men who are mentioned by name.
Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
18 They assembled all the congregation together on the first day of the second month; and they declared their ancestry by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, one by one.
wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
19 As the LORD commanded Moses, so he counted them in the wilderness of Sinai.
kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
20 The children of Reuben, Israel’s firstborn, their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, one by one, every male from twenty years old and upward, all who were able to go out to war:
Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
21 those who were counted of them, of the tribe of Reuben, were forty-six thousand five hundred.
Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
22 Of the children of Simeon, their generations, by their families, by their fathers’ houses, those who were counted of it, according to the number of the names, one by one, every male from twenty years old and upward, all who were able to go out to war:
Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
23 those who were counted of them, of the tribe of Simeon, were fifty-nine thousand three hundred.
Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
24 Of the children of Gad, their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war:
Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
25 those who were counted of them, of the tribe of Gad, were forty-five thousand six hundred fifty.
Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
26 Of the children of Judah, their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war:
Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
27 those who were counted of them, of the tribe of Judah, were seventy-four thousand six hundred.
Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
28 Of the children of Issachar, their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war:
Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
29 those who were counted of them, of the tribe of Issachar, were fifty-four thousand four hundred.
Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
30 Of the children of Zebulun, their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war:
Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
31 those who were counted of them, of the tribe of Zebulun, were fifty-seven thousand four hundred.
Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
32 Of the children of Joseph: of the children of Ephraim, their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war:
Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
33 those who were counted of them, of the tribe of Ephraim, were forty thousand five hundred.
Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
34 Of the children of Manasseh, their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war:
Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
35 those who were counted of them, of the tribe of Manasseh, were thirty-two thousand two hundred.
Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
36 Of the children of Benjamin, their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war:
Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
37 those who were counted of them, of the tribe of Benjamin, were thirty-five thousand four hundred.
Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
38 Of the children of Dan, their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war:
Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
39 those who were counted of them, of the tribe of Dan, were sixty-two thousand seven hundred.
Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
40 Of the children of Asher, their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war:
Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
41 those who were counted of them, of the tribe of Asher, were forty-one thousand five hundred.
Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
42 Of the children of Naphtali, their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war:
Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
43 those who were counted of them, of the tribe of Naphtali, were fifty-three thousand four hundred.
Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
44 These are those who were counted, whom Moses and Aaron counted, and the twelve men who were princes of Israel, each one for his fathers’ house.
Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
45 So all those who were counted of the children of Israel by their fathers’ houses, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war in Israel—
Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
46 all those who were counted were six hundred three thousand five hundred fifty.
Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
47 But the Levites after the tribe of their fathers were not counted among them.
Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
48 For the LORD spoke to Moses, saying,
Bwana alikuwa amemwambia Mose:
49 “Only the tribe of Levi you shall not count, neither shall you take a census of them among the children of Israel;
“Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
50 but appoint the Levites over the Tabernacle of the Testimony, and over all its furnishings, and over all that belongs to it. They shall carry the tabernacle and all its furnishings; and they shall take care of it, and shall encamp around it.
Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
51 When the tabernacle is to move, the Levites shall take it down; and when the tabernacle is to be set up, the Levites shall set it up. The stranger who comes near shall be put to death.
Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
52 The children of Israel shall pitch their tents, every man by his own camp, and every man by his own standard, according to their divisions.
Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
53 But the Levites shall encamp around the Tabernacle of the Testimony, that there may be no wrath on the congregation of the children of Israel. The Levites shall be responsible for the Tabernacle of the Testimony.”
Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
54 Thus the children of Israel did. According to all that the LORD commanded Moses, so they did.
Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.

< Numbers 1 >