< Job 18 >

1 Then Bildad the Shuhite answered,
Ndipo Bildadi Mshuhi alijibu na kusema, “
2 “How long will you hunt for words? Consider, and afterwards we will speak.
Je, lini utaacha kusema kwako? Fikiri, na baadaye tutazungumza.
3 Why are we counted as animals, which have become unclean in your sight?
Kwa nini sisi tumehesabiwa kama wanyama mwitu; kwa nini tumekuwa wapumbavu machoni pako?
4 You who tear yourself in your anger, will the earth be forsaken for you? Or will the rock be removed out of its place?
Wewe ambaye wajirarua mwenyewe katika hasira yako, nchi haipaswi kuachwa kwa ajili yako au miamba inapaswa kuondolewa kutoka mahali pake?
5 “Yes, the light of the wicked will be put out. The spark of his fire won’t shine.
Ni dhahiri, nuru ya watu waovu itawekwa nje; cheche ya moto wake haitanga'ra.
6 The light will be dark in his tent. His lamp above him will be put out.
Nuru itakuwa giza katika hema yake; taa yake juu yake yeye itawekwa nje.
7 The steps of his strength will be shortened. His own counsel will cast him down.
Hatua za nguvu zake yeye zitafanywa kuwa fupi; mipango yake yeye mwenyewe itamwangusha yeye chini.
8 For he is cast into a net by his own feet, and he wanders into its mesh.
Kwa maana yeye atatupwa katika mtego kwa miguu yake mwenyewe; yeye atatembea katika mahangaiko.
9 A snare will take him by the heel. A trap will catch him.
Tanzi litamchukua yeye kwa kisigino; mtego utabaki kushikilia juu yake.
10 A noose is hidden for him in the ground, a trap for him on the path.
Tanzi limefichwa kwa ajili yake chini ya ardhi; na mtego kwa ajili yake katika njia.
11 Terrors will make him afraid on every side, and will chase him at his heels.
Watishao watamfanya yeye aogope juu ya sehemu zote; wao watamkimbiza yeye kwenye visigino vyake.
12 His strength will be famished. Calamity will be ready at his side.
Utajiri wake utageuka kuwa njaa, na majanga yatakuwa tayari upande wake.
13 The members of his body will be devoured. The firstborn of death will devour his members.
Sehemu za mwili wake zitakuwa zimemezwa; Hakika, mzaliwa wa kwanza wa kifo atazila sehemu zake yeye.
14 He will be rooted out of the security of his tent. He will be brought to the king of terrors.
Yeye ameraruliwa kutoka kwenye usalama wa hema yake na hakuweza kutembea kwenda kwa mfalme mwenye utisho.
15 There will dwell in his tent that which is none of his. Sulfur will be scattered on his habitation.
Watu ambao siyo wa kwake wataishi kwenye hema yake baada ya kuona ule moto mesambaa ndani ya nyumba yake yeye.
16 His roots will be dried up beneath. His branch will be cut off above.
Mizizi yake itanyauka chini yake; juu tawi lake yeye litakatwa.
17 His memory will perish from the earth. He will have no name in the street.
Kumbukumbu lake yeye litapotea kutoka katika nchi; yeye hatakuwa na jina katika mtaa.
18 He will be driven from light into darkness, and chased out of the world.
Yeye atafukuzwa kutoka katika nuru mpaka kwenye giza na kuwa amefukuzwa nje na ulimwengu huu.
19 He will have neither son nor grandson among his people, nor any remaining where he lived.
Hatakuwa na mtoto wa kiume wala mjukuu miongonni mwa watu wake, wala kizazi chochote kitakachobakia mahali alipokuwa amekaa.
20 Those who come after will be astonished at his day, as those who went before were frightened.
Wale wanaoishi upande wa magharibi watakuwa wametiwa hofu kwa kile kitakachotokea kwake siku moja; wale wanaoishi upande wa mashariki watakuwa wameogopeshwa kwa hicho.
21 Surely such are the dwellings of the unrighteous. This is the place of him who doesn’t know God.”
Hakika hizo ni nyumba za watu wasio haki, ni sehemu ya wale wasiomjua Mungu.”

< Job 18 >