< Job 12 >

1 Then Job answered,
Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
2 “No doubt, but you are the people, and wisdom will die with you.
“Hakuna shaka ninyi wanadamu; Hekima mtakufa nayo.
3 But I have understanding as well as you; I am not inferior to you. Yes, who doesn’t know such things as these?
Lakini nina ufahamu kama vile ninyi; Mimi siyo duni kwenu. Ni dhhiri, ni nani asiyefahamu vitu hivyo kama hivi?
4 I am like one who is a joke to his neighbor, I, who called on God, and he answered. The just, the blameless man is a joke.
Mimi ni kitu cha kuchekwa na jirani-Mimi, ni mmoja aliyemwita Mungu na ambaye alijibiwa na yeye! Mimi, ni mwenye haki na mtu asiyekuwa na hatia-Mimi sasa nimekuwa kitu cha kuchekwa.
5 In the thought of him who is at ease there is contempt for misfortune. It is ready for them whose foot slips.
Katika mawazo yake mtu fulani aliye katika kufurahi, kuna kudharau kwa mashaka; hufikiri katika njia ambayo huleta mambo mabaya zaidi kwa wale ambao miguu yao inateleza.
6 The tents of robbers prosper. Those who provoke God are secure, who carry their god in their hands.
Hema za wezi hufanikiwa, na wale ambao humkasirisha Mungu huhisi salama; mikono yao wenyewe ni miungu wao.
7 “But ask the animals now, and they will teach you; the birds of the sky, and they will tell you.
Lakini sasa waulize hao wanyama wa mwituni, na watakufundisha wewe; waulize ndege wa angani, na watakuambia wewe.
8 Or speak to the earth, and it will teach you. The fish of the sea will declare to you.
Au iambie ardhi, na itakufundisha wewe; samaki wa baharini watakutangazia wewe.
9 Who doesn’t know that in all these, the LORD’s hand has done this,
Ni myama yupi miongoni mwa hawa asiyefahamu kuwa mkono wa Yahwe umetenda haya?
10 in whose hand is the life of every living thing, and the breath of all mankind?
Katika mkono wake mna uzima wa kila kiumbe hai na pumzi ya wanadamu wote.
11 Doesn’t the ear try words, even as the palate tastes its food?
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile kaakaa lionjavyo chakula chake?
12 With aged men is wisdom, in length of days understanding.
Kwa wazee mna hekima; katika wingi wa siku mna ufahamu.
13 “With God is wisdom and might. He has counsel and understanding.
Pamoja na Mungu mna hekima na ukuu; yeye anayo mashauri na ufahamu.
14 Behold, he breaks down, and it can’t be built again. He imprisons a man, and there can be no release.
Tazama, yeye huangusha chini, na haiwezekani kujengwa tena; kama yeye akimtia gerezani mtu yeyote, hakutakuwa tena kufunguliwa.
15 Behold, he withholds the waters, and they dry up. Again, he sends them out, and they overturn the earth.
Tazama, kama yeye akiyazuia maji, yanakauka; na kama akiyaachilia nje yanaitaabisha ardhi.
16 With him is strength and wisdom. The deceived and the deceiver are his.
Pamoja na yeye mna nguvu na hekima; watu ambao wamedanganywa na mdanganyi wote pamoja wako katika nguvu zake.
17 He leads counselors away stripped. He makes judges fools.
Yeye huwaongoza washauri mbali bila kuvaa viatu katika huzuni; huwarudisha hakimu katika upumbavu.
18 He loosens the bond of kings. He binds their waist with a belt.
Yeye Huondoa minyororo ya mamlaka kutoka kwa wafalme; yeye hufunika viuno vyao kwa nguo.
19 He leads priests away stripped, and overthrows the mighty.
Yeye huwaongoza makuhani mbali bila kuvaa viatu na kuwapindua watu wakuu.
20 He removes the speech of those who are trusted, and takes away the understanding of the elders.
Yeye huondoa hotuba ya wale waliokuwa wameaminiwa na huondoa mbali ufahamu wa wazee.
21 He pours contempt on princes, and loosens the belt of the strong.
Yeye humwaga aibu juu ya binti za wafalme na hufungua mishipi ya watu wenye nguvu.
22 He uncovers deep things out of darkness, and brings out to light the shadow of death.
Yeye huweka wazi vitu vya kina kutoka katika giza na kuvileta nje kumuika vivuli mahali ambapa watu waliokufa wapo.
23 He increases the nations, and he destroys them. He enlarges the nations, and he leads them captive.
Yeye huyafanya mataifa kuwa na nguvu, na pia huyaharibu; Yeye pia huyakuza mataifa, na pia yeye huyaongoza mbali kama wafungwa.
24 He takes away understanding from the chiefs of the people of the earth, and causes them to wander in a wilderness where there is no way.
Yeye huondoa mbali ufahamu kutoka kwa viongozi wa watu wa nchi; huwafanya wao kutangatanga msituni mahali pasipo na njia.
25 They grope in the dark without light. He makes them stagger like a drunken man.
Wao wanapapasa katika giza bila kuwa na mwanga; yeye huwafanya wao kuweweseka kama mtu mlevi.

< Job 12 >