< 1 Chronicles 11 >

1 Then all Israel gathered themselves to David to Hebron, saying, “Behold, we are your bone and your flesh.
Kisha Waisraeli wote walikuja Hebroni kwa Daudi na kusema, “Angalia, sisi ni nyama na mifupa yako.
2 In times past, even when Saul was king, it was you who led out and brought in Israel. The LORD your God said to you, ‘You shall be shepherd of my people Israel, and you shall be prince over my people Israel.’”
Katika wakati uliopita, Sauli alipoo kuwa mfalme juu yetu, ni wewe uliye ongoza jeshi la Israeli. Yahweh Mungu wako alisema kwako, 'utawachunga watu wangu wa Isaraeli, na utakuwa mtawala wa watu wangu wa Israeli”'.
3 So all the elders of Israel came to the king to Hebron; and David made a covenant with them in Hebron before the LORD. They anointed David king over Israel, according to the LORD’s word by Samuel.
Kwaiyo wazee wote wa Israeli wakamjia mfalme huko Hebroni, na Daudi akafanya agano nao mbele ya Yahweh. Wakampaka mafuta Daudi kuwa mfalme wa Israeli. Kwa namna hii, neno la Yahweh lilo nenwa na Samweli likawa kweli.
4 David and all Israel went to Jerusalem (also called Jebus); and the Jebusites, the inhabitants of the land, were there.
Daudi na Israeli yote wakaenda Yerusalemu (yani, Yebusi). Sasa Wayebusi, wakazi wa nchi, walikuwa pale.
5 The inhabitants of Jebus said to David, “You will not come in here!” Nevertheless David took the stronghold of Zion. The same is David’s city.
Wakazi wa yebusi wakamwabia Daudi, “Hautakuja humu.” Lakini Daudi alichukuwa ngome ya Sayuni, mji wa Daudi.
6 David had said, “Whoever strikes the Jebusites first shall be chief and captain.” Joab the son of Zeruiah went up first, and was made chief.
Daudi alisema, “Yeyote atakaye washambulia Wayebusi wa kwanza atakuwa mkuu wa jeshi” kwaiyo Yoabu mwana wa Zeruia akashambulia wa kwanza, hivyo akafanywa mkuu wa jeshi.
7 David lived in the stronghold; therefore they called it David’s city.
Daudi akaanza kuishi katika hiyo ngome. Kwaiyo wakaiita mji wa Daudi.
8 He built the city all around, from Millo even around; and Joab repaired the rest of the city.
Akaimarisha mji kutoka Milo na hadi mpaka ukuta unao zunguka. Yoabu akaimairisha mji wote uliyo baki.
9 David grew greater and greater, for the LORD of Hosts was with him.
Daudi akawa mkuu na mkuu kwa sababu Yahweh wa Majeshi alikuwa naye.
10 Now these are the chief of the mighty men whom David had, who showed themselves strong with him in his kingdom, together with all Israel, to make him king, according to the LORD’s word concerning Israel.
Hawa walikuwa viongozi Daudi aliyo kuwa nao, waliyo jionyesha imara katika ufalme wake, pamoja na Israeli, kumfanya mfalme, kutii neno la Yahweh kuhusu Israeli.
11 This is the number of the mighty men whom David had: Jashobeam, the son of a Hachmonite, the chief of the thirty; he lifted up his spear against three hundred and killed them at one time.
Hii ni orodha ya wanajeshi shupavu wa Daudi. Yashobeami, mwana wa Mhakimoni, alikuwa mkuu wa kikosi cha thelathini. Aliwaua wanaume mia tatu na mkuki wake katika sehemu moja.
12 After him was Eleazar the son of Dodo, the Ahohite, who was one of the three mighty men.
Baada ya yeye alikuwa Eleazari mwana wa Dodo, Mahohi, aliyekuwa mmoja wa wanaume watatu hodari.
13 He was with David at Pasdammim, and there the Philistines were gathered together to battle, where there was a plot of ground full of barley; and the people fled from before the Philistines.
Alikuwa na Daudi huko Pasidamimu, na pale Wafilisti wakakusanyika pamoja kwa mapambano, ambapo palikuwa na uwanja wa ngano na jeshi liliwakimbia Wafilisti.
14 They stood in the middle of the plot, defended it, and killed the Philistines; and the LORD saved them by a great victory.
Walisimama katikati ya uwanja. Wakautetea na kuwakata Wafilisti na Yahweh akawaokoa na ushindi mkubwa.
15 Three of the thirty chief men went down to the rock to David, into the cave of Adullam; and the army of the Philistines were encamped in the valley of Rephaim.
Kisha watatu wa viongozi thelathini wakashuka chini kwenye mwamba wa Daudi, katika pango la Adulamu. Jeshi la Wafilisti walieka kambi katika bonde la Refaim.
16 David was then in the stronghold, and the garrison of the Philistines was in Bethlehem at that time.
Kwa wakati huo Daudi alikuwa katika ngome yake, pangoni, Wafilisti walikita kambi yao Bethilehemu.
17 David longed, and said, “Oh, that someone would give me water to drink from the well of Bethlehem, which is by the gate!”
Daudi alikuwa na kiu ya maji na akasema, “Laiti mtu akanipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho Bethilehemu, kisima kilicho pembeni mwa lango!”
18 The three broke through the army of the Philistines, and drew water out of the well of Bethlehem that was by the gate, took it, and brought it to David; but David would not drink any of it, but poured it out to the LORD,
Hawa wanaume hodari watatu wakatoboa kupita jeshi la Wafilisti na kuchota maji kwenye kisima cha Bethilehemu, kisima pembeni mwa lango. Wakachukuwa maji na kumletea Daudi, lakini alikataa kunywa. Badala yake, akamwaga chini kwa Yahweh.
19 and said, “My God forbid me, that I should do this! Shall I drink the blood of these men who have put their lives in jeopardy?” For they risked their lives to bring it. Therefore he would not drink it. The three mighty men did these things.
Kisha akasema, “Yahweh, iwe mbali na mimi, kwamba ni yanywe haya maji. Je ninywe damu ya wanaume walio hatarisha maisha yao?” Kwa sababu wameeka maisha ya hatarini, akakataa kunywa. Haya ni mambo wanaume hodari watatu walio fanya.
20 Abishai, the brother of Joab, was chief of the three; for he lifted up his spear against three hundred and killed them, and had a name among the three.
Abishai kaka wa Yoabu, alikuwa kiongozi wa watatu. Alitumia mkuki wake dhidi ya watu mia tatu na kuwaua. Ametajwa pamoja na wale watatu.
21 Of the three, he was more honorable than the two, and was made their captain; however he wasn’t included in the three.
Kati ya wale watatu, yeye alipewa heshima mara mbili na akawa kiongozi wao. Japo hakuwa mmoja wa miongoni mwao.
22 Benaiah the son of Jehoiada, the son of a valiant man of Kabzeel, who had done mighty deeds, killed the two sons of Ariel of Moab. He also went down and killed a lion in the middle of a pit on a snowy day.
Benaia mwana wa Yehoiada alikuwa mwanaume mwenye nguvu aliye fanya mambo makuu. Aliua wana wawili wa Arieli wa Moabu. Pia alishuka chini ya shimo na kumuua simba wakati theluji ikianguka.
23 He killed an Egyptian, a man of great stature, five cubits high. In the Egyptian’s hand was a spear like a weaver’s beam; and he went down to him with a staff, plucked the spear out of the Egyptian’s hand, and killed him with his own spear.
Alimua hadi Mmisri, mwanaume mwenye mita mbili na theluthi moja. Mmisri alikuwa na mkuki kama gongo la mshonaji, lakini alimfuata chini na fimbo tu. Akakamata mkuki katika mkono wa Mmisri na kumuua na mkuki wake.
24 Benaiah the son of Jehoiada did these things and had a name among the three mighty men.
Benaia mwana wa Yehoiada alifanya haya matukio, na akatajwa miongoni mwa wale wanaume hodari watatu.
25 Behold, he was more honorable than the thirty, but he didn’t attain to the three; and David set him over his guard.
Alisifika zaidi ya wale wanajeshi thelathini kwa ujumla, lakini hakuwa pewa hadhi ya wale wanajeshi watatu hodari. Daudi alimueka kiongozi wa walinzi wake.
26 The mighty men of the armies also include Asahel the brother of Joab, Elhanan the son of Dodo of Bethlehem,
Wanaume hodari walikuwa Asaheli kaka wa Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo wa Bethilehemu,
27 Shammoth the Harorite, Helez the Pelonite,
Shamothi Mherori, Helezi Mpeloni,
28 Ira the son of Ikkesh the Tekoite, Abiezer the Anathothite,
Ira mwana wa Ikeshi Mtekoi, Abi Eza Manathothi,
29 Sibbecai the Hushathite, Ilai the Ahohite,
Sibekai Mhushathite, Ilai Mahohite,
30 Maharai the Netophathite, Heled the son of Baanah the Netophathite,
Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana Mnetofathite,
31 Ithai the son of Ribai of Gibeah of the children of Benjamin, Benaiah the Pirathonite,
Itai mwana wa Ribai wa Gibea uzao wa Benjamini, Benaia Mpirathoni,
32 Hurai of the brooks of Gaash, Abiel the Arbathite,
Hurai wa mabonde ya Gaashi, Abieli Marbathi,
33 Azmaveth the Baharumite, Eliahba the Shaalbonite,
Azmavethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
34 the sons of Hashem the Gizonite, Jonathan the son of Shagee the Hararite,
Mwana wa Hashemu Mgizoni, Yonathani mwana wa Shagee Mhararite,
35 Ahiam the son of Sacar the Hararite, Eliphal the son of Ur,
Ahiamu mwana wa Sacari Mhararite, Elifali mwana wa Uri,
36 Hepher the Mecherathite, Ahijah the Pelonite,
Hefa Mmekarathi, Ahija Mpeloni,
37 Hezro the Carmelite, Naarai the son of Ezbai,
Hezro Mcarmeli, Maarai mwana wa Ezibai,
38 Joel the brother of Nathan, Mibhar the son of Hagri,
Yoeli kaka wa Nathani, Mibhari mwana wa Hagiri,
39 Zelek the Ammonite, Naharai the Berothite (the armor bearer of Joab the son of Zeruiah),
Zeleki Mamoni, Naharai Mberothi ( mbeba ngao ya Yoabu mwana wa Zeruia),
40 Ira the Ithrite, Gareb the Ithrite,
Ira Mithire, Garebu Mithire,
41 Uriah the Hittite, Zabad the son of Ahlai,
Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Ahlai,
42 Adina the son of Shiza the Reubenite (a chief of the Reubenites), and thirty with him,
Adina mwana wa Shiza Mreubeni ( kiongozi wa Wareubeni) na thelathini pamoja nae,
43 Hanan the son of Maacah, Joshaphat the Mithnite,
Hanani mwana wa Maaka, na Yoshafati Mmithini,
44 Uzzia the Ashterathite, Shama and Jeiel the sons of Hotham the Aroerite,
Uzia Mashiterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Waaroeri,
45 Jediael the son of Shimri, and Joha his brother, the Tizite,
Jediaeli mwana wa Shimri, Joha ( kaka yake Mtize),
46 Eliel the Mahavite, and Jeribai, and Joshaviah, the sons of Elnaam, and Ithmah the Moabite,
Elieli Mmahavi, Yeribai na Yoshavia mwana wa Elnaamu, Ithima Mmoabi,
47 Eliel, Obed, and Jaasiel the Mezobaite.
Elieli, Obedi, na Yaasieli Wamezobai.

< 1 Chronicles 11 >