< 1 Corinthians 12 >

1 Now concerning spiritual things, brothers, I don’t want you to be ignorant.
Kuhusu karama za rohoni, kaka na dada zangu sitaki mkose kufahamu.
2 You know that when you were heathen, you were led away to those mute idols, however you might be led.
Mwajua ya kuwa mlipokuwa wapagani mliongozwa kufuata sanamu zisizoongea, kwa njia zozote mliongozwa nazo.
3 Therefore I make known to you that no man speaking by God’s Spirit says, “Yeshua is accursed.” No one can say, “Yeshua is Lord,” but by the Holy Spirit.
Kwa hiyo, nataka mfahamu kwamba hakuna yeyote anenaye kwa Roho wa Mungu akisema, “Yesu amelaaniwa.” Hakuna yeyote atakayesema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa katika Roho Mtakatifu.
4 Now there are various kinds of gifts, but the same Spirit.
Basi kuna karama tofauti tofauti, bali Roho ni yeye yule.
5 There are various kinds of service, and the same Lord.
Na kuna huduma tofauti tofauti, bali Bwana ni yeye yule.
6 There are various kinds of workings, but the same God who works all things in all.
Na kuna aina mbalimbali za kazi, lakini Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.
7 But to each one is given the manifestation of the Spirit for the profit of all.
Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote.
8 For to one is given through the Spirit the word of wisdom, and to another the word of knowledge according to the same Spirit,
Maana mtu mmoja amepewa na Roho neno la hekima, na mwingine neno la maarifa kwa Roho yule yule.
9 to another faith by the same Spirit, and to another gifts of healings by the same Spirit,
Kwa mwingine humpa imani kwa Roho yeye yule, na kwa mwingine karama ya uponyaji kwa Roho mmoja.
10 and to another workings of miracles, and to another prophecy, and to another discerning of spirits, to another different kinds of languages, and to another the interpretation of languages.
Kwa mwingine matendo ya nguvu, na mwingine unabii. Na kwa mwingine uwezo wa kupambanua roho, mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingnine tafsiri za lugha.
11 But the one and the same Spirit produces all of these, distributing to each one separately as he desires.
Lakini Roho ni yule yule atendaye kazi hizi zote, kumpa kila mtu karama kwa kadiri ya uchaguzi wake mwenyewe.
12 For as the body is one and has many members, and all the members of the body, being many, are one body; so also is Messiah.
Kwa maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote ni vya mwili ule ule, vivyo hivyo na Kristo.
13 For in one Spirit we were all immersed into one body, whether Jews or Greeks, whether bond or free; and were all given to drink into one Spirit.
Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi au Wayunani, kwamba tu watumwa au huru, na wote tulinyweshwa Roho mmoja.
14 For the body is not one member, but many.
Kwa maana mwili si kiungo kimoja, bali ni vingi.
15 If the foot would say, “Because I’m not the hand, I’m not part of the body,” it is not therefore not part of the body.
Ikiwa mguu utasema, “kwa kuwa mimi si mkono, mimi si sehemu ya mwili,” hiyo haiufanyi kutokuwa sehemu ya mwili.
16 If the ear would say, “Because I’m not the eye, I’m not part of the body,” it’s not therefore not part of the body.
Na ikiwa sikio litasema, “kwa kuwa mimi si jicho, mimi si sehemu ya mwili,” hiyo hailifanyi kutokuwa sehemu ya mwili.
17 If the whole body were an eye, where would the hearing be? If the whole were hearing, where would the smelling be?
Kama mwili wote utakuwa jicho, kungekuwa wapi kusikia? Kama mwili wote ukiwa sikio, kungekuwa wapi kunusa?
18 But now God has set the members, each one of them, in the body, just as he desired.
Lakini Mungu aliweka kila kiungo cha mwili mahali pake kama alivyopanga mwenyewe.
19 If they were all one member, where would the body be?
Na kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20 But now they are many members, but one body.
Hivyo sasa viungo ni vingi, lakini mwili ni mmoja.
21 The eye can’t tell the hand, “I have no need for you,” or again the head to the feet, “I have no need for you.”
Jicho haliwezi kuuambia mkono, “sina haja na wewe.” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, sina haja na ninyi.”
22 No, much rather, those members of the body which seem to be weaker are necessary.
Lakini viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa na heshima kidogo vyahitajika zaidi.
23 Those parts of the body which we think to be less honorable, on those we bestow more abundant honor; and our unpresentable parts have more abundant modesty,
Na viungo vya mwili tunavyodhani vina heshima kidogo, twavipa heshima zaidi, na viungo vyetu visivyo na mvuto vina uzuri zaidi.
24 while our presentable parts have no such need. But God composed the body together, giving more abundant honor to the inferior part,
Na sasa viungo vyetu vilivyo na mvuto havina haja ya kupewa heshima, kwa kuwa tayari vina heshima. Lakini Mungu ameviunganisha viungo vyote pamoja, na amevipa heshima zaidi vile visivyo heshimiwa.
25 that there should be no division in the body, but that the members should have the same care for one another.
Alifanya hivyo ili pasiwepo mgawanyiko katika mwili, bali viungo vyote vitunzane kwa upendo wa mmoja.
26 When one member suffers, all the members suffer with it. When one member is honored, all the members rejoice with it.
Na wakati kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote vyaumia kwa pamoja. Au wakati kiungo kimoja kikiheshimiwa, viungo vyote vifurahi kwa pamoja.
27 Now you are the body of Messiah, and members individually.
Sasa ninyi ni mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.
28 God has set some in the assembly: first emissaries, second prophets, third teachers, then miracle workers, then gifts of healings, helps, governments, and various kinds of languages.
Na Mungu ameweka katika kanisa kwanza mitume, pili manabii, tatu waalimu, kisha wale wote watendao matendo makuu, kisha karama za uponyaji, wale wasaidiao, wale wafanyao kazi ya kuongoza, na wote walio na aina mbalimbali za lugha.
29 Are all emissaries? Are all prophets? Are all teachers? Are all miracle workers?
Je sisi sote ni mitume? Sisi sote ni manabii? Sisi sote ni waalimu? Je sisi sote tunafanya matendo ya miujiza?
30 Do all have gifts of healings? Do all speak with various languages? Do all interpret?
Je sisi sote tuna karama ya uponyaji? Sisi sote tunaongea kwa lugha? Sisi sote tunatafsiri lugha?
31 But earnestly desire the best gifts. Moreover, I show a most excellent way to you.
Tafuteni sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonesha njia iliyo bora zaidi.

< 1 Corinthians 12 >