< Numbers 34 >

1 The LORD spoke to Moses, saying,
BWANA akanena na Musa akasema,
2 “Command the children of Israel, and tell them, ‘When you come into the land of Canaan (this is the land that shall fall to you for an inheritance, even the land of Canaan according to its borders),
“Waamuru watu wa Israeli na uwaambie, 'Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani, nchi ambayo itakuwa mali yenu, nchi ya Kanaani na mipaka yake, mpaka wenu wa kusini utaendelea kutoka nyika ya Sini hadi mpaka wa Edomu.
3 then your south quarter shall be from the wilderness of Zin along by the side of Edom, and your south border shall be from the end of the Salt Sea eastward.
Mwisho wa mpaka wa kusini utakuwa mwisho wa bahari ya chumvi kuelekea mashariki.
4 Your border shall turn about southward of the ascent of Akrabbim, and pass along to Zin; and it shall pass southward of Kadesh Barnea; and it shall go from there to Hazar Addar, and pass along to Azmon.
Mpaka wenu utageukia kusini kutoka mlima kuelekea Akrabimu na kupitia nyika ya Sini. na kutokea huko utaelelkea kusini mwa Kadeshi Barinea na kuelekea Hazari Adari mpaka Azimoni.
5 The border shall turn about from Azmon to the brook of Egypt, and it shall end at the sea.
Kutoka huko, mpaka utageuka kutoka Azimoni kuelekea kijito cha Misri na kukifuata mpaka baharini.
6 “‘For the western border, you shall have the great sea and its border. This shall be your west border.
Mpaka wa Magharibi utakuwa pwani ya bahari kuu. Huu ndio utakuwa mpaka wenuwa Magharibi.
7 “‘This shall be your north border: from the great sea you shall mark out for yourselves Mount Hor.
Mpaka wenu wa kaskazini utaanzia kwenye bahari kuu hadi Mlima Hori,
8 From Mount Hor you shall mark out to the entrance of Hamath; and the border shall pass by Zedad.
kisha kutoka Mlima Hori hadi Lebo Hamathi, kisha Zedadi.
9 Then the border shall go to Ziphron, and it shall end at Hazar Enan. This shall be your north border.
Mpaka utaendelea hadi Zifroni na kuishia Hazari Enani. Huu ndio utakuwa mpaka wenu wa kaskazini.
10 “‘You shall mark out your east border from Hazar Enan to Shepham.
Kisha mtaweka alama za mpaka wenu wa mashariki ambao utaanzia Hazari Enani kuelekea kusini Shefamu.
11 The border shall go down from Shepham to Riblah, on the east side of Ain. The border shall go down, and shall reach to the side of the sea of Chinnereth eastward.
Kisha mpaka wa kusini utaendelea kutoka Shefamu hadi Ribla, upande wa masharikia mwa Aini. Mpaka utaedelea upande huo wa mashariki hadi upande wa mashariki wa bahari ya Kinerethi.
12 The border shall go down to the Jordan, and end at the Salt Sea. This shall be your land according to its borders around it.’”
Kisha mpaka utaendelea kuelekea kusini hadi mto Yorodani na hadi bahari ya chumvi. Hii ndiyo itakuwa nchi yenu, kwa kuifuata mipaka yake yote inayozunguka.'”
13 Moses commanded the children of Israel, saying, “This is the land which you shall inherit by lot, which the LORD has commanded to give to the nine tribes, and to the half-tribe;
Kisha Musa akawaamuru watu wa Israeli akasema, “Hii ndiyo nchi ambayo mtaipokes kwa kura, ambayo BWANA ameamuru kuwapa wale makabila tisa na nusu.
14 for the tribe of the children of Reuben according to their fathers’ houses, the tribe of the children of Gad according to their fathers’ houses, and the half-tribe of Manasseh have received their inheritance.
Kabila ya uzao wa Reubeni, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na uzao wa kabila la Gadi, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na nusu ya Manase wamepata ardhi yao.
15 The two tribes and the half-tribe have received their inheritance beyond the Jordan at Jericho eastward, toward the sunrise.”
Wale makabila mawili na nusu wameshapata mgawo wao ng'ambo ya mto Yorodani upande wa mashariki, kuelekea kule linakotokea jua.”
16 The LORD spoke to Moses, saying,
BWANA akanena na Musa akasema,
17 “These are the names of the men who shall divide the land to you for inheritance: Eleazar the priest, and Joshua the son of Nun.
“Haya ndiyo majinaya watu watakaoigawa ardhi kwa ajili ya urithi wao: Eliazari kuhani na Joshua mwana wa Nuni.
18 You shall take one prince of every tribe, to divide the land for inheritance.
Mtachagua kiongozi mmoja toka kila kabila ili kuigawa ardhi kwa koo zao.
19 These are the names of the men: Of the tribe of Judah, Caleb the son of Jephunneh.
Haya ndiyo majina ya wanaume: Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune.
20 Of the tribe of the children of Simeon, Shemuel the son of Ammihud.
Kutoka kwenye kabila la uzao wa Simeoni, Shemueli mwana wa Amihudi.
21 Of the tribe of Benjamin, Elidad the son of Chislon.
Kutoka kabila la Benjamini, Elidadi mwana wa Kisloni.
22 Of the tribe of the children of Dan a prince, Bukki the son of Jogli.
Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Dani, Buki mwana wa Jogili.
23 Of the children of Joseph: of the tribe of the children of Manasseh a prince, Hanniel the son of Ephod.
Kiongozi kutoka uzao wa Yusufu, kwenye kabila la Manase, Hannieli mwana wa Efodi.
24 Of the tribe of the children of Ephraim a prince, Kemuel the son of Shiphtan.
Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Efraimu, Kemueli mwana wa Shiftani.
25 Of the tribe of the children of Zebulun a prince, Elizaphan the son of Parnach.
Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Zabuloni, Elizafani mwana wa Parinaki.
26 Of the tribe of the children of Issachar a prince, Paltiel the son of Azzan.
Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Isakari, Palitieli mwana wa Azzani.
27 Of the tribe of the children of Asher a prince, Ahihud the son of Shelomi.
Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Asheri, Ahihudi mwana wa Shelomi.
28 Of the tribe of the children of Naphtali a prince, Pedahel the son of Ammihud.”
Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Naftali, Pedaheli mwana wa Amihudi.”
29 These are they whom the LORD commanded to divide the inheritance to the children of Israel in the land of Canaan.
BWANA aliwaamuru wanaume hawa kuigawa nchi ya Kanaani na kuwapa kila kabla sehemu yao.

< Numbers 34 >