< Job 41 >

1 “Can you draw out Leviathan with a fish hook, or press down his tongue with a cord?
Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
2 Can you put a rope into his nose, or pierce his jaw through with a hook?
Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
3 Will he make many petitions to you, or will he speak soft words to you?
Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
4 Will he make a covenant with you, that you should take him for a servant forever?
Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
5 Will you play with him as with a bird? Or will you bind him for your girls?
Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
6 Will traders barter for him? Will they part him among the merchants?
Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
7 Can you fill his skin with barbed irons, or his head with fish spears?
Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
8 Lay your hand on him. Remember the battle, and do so no more.
Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
9 Behold, the hope of him is in vain. Won’t one be cast down even at the sight of him?
Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
10 None is so fierce that he dare stir him up. Who then is he who can stand before me?
Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
11 Who has first given to me, that I should repay him? Everything under the heavens is mine.
Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
12 “I will not keep silence concerning his limbs, nor his mighty strength, nor his goodly frame.
Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
13 Who can strip off his outer garment? Who will come within his jaws?
Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
14 Who can open the doors of his face? Around his teeth is terror.
Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
15 Strong scales are his pride, shut up together with a close seal.
Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
16 One is so near to another, that no air can come between them.
Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
17 They are joined to one another. They stick together, so that they can’t be pulled apart.
Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
18 His sneezing flashes out light. His eyes are like the eyelids of the morning.
Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
19 Out of his mouth go burning torches. Sparks of fire leap out.
Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
20 Out of his nostrils a smoke goes, as of a boiling pot over a fire of reeds.
Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
21 His breath kindles coals. A flame goes out of his mouth.
Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
22 There is strength in his neck. Terror dances before him.
Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
23 The flakes of his flesh are joined together. They are firm on him. They can’t be moved.
Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
24 His heart is as firm as a stone, yes, firm as the lower millstone.
Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
25 When he raises himself up, the mighty are afraid. They retreat before his thrashing.
Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
26 If one attacks him with the sword, it can’t prevail; nor the spear, the dart, nor the pointed shaft.
Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
27 He counts iron as straw, and bronze as rotten wood.
Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
28 The arrow can’t make him flee. Sling stones are like chaff to him.
Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
29 Clubs are counted as stubble. He laughs at the rushing of the javelin.
Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
30 His undersides are like sharp potsherds, leaving a trail in the mud like a threshing sledge.
Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
31 He makes the deep to boil like a pot. He makes the sea like a pot of ointment.
Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
32 He makes a path shine after him. One would think the deep had white hair.
Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
33 On earth there is not his equal, that is made without fear.
Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
34 He sees everything that is high. He is king over all the sons of pride.”
Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”

< Job 41 >