< Exodus 11 >

1 The LORD said to Moses, “I will bring yet one more plague on Pharaoh, and on Egypt; afterwards he will let you go. When he lets you go, he will surely thrust you out altogether.
Kisha Yahweh akamwambia Musa, “Bado kuna pigo moja nitalo lileta kwa Farao na Misri. Baada ya hilo, atakuacha uondoke hapa. Atakapo kuachia uende, ata kuondoa kabisa.
2 Speak now in the ears of the people, and let every man ask of his neighbor, and every woman of her neighbor, jewels of silver, and jewels of gold.”
Waelekeze watu kwamba kila mwanaume na mwanamke amuulizie jirani yake vitu vya fedha na vitu vya dhahabu.”
3 The LORD gave the people favor in the sight of the Egyptians. Moreover, the man Moses was very great in the land of Egypt, in the sight of Pharaoh’s servants, and in the sight of the people.
Sasa Yahweh aliwafanya Wamisri kuwa na shauku ya kuwapendeza Waisraeli. Aidha, Musa alikuwa wakuvutia sana machoni pa watumishi wa Farao na watu wa Misri.
4 Moses said, “This is what the LORD says: ‘About midnight I will go out into the middle of Egypt,
Musa akasema, “Yahweh asema hivi: 'Wakati wa usiku wa manane nitaenda Misri yote.
5 and all the firstborn in the land of Egypt shall die, from the firstborn of Pharaoh who sits on his throne, even to the firstborn of the female servant who is behind the mill, and all the firstborn of livestock.
Wazaliwa wa kwanza wote wa nchi ya Misri watakufa, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, anaye keti kiti chake cha enzi, mpaka mzaliwa wa kwanza wa misichana mtumwa anaye saga mbegu, na kwa wazaliwa wa kwanza wa mifugo.
6 There will be a great cry throughout all the land of Egypt, such as there has not been, nor will be any more.
Kisha kutakuwa na kilio kikubwa nchi yote ya Misri, kama ambacho hakijawai wala hakitatokea tena.
7 But against any of the children of Israel a dog won’t even bark or move its tongue, against man or animal, that you may know that the LORD makes a distinction between the Egyptians and Israel.
Lakini ata mbwa hata bweka kwa watu wa Israeli, dhidi ya mtu au mnyama. Kwa hili utajuwa kuwa nina watendea Wamisri na Waisraeli tofauti.'
8 All these servants of yours will come down to me, and bow down themselves to me, saying, “Get out, with all the people who follow you;” and after that I will go out.’” He went out from Pharaoh in hot anger.
Watumishi wote hawa wako, Farao, watakuja chini yangu na kunisujudu mimi. Watasema, 'Nenda, wewe na watu wote wanao kufuata!' Baada ya hapo nitaondoka.” Kisha akaondoka mbele ya Farao kwa hasira kubwa.
9 The LORD said to Moses, “Pharaoh won’t listen to you, that my wonders may be multiplied in the land of Egypt.”
Yahweh akamwambia Musa, Farao hatakusikiliza. Hii ni ili nifanye mambo ya ajabu katika nchi ya Misri.”
10 Moses and Aaron did all these wonders before Pharaoh, but the LORD hardened Pharaoh’s heart, and he didn’t let the children of Israel go out of his land.
Musa na Aruni wakafanya mambo haya ya kushangaza mbele za Farao. Lakini Yahweh aliufanya moyo wa Farao mgumu, na Farao hakuwaacha watu wa Israeli kuondoka katika nchi yake.

< Exodus 11 >